Tanzania Sicklecell Warriors

Tanzania Sicklecell Warriors Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Tanzania Sicklecell Warriors, Nonprofit Organization, Mwanza.

TASIWA is an organisation based on education and awareness about sickle cell disease but also giving hope to the families that have been affected direct or indirect by sickle cell disease

Sikoseli sio kikomo cha mtu kutimiza ndoto zao! Wanaoishi na changamoto hii wana uwezo mkubwa wa kusoma, kufanya kazi, k...
04/06/2026

Sikoseli sio kikomo cha mtu kutimiza ndoto zao! Wanaoishi na changamoto hii wana uwezo mkubwa wa kusoma, kufanya kazi, kupenda, na kuwa viongozi wakubwa kwenye jamii yetu. 🩺❤️

Kinachohitajika si huruma, bali ni fursa sawa, upendo, lishe bora, na matibabu sahihi ya mapema. Unyanyapaa unatokana na ukosefu wa uelewa, na ni wajibu wetu sote k**a jamii kusimama nao bega kwa bega ili kuwajengea hali ya kujiamini na matumaini mapya.

Hakuna ndoto inayoweza kuzimwa na seli mundu pale ambapo jamii inatoa ushirikiano na upendo wa dhati. Tuunge mkono juhudi hizi za kueneza uelewa!

Tusaidie kusambaza ujumbe huu: Gonga 'Like' na 'Share' poster hii ili kuwafikia watu wengi zaidi na kutengeneza jamii yenye uelewa na usawa. 🔄💬


🩸 Sikoseli si udhaifu, ni hali ya kiafya inayohitaji uelewa, msaada na huduma sahihi.Maumivu ya mara kwa mara, uchovu mk...
03/06/2026

🩸 Sikoseli si udhaifu, ni hali ya kiafya inayohitaji uelewa, msaada na huduma sahihi.

Maumivu ya mara kwa mara, uchovu mkali, homa za mara kwa mara, ngozi kuwa ya njano, pamoja na kuvimba mikono au miguu ni baadhi ya dalili muhimu za ugonjwa wa sikoseli. Kutambua dalili hizi mapema kunaweza kusaidia kupata matibabu na ushauri unaofaa kwa wakati.

Elimu sahihi kuhusu sikoseli ni hatua muhimu katika kupunguza unyanyapaa, kuongeza uelewa wa jamii, na kuboresha maisha ya watu wanaoishi na hali hii. Tuendelee kujifunza, kuelimisha wengine na kuwapa matumaini wale wanaoathiriwa na sikoseli.

Maarifa yanaokoa maisha. Tambua dalili, chukua hatua. ❤️



🩸 Je, unalijua group lako la damu na hali yako ya sikoseli?Maarifa haya yanaweza kuwa hatua muhimu katika kupanga maisha...
02/06/2026

🩸 Je, unalijua group lako la damu na hali yako ya sikoseli?
Maarifa haya yanaweza kuwa hatua muhimu katika kupanga maisha ya familia yenye afya. Kufanya vipimo mapema kunakupa nafasi ya kufanya maamuzi sahihi na kuelewa hatari zinazoweza kujitokeza kwa watoto watakaozaliwa.
Elimu ni nguvu. Taarifa sahihi leo zinaweza kusaidia kujenga kizazi chenye afya kesho. Chukua hatua, fahamu hali yako, na wahimize wengine kufanya hivyo pia.


Living with sickle cell disease comes with challenges, but it also reveals extraordinary courage, resilience, and determ...
01/06/2026

Living with sickle cell disease comes with challenges, but it also reveals extraordinary courage, resilience, and determination. Every day, individuals living with sickle cell continue to pursue their dreams, overcome obstacles, and inspire those around them.

As reminds us, sickle cell disease does not define a person's future. It is a journey that showcases strength, perseverance, and the power of hope.

Let us continue to raise awareness, fight stigma, and support everyone affected by sickle cell disease. Together, we can build a more understanding and inclusive society.

💙 Every challenge faced is a testament to strength. 💙 Every victory achieved is a reason to celebrate. 💙 Every voice matters in the fight against sickle cell disease.

