Piro Zanzibar

Piro Zanzibar PIRO Zanzibar. Inajishughilisha na Kuwasaidia Wanawake na Vijana katika Afya ya Uzazi Jamii, Elimu ya Uchumi wa Buluu na Mazingira. Biashara na Ujasiriamali.

Kusimamia Vikundi Vya Hisa Vya Vijana (YSLA.)

01/06/2026

Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani. PIRO imefanikisha zoezi la Upandaji wa Miti

THE POPULAR INSPIRNG AND RELIEF ORGANIZATION (PIRO) YAONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZI...
01/06/2026

THE POPULAR INSPIRNG AND RELIEF ORGANIZATION (PIRO) YAONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI 2026
Katika kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoadhimishwa kila tarehe 5 Juni, Taasisi ya The Popular Inspiring and Relief Organization (PIRO) leo imeungana na Wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali katika Bwawa la Kisongoni, Mkoa wa Kaskazini Unguja, kufanya zoezi kubwa la upandaji miti kwa lengo la kuendeleza Zanzibar ya Kijani na kulinda mazingira yetu.
Katika shughuli hiyo, PIRO imefanikiwa kupanda miti zaidi ya 15,000 ya aina mbalimbali ikiwemo Mivinje, Mikungu, Mitondoo, Mianzi, Jakaranda, Mikristimasi, Cedrela na Pongamia. Zoezi hili limeambatana na utoaji wa elimu ya mazingira kwa jamii na wanafunzi ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji.
"Mazingira ndiyo maisha yetu."
Kupanda miti ni hatua muhimu katika kuimarisha uoto wa asili, kuhifadhi vyanzo vya maji, kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi, kuboresha ubora wa hewa na kutengeneza makazi salama kwa viumbe hai.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Kanda wa PIRO alisema:
"Katika kuadhimisha World Environment Day, tunawakumbusha wananchi wote kuwa mazingira si jambo la hiari bali ni msingi wa uhai wetu. Dunia inakabiliwa na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, uchafuzi wa mazingira na uharibifu wa misitu. Hatuwezi kubaki watazamaji; kila mmoja ana wajibu wa kuchukua hatua kwa kupanda miti, kupunguza matumizi ya plastiki na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kulinda mazingira."
Aliongeza kuwa vijana wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya kwa kutumia ubunifu, maarifa na mshik**ano katika kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Tukilinda mazingira leo, tunahakikisha kesho yenye usalama, afya njema na maendeleo endelevu kwa vizazi vijavyo.
PIRO inaendelea kutoa wito kwa wananchi wote kushiriki kikamilifu katika juhudi za uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti, kulinda vyanzo vya maji na kuacha vitendo vinavyoharibu mazingira.
"Hakuna sayari nyingine ya kukimbilia; tuna wajibu wa kuitunza dunia tuliyonayo."


ZAYSO CHARITY FESTIVAL 2026 – YATIMA DAY TABASAMU LAO, FURAHA YETUKwa moyo wa upendo, mshik**ano na uwajibikaji wa kijam...
30/05/2026

