06/20/2026
Kutafuta usalama ni haki ya kila mtu.
Kwa mamilioni ya wakimbizi, usalama unamaanisha mahali pa kulala kwa amani, mtoto kurudi shuleni, familia kubaki pamoja na nafasi ya kuanza upya.
Jumamosi Siku ya Wakimbizi Duniani, tunasimama pamoja na watu wote waliolazimika kuyakimbia makazi yao.
Kwa sababu haki ya kutafuta usalama ni haki ya binadamu.
Mpaka kila mmoja awe salama, kazi bado haijaisha.