Maisha na Tembo

Maisha na Tembo Maisha na Tembo (Lives with elephants), is an advocacy and awareness project initiated by TEF🐘🐝

Elimu ya uhifadhi mashuleni ni uwekezaji wa Taifa la kesho.Kuelimisha watoto kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na ...
20/05/2026

Elimu ya uhifadhi mashuleni ni uwekezaji wa Taifa la kesho.

Kuelimisha watoto kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na wanyamapori ni hatua muhimu ya kujenga jamii yenye uelewa, uwajibikaji na uwezo wa kuishi kwa amani na tembo pamoja na viumbe wengine wa porini.

Kupitia elimu hii, tunakuza kizazi kinachotambua thamani ya urithi wa asili na wajibu wa kuulinda kwa manufaa ya sasa na ya vizazi vijavyo.



πŸ“ Teknolojia na uhifadhi vinaenda sambamba.Ufuatiliaji wa mienendo ya tembo kupitia mikanda ya visukuma  mawimbi, husaid...
13/05/2026

πŸ“ Teknolojia na uhifadhi vinaenda sambamba.

Ufuatiliaji wa mienendo ya tembo kupitia mikanda ya visukuma mawimbi, husaidia kuelewa njia zao za uhamaji na kutambua maeneo yenye migogoro kati ya binadamu na tembo.

Taarifa hizi huimarisha mipango ya uhifadhi, na husaidia kulinda tembo pamoja na usalama wa jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi.



06/05/2026

Uharibifu wa makazi ya asili ya Tembo hupunguza maeneo ya malisho na kuchochea migogoro kati ya tembo na binadamu.

Hivyo, ni wajibu wa kila Mtanzania kuwa balozi wa uhifadhi wa mazingira ili kulinda tembo wetu, kuimarisha ustawi wa wanyamapori na kulinda urithi wetu wa asili.



Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori [Sura ya 283, Toleo Lililorekebishwa la Mwaka 2022], shughuli za kibinad...
29/04/2026

Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori [Sura ya 283, Toleo Lililorekebishwa la Mwaka 2022], shughuli za kibinadamu zinadhibitiwa ndani na karibu na mipaka ya maeneo ya hifadhi, ambapo katika baadhi ya maeneo huwekwa ukanda wa ulinzi (buffer zone) unaoweza kufikia mita 500 kutoka mpaka wa hifadhi kulingana na kanuni na mipango husika ya matumizi ya ardhi.

Hivyo, ni muhimu kuzingatia na kutekeleza mpango bora wa matumizi ya ardhi katika vijiji hasa vinavyopakana na hifadhi, ili kupunguza mwigiliano hasi kati ya binadamu na tembo.

Vikundi vya kuweka na kukopa fedha (VSLAs), katika jamii zinazopakana na hifadhi, huwawezesha wanajamii kupata mitaji mi...
22/04/2026

Vikundi vya kuweka na kukopa fedha (VSLAs), katika jamii zinazopakana na hifadhi, huwawezesha wanajamii kupata mitaji midogo ya ujasiriamali. Hivyo, hupunguza utegemezi wa kilimo cha mazao ambacho huweza kuharibiwa na tembo 🐘.

Tunatoa wito kwa wadau mbalimbali kutumia mbinu hii, ili kupunguza migogoro kati ya watu na tembo, na kuboreshwa kwa riziki za jamii.

Tembo ni mnyama muhimu kwenye ikolojia. Kutoweka kwake huathiri mifumo ya ikolojia. Hivyo, tushirikiane kwa pamoja kuwal...
15/04/2026

Tembo ni mnyama muhimu kwenye ikolojia.
Kutoweka kwake huathiri mifumo ya ikolojia.
Hivyo, tushirikiane kwa pamoja kuwalinda na kuwahifadhi kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.

Je, wajua vikosi vya mwitikio wa haraka vya jamii hupunguza uharibifu wa tembo kwenye makazi ya watu kwa usalama?Jamii h...
08/04/2026

Je, wajua vikosi vya mwitikio wa haraka vya jamii hupunguza uharibifu wa tembo kwenye makazi ya watu kwa usalama?

Jamii hutoa taarifa mara tu tembo wanapoonekana wakikabili makazi au mashamba ya watu, ndipo vikosi hivyo huchukua hatua za haraka kuwadhibiti tembo na kurudi hifadhini kwa kutumia mbinu salama bila kuwadhuru.

Maisha na tembo yanawezekana tukichukua hatua sahihi kwa wakati.🐘🐘

🐝 Uzio wa Mizinga ya Nyuki: Suluhisho la Asili Dhidi ya Tembo 🌿🐘Uzio wa mizinga ya nyuki ni njia bunifu inayosaidia kuli...
01/04/2026

🐝 Uzio wa Mizinga ya Nyuki: Suluhisho la Asili Dhidi ya Tembo 🌿🐘

Uzio wa mizinga ya nyuki ni njia bunifu inayosaidia kulinda mashamba dhidi ya uvamizi wa tembo.

Kupitia mbinu hii:
βœ… Wakulima hupunguza uharibifu wa mazao
βœ… Hupata kipato cha ziada kupitia uvunaji na uuzaji wa asali
βœ… Huhifadhi mazingira kupitia uchavushaji unaofanywa na nyuki

🌍 Tuchukue hatua pamoja kulinda maisha ya jamii na tembo!





Matumizi bora ya ardhi kwa jamii zinazopakana na maeneo ya hifadhi ni njia mojawapo ya kupunguza migogoro baina ya watu ...
22/09/2025

Matumizi bora ya ardhi kwa jamii zinazopakana na maeneo ya hifadhi ni njia mojawapo ya kupunguza migogoro baina ya watu na wanyamapori hasa tembo.

Tunatoa wito kwa serikali za vijiji katika jamii zinazopakana na maeneo ya hifadhi kuzingatia mipango ya matumizi bora ya ardhi katika mipango yao ya maendeleo.

Kutoa elimu ya uhifadhi wa tembo na mazingira mashuleni husaidia kuwajengea watoto uelewa wa kutunza rasilimali za asili...
15/09/2025

Kutoa elimu ya uhifadhi wa tembo na mazingira mashuleni husaidia kuwajengea watoto uelewa wa kutunza rasilimali za asili, kuishi kwa usalama na tembo, na kupunguza migogoro kati ya binadamu na tembo huku tukiandaa wahifadhi wa baadaye.

Tujenge kizazi cha sasa na baadaye kwaajili ya uhifadhi endelevu. Tanzanian Elephant Foundation

Address

Aga Khan Road
Old Moshi
6502

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Maisha na Tembo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Maisha na Tembo:

Share