ZAYSO CHARITY FESTIVAL 2026 – YATIMA DAY
TABASAMU LAO, FURAHA YETU
Kwa moyo wa upendo, mshik**ano na uwajibikaji wa kijamii, Zanzibar Youth Support Organization (ZAYSO) kwa kushirikiana na wadau wake mbalimbali ikiwemo The Popular Inspiring and Relief Organization (PIRO) imefanikiwa kushiriki na kuandaa Tamasha la ZAYSO Charity Festival – Yatima Day 2026, lililofanyika tarehe 27–28 Mei 2026 (1447H) kwa lengo la kuwafariji na kuwasaidia watoto mayatima, watu wenye ulemavu pamoja na watu wasiojiweza katika kipindi cha Sikukuu ya Eid Al-Adha.
Tamasha hili halikuwa tu jukwaa la kutoa burudani au msaada, bali pia lilikuwa fursa muhimu ya kuelimisha jamii kuhusu masuala ya afya, ustawi wa watoto na maendeleo ya jamii. Kupitia ushiriki wa PIRO, tuliadhimisha kwa mafanikio Siku ya Hedhi Salama Duniani 2026 kwa kutoa elimu ya afya ya hedhi Salama na kugawa taulo za k**e kwa wasichana yatima, wenye ulemavu na washiriki wa tamasha hili. Akiwemo Mgeni Rasmi na Wasanii wa Qaswaida na Nasheed
Tumeendelea kusisitiza kuwa suala la hedhi salama ni jukumu la kila mmoja wetu. Wanaume na wavulana wana nafasi muhimu katika kuhakikisha wasichana na wanawake wanapata mazingira salama, yenye heshima na yanayowawezesha kuendelea na elimu, kazi na shughuli zao za kila siku bila vikwazo.
Aidha, tumetoa wito kwa Serikali, sekta binafsi, mashirika ya maendeleo na wadau mbalimbali kuwekeza zaidi katika:
Elimu ya afya ya hedhi Salama, Miundombinu rafiki ya maji na usafi wa mazingira, Vyoo salama mashuleni na katika jamii,Upatikanaji wa pedi kwa gharama nafuu ( )
Kadhalika, kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani (5 Juni), tumebeba kauli mbiu inayotuunganisha katika kujenga jamii bora:
"Mti kwa Mazingira; Ustawi kwa Binti – Tunza Utunzwe!"
Kauli mbiu hii inatukumbusha kuwa ustawi wa mtoto wa k**e, afya ya jamii na uhifadhi wa mazingira vina uhusiano mkubwa katika kujenga taifa lenye maendeleo endelevu.
Tunatoa shukrani za dhati kwa uongozi wa ZAYSO, washiriki wote, wadhamini, wahisani na wadau waliotuunga mkono katika kufanikisha tamasha hili. Tunajivunia kutunukiwa Cheti cha Ushiriki k**a ishara ya kuthamini mchango wetu katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii.

🌍✨ *SIKU YA VIJANA KIMATAIFA 2026* ✨🌍🗓 *12 Agosti 2026*Vijana ndio nguvu ya kazi taifa, wabunifu wa Leo na kesho pia ni ...
25/05/2026

🌍✨ *SIKU YA VIJANA KIMATAIFA 2026* ✨🌍
🗓 *12 Agosti 2026*

Vijana ndio nguvu ya kazi taifa, wabunifu wa Leo na kesho pia ni chachu ya maendeleo endelevu ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Kupitia Maadhimisho haya muhimu, tunalenga kuhamasisha ushiriki wa vijana katika ajira, ubunifu, Ujuzi, uwezeshaji, mazingira na maendeleo ya jamii.

PIRO* kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea kuwa mstari wa mbele kuhakikisha shughuli hii kubwa ya vijana inafanikiwa kwa kiwango cha juu zaidi. Tunawaalika wadau, wahisani, taasisi, kampuni binafsi pamoja na jamii kushiriki kuwekeza kwa vijana wetu kwa ajili ya mustakabali bora.

Mchango wako ni matumaini kwa vijana!*
Tushirikiane kujenga kizazi chenye uwezo, maadili, ubunifu, Ujuzi na ajira endelevu.

Pamoja Tunaweza!*
✔️ Kuibua vipaji vya vijana
✔️ Kukuza ubunifu na ajira
✔️ Kuimarisha ushiriki wa vijana katika maendeleo
✔️ Kujenga jamii yenye usawa na fursa kwa wote

COMING SOON…*
Maandalizi yanaendelea kwa nguvu kubwa!

