16/04/2015
🐓HAMASAAT🐓
Hatua ya mwanzo miongoni mwa hatua za kupata furaha ni swala.. ewe Mola tujaalie tuidumishe hadi tutakapokutana nawe
Tafuta raha yako daima kwa "kukumbatia" msahafu wako
Kwenye uhusiano wako na mtu mwingine: (kwa kadiri unavyotoa, ndivyo kadiri ya hadhari) kila mara ukizidisha kutoa, zidisha mfano wake kwenye hadhari, kwani hiyo itakufanya usizame kwenye bahari ya kitoa chako
{Na ni juu ya baba chakula chao na mavazi yao kwa sharia}
{kwa sharia}: kutokana na hali ya mwanamume, nyepesi au ngumu, halazimishwi mwenye hali ngumu asichokiweza
Akili na hekima:
Alisema Abu dardaa kumwambia Umm dardaa RA: nikighadhibika niridhie, na ukighadhibika nitakuridhia, na tusipofanya hivyo tunaweza kukosana upesi. Nani kati yetu anayetekeleza hayo?
"K**a kazi zinachosha, hakika kukaa bila kazi kunaleta uharibifu"
-omar bin al khatwab
Baadhi ya mambo hayakuumizi lakini yanakufunza,
hakika ulikuwa kwenye nia yako kuliko kawaida
Usishushe thamani ya nafsi yako kwa vile umekubali kukosolewa. Unachotakiwa ni kukubali makosa na kukubaliana na ukweli, na kuzidisha kuomba radhi ikilazimika, lakini hakuna ulazima wa kuiua nafsi yako
Mtu anayeishi kwa matumaini si kipofu wala si mwenye kuota ndoto za mchana, bali anaishi kiuhalisia; anatambua kwamba maisha pamoja na matatizo yake yote kuna suluhisho pembeni mwake
Ufupisho wa maisha
{Atakayefuata uongofu wangu hatapotea wala hatahangaika. Na atayepinga ukumbusho wangu hakika atakuwa na maisha ya dhiki}
Ewe Mola tunakuomba mwisho mwema
Ewe Mola mponye kila mgonjwa, na mfariji kila mwenye simanzi, na mruzuku kila aliyenyimwa, na ikubali toba ya kila mwenye kutubu, na upe furaha moyo wa kila mwenye huzuni, na warehemu maiti wetu na maiti waislamu
TUAMRISHANE
MEMA Inshallah