Umoja wa Mataifa

Umoja wa Mataifa Akaunti rasmi ya Umoja wa Mataifa. Kwa amani, utu & usawa katika ulimwengu wenye ustawi.

Kuvuta sigara huua. 🚭Tumbaku husababisha vifo vya takribani watu milioni 8 kila mwaka, wakiwemo zaidi ya milioni 1 wanao...
05/31/2026

Kuvuta sigara huua. 🚭

Tumbaku husababisha vifo vya takribani watu milioni 8 kila mwaka, wakiwemo zaidi ya milioni 1 wanaofariki kutokana na kuvuta moshi wa sigara kutoka kwa wengine.

Kuacha kuvuta kunawezekana, na kadri unavyokaa bila tumbaku, ndivyo afya yako inavyozidi kuimarika.

✅ Chagua tarehe ya kuacha kuvuta
✅ Mwambie mtu unayemwamini
✅ Zungumza na mhudumu wa afya
✅ Badili mazoea hayo kwa shughuli yenye afya zaidi

Jumapili ni .

- kupitia

📍DRC“Hamko peke yenu.”Akiwa Bunia, mashariki mwa DRC, Mkurugenzi Mkuu wa World Health Organization (WHO) , Dkt. Tedros A...
05/31/2026

📍DRC

“Hamko peke yenu.”

Akiwa Bunia, mashariki mwa DRC, Mkurugenzi Mkuu wa World Health Organization (WHO) , Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus , amewahakikishia wananchi wanaokabiliana na mlipuko wa Ebola kuwa hawajasahaulika.

Amesisitiza umuhimu wa kuzijumuisha jamii katika juhudi za kukabiliana na mlipuko huo, akieleza kuwa ushirikiano na imani ya wananchi ni muhimu katika kudhibiti ugonjwa huo.

“Tupo hapa. Tupo pamoja nanyi. Na tutapitia changamoto hii pamoja.”

Zaidi: https://news.un.org/sw/story/2026/05/1192611

Takribani wanajeshi na maafisa wa polisi 700 kutoka   wanahudumu katika operesheni nne za United Nations Peacekeeping du...
05/30/2026

Takribani wanajeshi na maafisa wa polisi 700 kutoka wanahudumu katika operesheni nne za United Nations Peacekeeping duniani.

Wakiwa mbali na familia zao na mara nyingi katika mazingira magumu na hatarishi, wanaendelea kuhudumu kwa ajili ya amani na kusaidia wale wanaohitaji zaidi.

Tunawatambua na kuwashukuru kwa huduma na kujitolea kwao.

Viazi ni zaidi ya chakula.Kwa mabilioni ya watu duniani, ni sehemu ya lishe ya kila siku. Kwa wakulima wengi, ni chanzo ...
05/30/2026

Viazi ni zaidi ya chakula.

Kwa mabilioni ya watu duniani, ni sehemu ya lishe ya kila siku. Kwa wakulima wengi, ni chanzo cha kipato na maisha.

Katika Siku ya Kimataifa ya Viazi, tunaangazia mchango wake katika usalama wa chakula duniani. https://www.fao.org/international-potato-day/en

Wape wakulima wa viazi neno moja!

Mlipuko wa   nchini DRC unaendelea kuathiri maisha ya maelfu ya watu ambao tayari wanakabiliwa na vita, njaa na ukosefu ...
05/29/2026

Mlipuko wa nchini DRC unaendelea kuathiri maisha ya maelfu ya watu ambao tayari wanakabiliwa na vita, njaa na ukosefu wa makazi.

Familia nyingi zinahitaji msaada wa haraka, kutoka chakula na maji safi hadi huduma za afya na vifaa vya kujikinga.

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kuongeza juhudi za kuwafikia walioathirika na kuokoa maisha.

Tangu mwaka 1948, zaidi ya wanawake na wanaume milioni 2 wa United Nations Peacekeeping  wamehudumu katika baadhi ya mae...
05/29/2026

Tangu mwaka 1948, zaidi ya wanawake na wanaume milioni 2 wa United Nations Peacekeeping wamehudumu katika baadhi ya maeneo yenye changamoto kubwa duniani.

Kila siku, wanasaidia kulinda raia, kuunga mkono amani, kufikisha misaada ya kibinadamu na kusaidia jamii zilizoathiriwa na migogoro.

Katika Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa, tunawatambua na kuwashukuru kwa huduma na kujitolea kwao kwa ajili ya dunia yenye amani zaidi. https://www.un.org/en/observances/peacekeepers-day

Hedhi ni sehemu ya kawaida ya maisha, si jambo la aibu.Lakini watu wengi duniani bado hawana bidhaa salama za hedhi au s...
05/28/2026

Hedhi ni sehemu ya kawaida ya maisha, si jambo la aibu.

Lakini watu wengi duniani bado hawana bidhaa salama za hedhi au sehemu nzuri za kujisitiri na kujihudumia.

Katika , tuvunje ukimya na unyanyapaa kuhusu hedhi.

Angalia kazi inayofanywa na UNFPA: https://www.unfpa.org/menstrual-health

Barua ya kibinafsi kutoka kwa Mkuu wa , Dkt. , kwa watu wa DRC, hasa Ituri wakati wa mlipuko wa  .“Hamko peke yenu.”Amep...
05/28/2026

Barua ya kibinafsi kutoka kwa Mkuu wa , Dkt. , kwa watu wa DRC, hasa Ituri wakati wa mlipuko wa .

“Hamko peke yenu.”

Amepongeza ujasiri wa wahudumu wa afya na jamii zinazoendelea kupambana kuokoa maisha katika mazingira magumu, huku akitoa wito wa usitishaji wa mapigano ili misaada iweze kufika kwa wanaohitaji.

Afya ya akili ni muhimu k**a afya ya mwili. 🏃🏽 Fanya mazoezi mara kwa mara🥗 Kula vyakula vyenye lishe😴 Pata muda wa kupu...
05/27/2026

Afya ya akili ni muhimu k**a afya ya mwili.

🏃🏽 Fanya mazoezi mara kwa mara
🥗 Kula vyakula vyenye lishe
😴 Pata muda wa kupumzika
🗣 Zungumza kuhusu hisia zako
🤝 Tafuta msaada unapouhitaji

Address

New York, NY
10017

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Umoja wa Mataifa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share