Taasisi ya PIRO kwa kushirikiana na IUCN pamoja na Arena imefanikiwa kufanya shughuli ya usafi wa mazingira ya bahari (C...
22/05/2026

Taasisi ya PIRO kwa kushirikiana na IUCN pamoja na Arena imefanikiwa kufanya shughuli ya usafi wa mazingira ya bahari (Clean Up Activity) katika eneo la Tibirinzi, Wilaya ya Chake Chake – Mkoa wa Kusini Pemba kwa lengo la kuondoa taka za plastiki zinazohatarisha afya ya bahari na viumbe hai wa majini.

Kupitia shughuli hii, vijana na wanajamii walishiriki kukusanya taka za plastiki na kuhamasisha umuhimu wa utunzaji wa mazingira katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. 🌱

♻️ Shughuli hii ni sehemu ya maandalizi kuelekea uzinduzi wa mradi wa IslandPlas Zanzibar, mradi unaolenga:
✅ Kununua taka za plastiki kutoka kwa wananchi
✅ Kuzikusanya katika maeneo maalum
✅ Kuzichakata na kuzitumia tena kwa matumizi mapya
✅ Kukuza uchumi wa kijani na ajira kwa vijana
✅ Kulinda mazingira ya bahari na fukwe za Zanzibar

🌍 Bahari safi ni wajibu wetu sote!
Tushirikiane kujenga Zanzibar safi, salama na yenye mazingira endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

🤝 Karibu ufuatilie na kuunga mkono kazi za PIRO katika uhifadhi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi na maendeleo ya jamii.






CleanUpCampaign
EnvironmentalConservation
BlueEconomy
RecycleForFuture
ZanzibarEnvironment
PembaCleanUp
FightClimateChange
MarineConservation
GreenCommunity
SustainableZanzibar
IUCN
Arena
WasteRecycling
ProtectOurSea
ClimateJustice

Leo Tarehe 20 May. 2026 Nimejumuika na Wadau Wa Maendeleo ya Vijana Tukiwa Sambamba na Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya ...
20/05/2026

Leo Tarehe 20 May. 2026 Nimejumuika na Wadau Wa Maendeleo ya Vijana Tukiwa Sambamba na Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar ndugu Shaib Ibrahim Muhamed katika kikao cha kwanza kuhusu kuelekea katika maadhimisho ya siku ya vijana Kimataifa kwa mwaka huu na kuweka mikakati ya pamoja na kufanisha maadhimisho hayo.
Tunaishukuru Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji kupitia Idara ya Maendeleo ya Vijana Kuweka kikao cha pamoja kwa ajili ya kujadili na kuratibu kuelekea siku ya vijana kimataifa kwa mwaka wa 2026 kuweza kuchukua vijana mbalimbali wabunifu wa fani ili kuweza kuonesha ubunifu wao.
Kikao hicho kimafanyika katika ukumbi wa Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji iliopo Magomeni Wandaras.
Kikao hicho niliendeshwa na kusimamiwaa na Mwenyekiti wa kikao Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Vijana.

Kupitia VCAT Sessions pamoja na mafunzo maalum juu ya kuripoti kwa umakini, usahihi na weledi taarifa za SRHR yaliyotole...
19/05/2026

Kupitia VCAT Sessions pamoja na mafunzo maalum juu ya kuripoti kwa umakini, usahihi na weledi taarifa za SRHR yaliyotolewa kwa Waandishi wa Habari na PIRO chini ya Mradi wa *Elevate Access to Sexual Reproductive Health and Rights (SRHR) Tanzania and Zanzibar* kwa ufadhili wa EngenderHealth Tanzania, hatua mbalimbali zimeanza kuleta matokeo chanya katika utoaji wa elimu kwa jamii kupitia vyombo vya habari.

Miongoni mwa maadhimio ya mafunzo hayo ni kuandaa makala mbalimbali zinazolenga kuelimisha jamii kuhusu afya ya uzazi na haki zake, ambapo hadi sasa hatua za utekelezaji zinaendelea kuchukuliwa kwa mafanikio makubwa. Aidha, waandishi wa habari wameendelea kufanya mahojiano na wataalamu wa huduma za afya ili kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi na zenye kuleta mabadiliko chanya.

