Nihurumie foundation TZ

Nihurumie foundation TZ Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Nihurumie foundation TZ, Non-Governmental Organization (NGO), Namtumbo, Songea.

Kwanza niwashukuru wote mlioshiriki kumchangia dada  ambaye anaendelea na matibabu katika hospitali ya Manipal, Bangalor...
09/04/2022

Kwanza niwashukuru wote mlioshiriki kumchangia dada ambaye anaendelea na matibabu katika hospitali ya Manipal, Bangalore, India. Kwa siku chache tulizofanya challenge yetu alipata 42M kati ya 65M alizokua akihitaji. Hivyo bado 23M ambazo tutazimalizia mwisho wa mwezi huu.

Nililazimika kukatisha challenge ya Mishy na kumuomba tuendelee mwisho wa mwezi, kwa ajili ya ndugu yangu Joseph Massawe ambaye ni mgonjwa sana. Joseph alianza kuugua 2020 kwa kuvimba mwili na kupata michubuko kwenye ngozi. Alitibiwa Agha Khan na Rabinisia lakini hali yake haikutengemaa. Aliendelea kupata changamoyo ya mapafu na moyo kushindwa kufanya kazi vizuri.

Baadae alichukuliwa sampuli (biopsy) na majibu yakaonesha ana "auto immune syndrome" yani mfumo wake wa kinga kushambulia mwili wake badala ya kumlinda (immune system attacking your body instead of protecting it). Magonjwa haya kwa ujumla huitwa Rhaematological disease.

Matibabu yake ni kupandikizwa seli kinga nyingine (immunoglobulin replacement therapy) ambayo hufanyika nje ya nchi. Familia ikampeleka Medicana international Hospital iliyopo mjini Izmir, Uturuki.

Alipofika ikaonekana ana maji kwenye chamber moja ya moyo (pedicarium) na infection kwenye mapafu. Madaktari wakashauri kabla ya upandikizaji wa seli, atibiwe kwanza magonjwa yanayomsumbua. Ametibiwa na hali yake imetengemaa kidogo hivyo kwa sasa anaweza kupandikizwa seli.

Gharama za upandikizaji ni $19,000 lakini pia ana deni la $6,000 na hivyo kufanya jumla kuwa $25,000 sawa na TZS 60M.

Bahati mbaya kipindi hiki ambacho yupo tayari kupandikizwa seli, familia imeishiwa nguvu. Kwa zaidi ya miaka miwili familia imetumia gharama kubwa kumtibia, hivyo kwa sasa pumzi imekata.

Hivyo ndugu, jamaa na marafiki tumejipigapiga ili kuokoa maisha yake na kupata 20M, bado 40M. Kwa unyenyekevu naomba tuwe na challenge ya masaa 72 kuokoa maisha ya ndugu yetu huyu. Kumbuka bila kufanya upandikizaji wa seli Joseph hataweza kuendelea kuishi.

Tuma mchango wako kwenda (Tigopesa) 0714-049556 AU (MPESA) 0745-777112 Martina Desdery Massawe. Huyu ni dada mkubwa wa Joseph. Asante na Mungu akubariki.

Nihurumie foundation TZ

Leo dada  ameingizwa theatre kwa ajili ya upasuaji wake wa pili wa uti wa mgongo, baada ya kulipa nusu ya kiasi cha pesa...
31/03/2022

Leo dada ameingizwa theatre kwa ajili ya upasuaji wake wa pili wa uti wa mgongo, baada ya kulipa nusu ya kiasi cha pesa kilichokua kinahitajika. Asanteni watanzania wote mliowezesha jambo hili jema. Mungu awabariki sana.

Tumuombee upasuaji wake uende vizuri na aweze kutoka salama. Tuwaombee madaktari na manesi wanaomhudumia. Tumuombee Mishy aweze kupona na kurudi salama. Kumbuka madaktari hutibu lakini Mungu ndiye huponya.

Wakati huohuo tuendelee kuchangia gharama zilizobakia. Tuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Aisee tumeupiga mwingi sana. Kutoka 28M jana saa 4 usiku hadi 34M muda huu si kazi ndogo. Hongereni sana wote mliofaniki...
30/03/2022

Aisee tumeupiga mwingi sana. Kutoka 28M jana saa 4 usiku hadi 34M muda huu si kazi ndogo. Hongereni sana wote mliofanikisha kazi hii kubwa. Sasa imebaki 1M tu ili dada Mishy kesho aingie theatre kwa upasuaji wa pili. Kiasi kilichobaki tutachanga baada ya upasuaji.

