07/07/2023
_Wamefika hapa kwakuwa hakuendekeza tamaa za ujana kutaka kunufaika na kijana bali alijua atakacho_Yeye alikuwa anaomba amtumie kijana wa ndoto zake angalau hata ya matumizi_Ndoa ilipofungwa aliendelea na tabia zake zilezile za wakati wa uchumba hakuota kiburi kwamba tayari meli imetia nanga. Gentlemen hata alipochepuka alijutia pia hakusahau k**a ana mke nyumbani na wala hakumdharau alipo beba ujauzito . Waliendelea kupendana hata walipo pitia wakati wa ukata wa fedha, dhahiri shairi Abadani wakabembelezana walipolala njaa . Alipokuwa binti alijidhatiti kwamba hata aje mwenye Range au Barack Obama kumtaka asingaliweza kukubali , Na Mungu hakuacha kusikiliza ombi lao *masikini huyu aliita Bwana kamsikiliza* leo hii ukiwatazama k**a filamu zenye behind the scenes kumbe ni real na kuongeza kuwa ni reality . Mwanzo hakuna aliyeamini k**a watafika?,Hata wazazi walikuwa pingamizi kwani walitaka binti yao aolewe na tajiri mwenye hadhi k**a wao lakini _true love never ask why_binti kakataa kumsikiliza baba yake aliyesababu ya uwepo wake &mama yake miezi 9 tumboni.
Kwakuwa walikuwa na upendo wa dhati hawakuwa na haja ya kuogopa laana ya wazazi kwakuwa waliamini kuwa upendo wao ni Mungu kawakutanisha ila wao waliamini upinzani wa wazazi ni tamaa ya mali za dunia , Hawakujua usemi usemao hakuna mzazi anayependa mwanae ateseke. Wakakubali kupata laana na kutengwa na familia ya upande wa mwanamke kutokana na umaskini wa kijana mwenye kumuoa binti wa familia ya kitajiri .
Leo hii hakuna anayeamini miujiza iliyotendeka katika ndoa ya vijana hao iliyofungwa na watu kidogoo ikiwa inatimiza miaka tisini na kenda huku ikiwa ni sehemu ya vijana wengine kwenda kutalii k**a kivutio na kuchota hekima . Wakiuliza maswali mengi imekuwaje mmefikia katika umri huu mkiwa pamoja ?, Hamjakumbwa na changamoto? . Wao walijibu hakuna maisha yanayo kosa changamoto ila tulimtanguliza Mungu kuwa sehemu ya maisha yetu hatukumkimbilia tuu wakati wa shida hata ule wa furaha , tulipokoseana tuliombana msamaha na ndio ilikuwa jadi ya maisha yetu. Tuziombee ndoa zinazo vunjika Mungu aingilie kati wazazi walee watoto pamoja na kukumbuka agano lao . Mali isiwe kigezo cha ndoa kuvunjika bali upendo utamalaki kati yao .
Ee Mungu zitazame ndoa uzijalie upendo usio na mipaka k**a ile ya Familia Takatifu ya Yesu , Maria na Yosef . Amina