Umoja wa Mataifa

Umoja wa Mataifa Akaunti rasmi ya Umoja wa Mataifa. Kwa amani, utu & usawa katika ulimwengu wenye ustawi.

Kutafuta usalama ni haki ya kila mtu.Kwa mamilioni ya wakimbizi, usalama unamaanisha mahali pa kulala kwa amani, mtoto k...
06/20/2026

Kutafuta usalama ni haki ya kila mtu.

Kwa mamilioni ya wakimbizi, usalama unamaanisha mahali pa kulala kwa amani, mtoto kurudi shuleni, familia kubaki pamoja na nafasi ya kuanza upya.

Jumamosi Siku ya Wakimbizi Duniani, tunasimama pamoja na watu wote waliolazimika kuyakimbia makazi yao.

Kwa sababu haki ya kutafuta usalama ni haki ya binadamu.

Mpaka kila mmoja awe salama, kazi bado haijaisha.

Jana.Leo.Kesho.Na siku zote.Hadi kila mtu awe salama, tutaendelea kusimama pamoja na wakimbizi.- UNHCR, the UN Refugee A...
06/20/2026

Jana.
Leo.
Kesho.
Na siku zote.

Hadi kila mtu awe salama, tutaendelea kusimama pamoja na wakimbizi.

- UNHCR, the UN Refugee Agency

Kuelekea   Jumapili, watu wengi walikusanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kushiriki mazoezi ya...
06/19/2026

Kuelekea Jumapili, watu wengi walikusanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kushiriki mazoezi ya yoga. 🧘

Mazoezi haya ya kale huunganisha mwili na akili, na huchangia afya ya akili na utulivu wa ndani.

Leo, yoga imeenea duniani kote na inaendelea kuvutia watu zaidi.

“Wanawake wanapokuwa salama, jamii huwa na amani zaidi.”Akilihutubia Baraza la Usalama, Mkuu wa  Women Sima Bahous amese...
06/19/2026

“Wanawake wanapokuwa salama, jamii huwa na amani zaidi.”

Akilihutubia Baraza la Usalama, Mkuu wa Women Sima Bahous amesema wanawake wanapaswa kuwa na nafasi muhimu katika juhudi za kujenga amani.

“Wanawake wanaposhiriki katika kufanya maamuzi, amani hupatikana kwa haraka zaidi na huwa na uwezekano mkubwa wa kudumu.”

Usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake ni msingi wa amani ya kudumu.

Kadri migogoro inavyozidi kuongezeka duniani, wasichana na wavulana wengi zaidi wanakabiliwa na ubakaji, utumwa wa kingo...
06/19/2026

Kadri migogoro inavyozidi kuongezeka duniani, wasichana na wavulana wengi zaidi wanakabiliwa na ubakaji, utumwa wa kingono, ndoa za kulazimishwa na usafirishaji haramu.

Katika Siku ya Kimataifa ya Kukomesha Ukatili wa Kijinsia katika Migogoro, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres anatoa wito wa kukomesha uhalifu huu wa kutisha, kuwalinda watoto, kuwawajibisha wahusika na kuzuia mateso zaidi.

Wakati wa ziara yake nchini Haiti jana, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alikutana na wanawake na wanaum...
06/18/2026

Wakati wa ziara yake nchini Haiti jana, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alikutana na wanawake na wanaume wa Kikosi cha Kukabiliana na Magenge.

Amesema kuwasili kwa kikosi hicho kunatoa fursa muhimu ya kupunguza ghasia, kurejesha usalama na kuwapa wananchi matumaini mapya.

Kwa sasa, ghasia za magenge zinaendelea kudhoofisha maisha ya kila siku nchini Haiti, kuathiri uchumi, elimu na utoaji wa misaada ya kibinadamu.

Chuki haianzi kwa vurugu.Huanzia kwenye maneno.Katika Siku ya Kimataifa ya Kupinga Matamshi ya Chuki, Katibu Mkuu wa Umo...
06/18/2026

Chuki haianzi kwa vurugu.

Huanzia kwenye maneno.

Katika Siku ya Kimataifa ya Kupinga Matamshi ya Chuki, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameonya kuwa matamshi ya chuki yanaweza kuwa hatua ya kwanza ya kuwavua wengine utu wao.

Tukatae ubaguzi na chuki katika aina zake zote.

06/17/2026

📍Haiti

"Haiti kwa sasa inakabiliwa na moja ya migogoro mikubwa zaidi ya kibinadamu katika eneo la Amerika.

Leo, zaidi ya nusu ya wananchi wa Haiti - takribani watu milioni 6.4 - wanahitaji msaada wa kibinadamu. Wanawake na watoto ndio wanaoathirika zaidi.

Nimekutana na familia ambazo zimepoteza kila kitu, lakini bado zinaendelea kusimama imara kwa ujasiri na utu wa kipekee. Ustahimilivu wao umenigusa sana.

Familia hizi haziombi huruma kutoka kwa dunia.

Zinasubiri hatua."

- António Guterres, baada ya kutembelea kituo cha watu waliolazimika kuhama makazi yao mjini Port-au-Prince, Haiti.

📍Haiti"Nimekuja Haiti na ujumbe mmoja rahisi: hamko peke yenu.”Akiwa katika kambi ya watu waliolazimika kuyakimbia makaz...
06/17/2026

📍Haiti

"Nimekuja Haiti na ujumbe mmoja rahisi: hamko peke yenu.”

Akiwa katika kambi ya watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesisitiza umuhimu wa kuongeza msaada kwa Wahaiti wanaokabiliwa na vurugu na ukatili wa magenge halifu, uhaba wa chakula, ukosefu wa usalama na kuhama makazi.

“Huu ndio wakati ambao jumuiya ya kimataifa inapaswa kujitokeza na kuchukua hatua.”

"Haki za binadamu zinafanya kazi, hata pale zisipopewa vichwa vya habari."Akizungumza mbele ya Baraza la Haki za Binadam...
06/16/2026

"Haki za binadamu zinafanya kazi, hata pale zisipopewa vichwa vya habari."

Akizungumza mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Mkuu wa United Nations Human Rights Volker Türk alisema haki za binadamu zinaendelea kubadilisha maisha, kupunguza migawanyiko na kupanua uhuru wa watu duniani.

Hata hivyo, alionya kuhusu "changamoto kubwa za haki za binadamu" na "mashambulizi yasiyo na aibu dhidi ya sheria za kimataifa" yanayosababisha mateso makubwa ya kibinadamu.

"Ni lazima tuyakemee kila wakati na kila mahali, na tufanye kazi ya kuyadhibiti na kuyakomesha."

Address

New York, NY
10017

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Umoja wa Mataifa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share