Tuendelee kuupiga mwingi kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Group la  kanda ya kaskazini wanaendelea kujichanga ili kuongeza nguvu kwenye matibabu ya dada . Lengo ni kuhakikisha Mi...
30/03/2022

Group la kanda ya kaskazini wanaendelea kujichanga ili kuongeza nguvu kwenye matibabu ya dada . Lengo ni kuhakikisha Mishy anaingia theatre kesho. Ungana nao sasa kwa kutuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Bado 3M ili kesho dada  aingie theatre kwa operation ya pili. Tuendelee kutuma michango yetu kwenda M-Pesa 0766180656, T...
30/03/2022

Bado 3M ili kesho dada aingie theatre kwa operation ya pili. Tuendelee kutuma michango yetu kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸ™

Nihurumie foundation TZ

HABARI NJEMA ⚑⚑πŸ”₯Habari njema ni kwamba menejimenti ya Hospitali ya Manipal imekubali maombi ya kumfanyia dada Mishally u...
29/03/2022

HABARI NJEMA ⚑⚑πŸ”₯

Habari njema ni kwamba menejimenti ya Hospitali ya Manipal imekubali maombi ya kumfanyia dada Mishally upasuaji wa pili keshokutwa (alhamisi) ikiwa tutaweza kulipa anagalua nusu ya gharama kufikia kesho. Hii ina maana kwamba by kesho saa 8 mchana Mishy anatakiwa awe amedeposit angalau 35M, halafu nyingine atazilipa baada ya upasuaji.

Hadi sasa kiasi alichopata Mishy ni 28M, that means bado 7M tu ili alhamisi awe na uhakika wa kuingia theatre. Naomba tuitumie nafasi hii ili aweze kufanyiwa upasuaji. Tukumbuke hii ni nafasi ya pili, tusiipoteze tena.

Leo tuweke malengo ya kufika 30M, halafu kesho tukamilishe 5M ili Mishy aingie kwenye upasuaji. Akitoka tuwe tumebaki na deni la 30M. Tukiwa na nia inawezekana. Tuanze sasa safari ya kuelekea 30M.

Tuendelee kutuma michango yetu kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Leo tumedorora kidogo. Mishaly ananiambia kwenye simu yake kuna ongezeko la 1M tu toka asubuhi. Hii inafanya jumla kuwa ...
28/03/2022

Leo tumedorora kidogo. Mishaly ananiambia kwenye simu yake kuna ongezeko la 1M tu toka asubuhi. Hii inafanya jumla kuwa 26M. Tuendelee kumshika mkono dada yetu, tusimuache peke yake. Tuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Asanteni sana wote mnaoendelea kuupiga mwingi kwa ajili ya matibabu ya dada Mishaly Sumary ambaye yupo nchini India kati...
28/03/2022

Asanteni sana wote mnaoendelea kuupiga mwingi kwa ajili ya matibabu ya dada Mishaly Sumary ambaye yupo nchini India katika hospitali ya Manipal, mjini Banalore. Kiasi kilichopatikana hadi sasa ni 25M. Jipigie makofi k**a wewe ni miongoni mwa watu waliochangia. Hata k**a umetoa senti moja wewe ni shujaa. Bila senti yako Mishy asingekua na 25M sasa.

Endelea kutuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu awabariki sana!!
Nihurumie foundation TZ

Tumefikisha 21M sawa na 33% ya kuchangia 65M kwa ajili ya matibabu ya dada  aliyepo nchini India. Sasa naomba niwakaribi...
27/03/2022

Tumefikisha 21M sawa na 33% ya kuchangia 65M kwa ajili ya matibabu ya dada aliyepo nchini India. Sasa naomba niwakaribishe rasmi team jerojero uwanjani waupige mwingi. K**a una jero moja toa kwa ajili yako. K**a unazo mbili mlipie mkeo/mumeo. K**a una zaidi mlipie mzazi wako, mwanao, mchungaji wako, imamu wako, mwalimu wako etc.

Team jerojero hamjawahi kuniangusha. Hebu tuanze kazi tumsaidie dada yetu aweze kusimama tena. Tuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Jana Jumamosi, 26-03-2022 mwanafamilia wa   ndugu yangu Francis Daudi alimtembelea Dada yetu,  kwenye apartment ya Class...
27/03/2022

Jana Jumamosi, 26-03-2022 mwanafamilia wa ndugu yangu Francis Daudi alimtembelea Dada yetu, kwenye apartment ya Classic Home, iliyopo mjini Bangalore (India) ambapo anasubiri kufanyiwa operesheni ya pili kwenye hospital ya Manipal, Bangalore.