Leo kupitia ZBC na *Spice FM*, tumeshuhudia mahojiano muhimu yakifanyika kuhusu huduma za afya pamoja na huduma baada ya kuharibika kwa ujauzito. Katika kipindi hicho tulipata fursa ya kumualika Madam Zuwena Ali Salim ambaye alikuwa miongoni mwa wakufunzi waliochaguliwa na PIRO kutoa mafunzo hayo. Sambamba na hilo, yeye ni mdau mkubwa anayetekeleza mradi huo kupitia ZANA kwa lengo la kuendelea kuelimisha jamii na kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi kuhusu SRHR.

Kwa pamoja tunaendelea kutumia nguvu ya vyombo vya habari kuleta mabadiliko chanya, kuondoa unyanyapaa, na kujenga jamii yenye uelewa mpana kuhusu afya ya uzazi na haki zake.






HealthReporting
MediaForChange
AfyaYaUzazi
Zanzibar
Tanzania
SpiceFM
ZBC
ZANA
CommunityAwareness
EndingStigma
YouthEmpowerment
JournalismForImpact
HealthEducation

🌟 **Kuwekeza kwa Watoa Huduma ni Kuwekeza kwa Afya ya Vijana!** 🌟PIRO kwa kushirikiana na Wizara ya Afya pamoja na wadau...
28/04/2026

🌟 **Kuwekeza kwa Watoa Huduma ni Kuwekeza kwa Afya ya Vijana!** 🌟

PIRO kwa kushirikiana na Wizara ya Afya pamoja na wadau mbalimbali imeendelea kujenga uwezo wa watoa huduma za afya na Community Health Workers (CHWs) kupitia mafunzo ya **maadili ya kitaaluma katika huduma rafiki kwa vijana**.

Mafunzo haya yamelenga kuboresha utoaji wa huduma za **Sexual Reproductive Health and Rights (SRHR)**, huduma za **Post-Abortion Care (PAC)** pamoja na huduma za upangaji uzazi kwa heshima, usawa na bila ubaguzi.

Tunapoimarisha maarifa na maadili ya watoa huduma, tunafungua milango ya vijana kupata huduma bora, salama na zenye kuzingatia utu wao. 💙

🙏 Tunawaalika wadau, taasisi na jamii kuendelea kushirikiana nasi katika kujenga kizazi chenye afya, uelewa na matumaini. Pamoja tunaweza kuleta mabadiliko ya kweli!

CommunityHealthWorkers Zanzibar HealthForYouth EmpoweringCommunities ProfessionalEthics BetterFuture YouthHealth PartnershipForChange

05/04/2026
TAKA SI UCHAFU, NI FURSA YA KIPATO!Je, unajua kuwa taka unazoziona kila siku zinaweza kuwa chanzo cha kipato na ajira? 💰...
24/03/2026

TAKA SI UCHAFU, NI FURSA YA KIPATO!

Je, unajua kuwa taka unazoziona kila siku zinaweza kuwa chanzo cha kipato na ajira? 💰

Ni wakati wa kubadili mtazamo wetu — badala ya kuona taka k**a uchafu, tuzitumie k**a fursa ya kujikwamua kiuchumi na kulinda mazingira yetu 🌱

✔️ Tenganisha taka zako
✔️ Tumia tena (reuse)
✔️ Recycle kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi

Ungana na PIRO katika kuifanya Zanzibar kuwa safi, salama, na yenye fursa zaidi kwa wote! 🤝

📢 *Tuchukue hatua leo kwa kesho bora!*

YouthForChange SustainableZanzibar LindaMazingira

Address

Chake Chake Pemba
Zanzibar
ZANZIBAR

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Piro Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Piro Zanzibar:

Share