30/08/2026
Vikundi vya Kijaluba vya wakulima wa mboga mboga, Jitihada na Tuwezeshwe, katika Wilaya ya Kaskazini B, Unguja, vimeanza kutumia ujuzi walioupata kupitia Mradi wa CADiR chini ya Mpango wa Uwezeshaji Kiuchumi, huku tayari wakiwa wameanza kuvuna na kuuza mazao yao.
Hata hivyo, changamoto ya upatikanaji wa maji na miundombinu ya umwagiliaji bado inaendelea kuathiri uzalishaji. Kwa sasa, wanachama hutumia madumu kubeba maji kwenda mashambani, jambo linalowaletea ugumu zaidi wanachama wenye ulemavu.