Francis alikua safarini kutokea Basel (Uswisi) kwenda New Delhi (India). Kabla hajaondoka New Delhi aliamua kusafiri hadi Bangalore kwenda kumjulia hali dada Mishy. Hiki ni kiwango cha juu cha kujitoa. Ni upendo wa Agape. Namshukuru sana ndugu yangu kwa majitoleo yake hasa kipindi hiki cha kwaresma.

Kwa wasiofahamu, Miaka 11 iliyopita Mishy akitoka kazini alivamiwa na kundi la Wahuni, waliompiga na kumuumiza vibaya. Walimvunja nyonga, mbavu, mguu, mkono, taya na uti wa Mgongo. Miaka yote 11 imekua ya mateso kwake, na amekua mtu wa kulala tu kitandani. January mwaka huu tulimchangia 53M akaenda India kwa matibabu. Alifanyiwa upasuaji wa kwanza ambao umeonesha mafanikio.

Anahitajika kufanyiwa upasuaji wa pili ambao gharama zake ni 65M. Tarehe ya upasuaji ilikua leo lakini upasuaji huo umeshindwa kufanyika kwa kukosa fedha. Hadi sasa kiasi kilichopatikana ni 20M tu.

Naomba tuendelee kumsaidia ili kutimiza gharama za matibabu zinazohitajika, pamoja na kutatua changamoto nyingine zinazomkabili ikiwemo kukosa fedha za physiotherapy.

Endelea kutuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766-180656, TigoPesa 0718-626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly

Nihurumie foundation TZ

Ameandika Malisa GJ  Mishaly yupo kwenye mkwamo katika nchi ya ugeni. Kilomita nyingi kutoka nchi ya wazazi wake. Amekwa...
27/03/2022

Ameandika Malisa GJ
Mishaly yupo kwenye mkwamo katika nchi ya ugeni. Kilomita nyingi kutoka nchi ya wazazi wake. Amekwama kufanyiwa upasuaji wa pili kwa kukosa fedha. Amekwama kulipia appartment. Amekwama kurenew visa. Amekwama hata hela ya chakula, anakula mara moja tu kwa siku k**a mfungwa.

Wakati wewe ambaye huna tatizo lolote la kiafya unakula mara 3 kwa siku, Mishy aliyevunjika uti wa mgongo na kulala kitandani miaka 11 anakula mara moja tu kwa siku. Katikati ya maumivu makali ya mgongo, ana maumivu ya hisia, na sasa yameongezeka maumivu ya njaa. Yupo kwenye mkwamo mkubwa.

Sisi ndio wa kumnasua kwenye mkwamo huo. Sisi "team jerojero" ndio tulimchangia 53M kupitia ukurasa huu akaenda India kutibiwa. Bahati mbaya fedha hizo hazikutosha kukamilisha matibabu. Zinahitajika 65M zaidi ili aweze kufanyiwa upasuaji wa pili na kurejea nchini. Kwa umoja wetu naomba tuungane kumpiga "tafu" k**a tulivyofanya awamu ya kwanza ambapo tumlimchangia 53M kwa siku 3 tu (masaa 72).

Sisi ndio tutakaomlipia gharama za matibabu zilizosalia. Sisi ndio tutakaommlipia aweze kurenew visa yake. Sisi ndio tutakaomlipia appartment. Sisi ndio tutakaomlipia chakula. Sisi ndio tutakaomlipia ticket ya kurudi. Hana watu wengine anaowategemea zaidi yetu. Hivyo naomba tusimtelekeze katika nchi ya ugeni. Kwa kuwa maji tushayavulia nguo hatuna budi kuyaoga.

Endelea kutuma mchango wako kwenda M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Nihurumie foundation TZ

Tunamshukuru Mungu dada yetu  anaendelea vizuri na matibabu katika hospitali ya , iliyopo Bangalore nchini India yapata ...
23/03/2022

Tunamshukuru Mungu dada yetu anaendelea vizuri na matibabu katika hospitali ya , iliyopo Bangalore nchini India yapata miezi mitatu sasa tangu tulipompeleka huko kwa matibabu mwezi January mwaka huu.

Mishy alivamiwa na watu wasiojulikana December 26 mwaka 2011 akitokea Burere Hospital, Kibaha alipokua anafanya kazi k**a muuguzi. Watu hao walimjeruhi kwa marungu na nondo na kumvunja mkono, mguu, nyonga, taya, meno, wakamtegua shingo na kumvunja uti wa mgongo. Walikimbia baada ya kujua wameua. Lakini kwa neema ya Mungu alizinduka akiwa kitandani MOI.

