WSCO MBOZI

WSCO MBOZI MBOZI DISTRICT PARALEGALS ORGANIZATION (WSCO)

Leo Tarehe 04/06/2026 Taasisi ya Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya MBOZI ( WSCO) kwa kushirikiana na Polisi Kata ya MAHENJ...
04/06/2026

Leo Tarehe 04/06/2026 Taasisi ya Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya MBOZI ( WSCO) kwa kushirikiana na Polisi Kata ya MAHENJE Inspector NELSON MWINUKA na Afisa Dawati la Msaada wa Kisheria Wilaya ya MBOZI Bi. LILIAN KIKOTI na Wajumbe wa kamati za MTAKUWWA Kata ya MAHENJE,Wamefanikiwa Kutoa Elimu ya Kisheria hususani, Elimu ya Kupinga Vitendo vya Ukatili, Dhidi ya Wanawake na Watoto katika Mkutano Mkuu wa Shule ya Msingi MAHENJE ambapo pamoja na Elimu zilizotolewa na wataalamu hao kikubwa wameweza kuwajengea uwezo wanafunzi kuhusiana na Mbinu mbalimbali za kujilinda Dhidi ya Ukatili kwa kipindi hiki Cha Likizo ambacho watakuwa Majumbani na wawapo maeneo mbalimbali Ambayo si Mazingira ya nyumbani, pamoja na Hilo wameweza kufundishwa Maana ya Ukatili,aina za Ukatili na Mifano yake,Madhara yake na Maeneo ya kutoa Taarifa pindi wanapoona viashiria vya Ukatili,au pindi unatokea,

Kwa upande wa wazazi nao wamejengewa Uwezo,na kuwahamasisha wazazi kujitahidi kuwalinda Watoto Wao Dhidi ya Vitendo vya Ukatili, na kuwa karibu na Watoto na Kupata Muda wa kuongea nao ili kujua changamoto zao na kutafuta ufumbuzi

22/05/2026
Leo tarehe 20/05/2026 Mtoa huduma ya Msaada wa kisheria ndugu SHEMU SIMON akiongozana na mtendaji wa kata tumefanikisha ...
21/05/2026

Leo tarehe 20/05/2026 Mtoa huduma ya Msaada wa kisheria ndugu SHEMU SIMON akiongozana na mtendaji wa kata tumefanikisha kuwapeleka watoto waliokua hawajalipoti shule ya Secondary Hezya, msaidizi wa kisheria ametoa elimu ya msaada wa kisheria kwa wazazi pamoja na watoto ni haki zipi mtoto anapaswa kuzipata ikiwemo elimu, maradhi n.k hivyo basi watoto na wazazi wamefurahia huduma ya msaada wa kisheria na kuaahidi kutoa ushirikiano na kuhakisha watoto wanasoma mpaka kumaliza elimu ya Secondary. Uongozi wa Shule ya Hezya Secondary umewapongeza sana Msaidizi wa Kisheria na Mtendaji wa Kata kwa Ufuatiliaji Mzuri wa wanafunzi watoro, Kwani wanahakikisha Watoto Wote wanapata Haki ya Elimu.

Leo tarehe 15/05/2026 Wasaidizi wa kisheria Kituo Cha  WSCO-Mbozi wamefanya kikao maalumu Cha kimkakati   kilicho lenga ...
15/05/2026

Leo tarehe 15/05/2026 Wasaidizi wa kisheria Kituo Cha WSCO-Mbozi wamefanya kikao maalumu Cha kimkakati kilicho lenga kuimalisha utendaji kazi Kwa ajili ya maendeleo ya taasisi kikao hicho kiliongozwa na Mkurugenzi Bi Rehema Peter Mbwaga ambapo mambo mbalimbali yamejadiliwa ambayo yatasaidia uendelevu wa Utoaji wa Huduma za Msaada wa Kisheria/ Upatikanaji wa Haki kwenye jamii ili kuhakikisha inaishi kwa Usawa,Haki ,Amani ili kuleta Maendeleo Endelevu.

Imetolewa na afisa mawasiliano taasisi ya Wasaidizi wa kisheria WSCO-mbozi.
Musa katyeka simbeye
0624781572

Taasisi ya Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya MBOZI Mkoani SONGWE inayojulikana kwa Jina la WOMEN AND STANDARD CHANGES ORGA...
15/05/2026

Taasisi ya Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya MBOZI Mkoani SONGWE inayojulikana kwa Jina la WOMEN AND STANDARD CHANGES ORGANIZATION ( WSCO) ilifanikiwa Kushiriki Tukio la Utambulisho wa Mradi wa FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY ( FCS) Uliofanyika katika Ukumbi wa UKINGA HILL HOTEL Uliopo katika Mji wa TUNDUMA Kikao hicho kilifanyika Siku 2 yaani Tarehe 28 na 29, April,2026 kikiwa na Lengo la kuelezea Shughuli zitakazofanyika katika Mradi Huo Mpya. Takribani Taasisi 9 za Mkoa wa Songwe zilizopata Mradi huo zilishiriki Vikao Hivyo.

27/02/2026
Msaidizi wa Kisheria Wilaya ya MBOZI Ndugu, CHRISTOPHER ANYELWISYE LUSOKO Leo Tarehe 27/02/2026 Ameshiriki Mafunzo yaliy...
27/02/2026

Msaidizi wa Kisheria Wilaya ya MBOZI Ndugu, CHRISTOPHER ANYELWISYE LUSOKO Leo Tarehe 27/02/2026 Ameshiriki Mafunzo yaliyoandaliwa na UMOJA WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA ( UTPC)
Yaliyolenga kujua Dhana nzima ya Uandishi wa Habari, Kutenda na Matokeo na kuona umhimu wa Waandishi wa Habari kwenye Jamii Kwani wao wamekaa katikati Kati ya Wananchi na Serikali jinsi wanavyochochea Maendeleo kwenye Jamii.

Address

LAMI Street
Songwe
54201

Telephone

+255757652614

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when WSCO MBOZI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to WSCO MBOZI:

Shortcuts

Share