31/12/2024
UJUMBE KWA VIJANA WENZANGU
Habari za leo Vijana wenzangu?
Natumai wote tuwazima wa afya na tunaendelea vizuri. Kwa wale wenye changamoto Mungu atawafanyia wepesi kwenye changamoto zao.
Sisi Vijana tunazo *ndoto,* ndoto hizi hutofautiana kulingana na shauku, vipaji, imani pamoja na uwezo ambao Mungu kila mtu amemjaalia, tuendelee kuzipigania ndoto zetu bila kuchoka Wala kukatishwa tamaa.
Mwaka 2024 tulijiwekea malengo mbalimbali, wapo miongoni mwetu wamefanikiwa kuyatimiza baadhi ya malengo yao kikamilifu, tunawapingeza na kuwaombea kwa Mungu kila la kheri.
Wapo ambao miongoni mwetu malengo yao ndani ya huu mwaka hayakutimia kabisa kutokana na sababu mbalimbali, *tusikate tamaa* tuendelee kutiana moyo na kuombeana Mungu atufanyie wepesi kuyafikia malengo ya ndoto zetu. Hakika nafasi bado tunayo na *hata kesho jua litachomoza tena*.
Tuendelee kupambana na kuzikimbizia ndoto zetu kwa hari na shauku kubwa, huku tukiamini *ipo siku mambo yatajipa tu*. Ni makosa makubwa sana kukata tamaa kwa kile unachokipigania, tuendelee kupambana huku tukimtumainia Mungu katika tunayoyaendea.
Mwaka huu ndio umeshaisha, basi mwaka mpya ukawe mwaka wa baraka na ufunguo wa kufungua kila hitaji letu.
Nawatakia heri na fanaka ya mwaka mpya wa 2025.
Nimimi Ndungu yenu
*Swalehe Iddi Mwamnyeke*