TAMWAZanzibar

TAMWAZanzibar TAMWA Zanzibar is a non-partisan not for profit sharing, non-Governmental professional membership organization fully registered in 1987.

08/03/2026

Mkurugenzi wa TAMWA-ZNZ, Nairat Abdulla Ali, akitoa salamu za maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2026.
Tunapoadhimisha siku hii muhimu, tunaendelea kusisitiza umuhimu wa usawa wa kijinsia, uongozi wa wanawake na ushiriki wao katika maendeleo ya jamii.

TAMWA-ZNZ inaanza rasmi kampeni ya kidijitali ya kukusanya maoni ya jamii kuhusu mchango wa wanawake viongozi katika kul...
05/03/2026

TAMWA-ZNZ inaanza rasmi kampeni ya kidijitali ya kukusanya maoni ya jamii kuhusu mchango wa wanawake viongozi katika kuleta maendeleo ya jamii.

Wewe unaonaje? Mwanamke kiongozi ameleta mabadiliko gani katika jamii yako?

March sets the tone.A month to honour the women who lead, inspire and transform our communities every day.
02/03/2026

March sets the tone.

A month to honour the women who lead, inspire and transform our communities every day.

March is here! A month dedicated to celebrating the strength, leadership and rights of women across Zanzibar and beyond....
01/03/2026

March is here! A month dedicated to celebrating the strength, leadership and rights of women across Zanzibar and beyond.

At TAMWA-ZNZ, we honour the voices, resilience and contributions of women who continue to shape our communities every day.

Let’s celebrate. Let’s uplift. Let’s stand with women.

Uongozi wa wanawake hauanzi ghafla ukubwani, huanza mapema, darasani.Kuwahamasisha watoto wa k**e kugombea nafasi za uon...
27/02/2026

Uongozi wa wanawake hauanzi ghafla ukubwani, huanza mapema, darasani.

Kuwahamasisha watoto wa k**e kugombea nafasi za uongozi katika serikali za wanafunzi ni hatua muhimu ya kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi, kujiamini na kuwa viongozi wa kesho.

Tuwape nafasi leo ili waongoze kesho.


Mazungumzo na jamii ya Shehia ya Bopwe, Wete – Pemba yamefungua hatua muhimu katika utekelezaji wa mradi wa CADiR, unaol...
26/02/2026

Mazungumzo na jamii ya Shehia ya Bopwe, Wete – Pemba yamefungua hatua muhimu katika utekelezaji wa mradi wa CADiR, unaolenga kuimarisha uwezo wa watu wenye ulemavu kupitia vikundi vya kuweka na kukopa.

Kupitia mkutano wa utambulisho wa mradi uliofanyika tarehe 25 Februari 2026, wanajamii walipata fursa ya kujadili namna watakavyoshiriki katika kuunda vikundi vitakavyowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kujiongezea kipato.

Zoezi la kuorodhesha majina ya wanachama linatarajiwa kuanza Jumapili ijayo.

Tunawashukuru kwa dhati wote waliojitokeza kujaza fomu za kushiriki katika Tuzo za Mabadiliko ya Tabia Nchi.Tunapenda ku...
25/02/2026

Tunawashukuru kwa dhati wote waliojitokeza kujaza fomu za kushiriki katika Tuzo za Mabadiliko ya Tabia Nchi.

Tunapenda kuwataarifu kuwa zoezi la upokeaji wa fomu limefungwa rasmi, na hatua zinazofuata za mchakato wa tathmini zinaendelea.

Asanteni kwa ushiriki wenu na mchango wenu katika kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Uwezeshaji wa kiuchumi ni hatua muhimu katika kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika ma...
25/02/2026

Uwezeshaji wa kiuchumi ni hatua muhimu katika kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata nafasi sawa ya kushiriki katika maendeleo ya jamii.

Kwa kushirikiana na pamoja na tunaendelea kujenga uwezo wa watu wenye ulemavu kwa kuimarisha vikundi vya kuweka na kukopa vinavyowawezesha kujitegemea kiuchumi na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kujiongezea kipato.

Hatua hii inalenga kuondoa vikwazo vya kijamii na kiuchumi vinavyowazuia kushiriki katika fursa za maendeleo.

Ewe Mwanahabari wa k**e!!Karibu  ujiunge nasi ili uwe sehemu ya Wanahabari Wanawake wanaotumia kalamu na sauti zao kulet...
24/02/2026

Ewe Mwanahabari wa k**e!!
Karibu ujiunge nasi ili uwe sehemu ya Wanahabari Wanawake wanaotumia kalamu na sauti zao kuleta mabadiliko chanya, kukuza usawa wa kijinsia na kutetea haki za wanawake na watoto katika jamii.

Kujenga jamii salama kunahitaji hatua za makusudi kupinga udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto.Ni wajibu wa kila mm...
23/02/2026

Kujenga jamii salama kunahitaji hatua za makusudi kupinga udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto.

Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuhakikisha wanawake na watoto wanaishi katika mazingira yanayowawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii bila hofu wala vikwazo.

Kila habari nzuri ni hatua kuelekea jamii yenye usawa.
17/09/2025

Kila habari nzuri ni hatua kuelekea jamii yenye usawa.

Address

Tunguu
Zanzibar City

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAMWAZanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to TAMWAZanzibar:

Share