Akiwa MOI alifanikiwa kupata matibabu ya mguu, mkono na nyonga vilivyovunjika. Pia aliweza kuunga shingo (japo bado anatumia neck support), taya na kupata meno bandia kufidia yale yaliyong'olewa. Lakini hawakufanikiwa kuunga uti wa mgongo. Hivyo kwa miaka 11 amelala kitandani kwa mateso makubwa na maumivu makali.

Kwa zaidi ya mwaka mmoja familia ya GH tumekua tukimsaidia kwa mahitaji yake mbalimbali. Na mwaka jana December nilimleta kumuombea msaada wa kwenda India kwa matibabu ya uti wa mgongo.

Kwa umoja wetu tulifanikiwa kumchangia 53M ndani ya masaa 72 (siku 3) na akaweza kwenda India kwa matibabu. Alifanyiwa upasuaji wa kwanza mwezi January 20 mwaka huu. Upasuaji huo uliofanyika kwa masaa 8 ulimalizika salama na umekua na matokeo chanya. Sasa mikono yake miwili sasa inafanya kazi na ameanza kupata "sense" miguuni ambapo kwa zaidi ya miaka 10 ilikua imekufa ganzi.

Hata hivyo Mishy anahitaji upasuaji wa pili ili aweze kusimama na ikiwezekana kutembea kabisa. Upasuaji huo ulipangwa kufanyika tar.13 March 2022 lakini haikuwezekana kutokana na kukosa fedha. Niliwasiliana na Menejimenti ya hospitali wamfanyie upasuaji halafu tutalipa baadae lakini ilishindikana kwa sababu hata upasuaji wa kwanza fedha hazikutosha. Alibaki na deni la $10,000.

Gharama za upasuaji wa pili ni $30,000 lakini tumekua na mazungumzo marefu na menejimenti ya hospitali ili wapunguze gharama kwa sababu Mishy hana uwezo. Tumeieleza hospitali kwamba Mishy anatibiwa kwa michango midogomidogo inayotolewa na watanzania wanaoguswa hivyo hataweza kumudu ghafama hizo.

Baada ya kuomba sana hatimaye wamekubali punguza gharama hadi $16,000 na wamemuandikia tarehe ya upasuaji itakua jumapili March 27 mwaka huu.

Masharti waliyotupa ni kwamba kabla ya jumapili kiasi chote ($10,000 + $16,000) kiwe deposited kwenye akaunti yao ili jumapili Mishy aingizwe theatre kwa upasuaji. Tukishindwa kufanya hivyo basi atalazimika kulipia gharama halisi za upasuaji ambazo ni $30,000 pamoja na deni la $10,000.

Hivyo basi naomba tuanze challenge yetu kwa dharura usiku huu kwa ajili ya kuhakikisha Mishy anaingia kwenye upasuaji jumapili. Hata hivyo baada ya upasuaji atahitaji $3,000 kwa ajili ya physiotherapy kwa wiki tatu zaidi atakazokaa India.

Pia Mishy ameishiwa fedha ya chakula. Kwa wiki mbili sasa amekua akila mara moja tu (usiku) ili kupunguza makali ya bajeti. Juzi alinipigia kuniambia "kaka yangu hata hela ya kula mara moja imeniishia, na nimekua nikisaidiwa chakula na wagonjwa wenzangu"

Namshukuru sana shemeji yangu ambaye aliokoa jahazi na kumtumia pesa kidogo za chakula za kumsaidia kwa siku hizi chache. Mungu akubariki sana shem wangu wa nguvu.

Kwahiyo gharama halisi za matibabu zilizobaki kwa sasa ni $29,000 ambazo ni sawa na TZS 60M. Ukijumlisha gharama za ticket na kurenew visa (maana visa yake imeisha leo) gharama zote zinaweza kufika TZS 65M.

Hivyo basi naomba tuwe na challenge ya masaa 96 (siku 4) za kutafuta 65M kwa ajili ya kukamilisha matibabu ya dada yetu Mishy ili aweze kusimama tena.

Michango yote inapokelewa kupitia namba za Mishaly mwenyewe M-Pesa 0766180656, Tigopesa 0718626642 au Bank Account (CRDB ) 0152078706601, jina Mishaly Sumary. Simu yake amemuachia kaka yake ambaye ndiye anayepokea kwa niaba yake.

Asante sana na Mungu akubariki.! πŸ™πŸΎ

Address

Namtumbo
Songea

Telephone

+255763511516

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nihurumie foundation TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Nihurumie foundation TZ:

Shortcuts

Share