On May 21, 2026, TASIWA, accompanied by the Geita Regional NCD Coordinator, had the privilege of meeting with the Direct...
29/05/2026

On May 21, 2026, TASIWA, accompanied by the Geita Regional NCD Coordinator, had the privilege of meeting with the Director of the Health Department – Catholic Diocese of Geita to explore possible collaboration in the fight against sickle cell disease in the Geita Region.

Geita is one of the regions in the Lake Zone of Tanzania facing a significant burden of sickle cell disease, and we believe that joint efforts will play a vital role in ensuring communities receive accurate SCD education, patients access timely and appropriate treatment, healthcare providers are empowered with the necessary skills and resources, and families affected by sickle cell disease are economically supported.

This meeting was especially important for TASIWA as it reflects our commitment to strengthening collaboration with different stakeholders, including faith-based organizations, to expand our reach within communities. We had very positive and meaningful discussions that created a promising direction toward reaching and supporting more communities through collective action.


Msaada wa kweli huanza kwa kuelewa. Watu wanaoishi na sikoseli hawahitaji huruma pekee, wanahitaji kupendwa, kusikilizwa...
28/05/2026

Msaada wa kweli huanza kwa kuelewa.
Watu wanaoishi na sikoseli hawahitaji huruma pekee, wanahitaji kupendwa, kusikilizwa na kuungwa mkono kila siku. Neno jema, upendo na uwepo wetu vinaweza kuwa chanzo cha nguvu na matumaini kwao.
Tuendelee kutoa elimu, kuondoa unyanyapaa na kuwa sehemu ya mabadiliko chanya katika maisha ya watu wenye sikoseli.


🕌 Eid Mubarak from TASIWA On this special celebration of Eid Al-Adha, we wish everyone a joyful, peaceful, and blessed h...
26/05/2026

🕌 Eid Mubarak from TASIWA
On this special celebration of Eid Al-Adha, we wish everyone a joyful, peaceful, and blessed holiday filled with love and hope.
May this season inspire kindness, unity, good health, and the protection of rights and dignity for all people in our communities.

Together, we can continue creating a healthier and more inclusive future.

Sikoseli si mwisho wa maisha wala ndoto.Kwa uelewa sahihi, matibabu mapema na support kutoka kwa jamii, watu wanaoishi n...
26/05/2026

Sikoseli si mwisho wa maisha wala ndoto.
Kwa uelewa sahihi, matibabu mapema na support kutoka kwa jamii, watu wanaoishi na sikoseli wanaweza kuendelea kusoma, kufanya kazi na kutimiza malengo yao k**a wengine.
Tuchague kuwa sauti ya faraja, elimu na matumaini kwa mashujaa wetu wa sikoseli kila siku. ❤️


.scd

Kwa siku tatu mfululizo, tumekuwa tukitoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili kuwaongezea uelewa kuhusu ugon...
25/05/2026

Kwa siku tatu mfululizo, tumekuwa tukitoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili kuwaongezea uelewa kuhusu ugonjwa wa sikoseli na kuwajengea uwezo wa kuwasaidia watu wenye sikoseli pamoja na familia zao.

Mafunzo haya yamelenga kuimarisha utambuzi wa mapema, kuwaunganisha wagonjwa kwenye vituo vya afya, pamoja na makundi saidizi kwa ajili ya msaada na huduma zaidi.

Mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa KETAN unaofadhiliwa na Pierre Fabre Foundation, wenye lengo la kuboresha maisha ya watu wenye sikoseli kupitia utambuzi wa mapema kwa watoto chini ya miaka mitano ili kuhakikisha wanaanza matibabu kwa wakati.

Wahudumu wa afya ngazi ya jamii ni kiungo muhimu sana katika kuhakikisha jamii inapata elimu sahihi, watoto wanatambuliwa mapema, na wagonjwa wanaunganishwa na huduma stahiki kwa wakati.

Sisi TASIWA tunaendelea kuthamini mchango mkubwa wa wahudumu hawa, na kila tunapopata nafasi ya kuwafikia tunaendelea kuwajengea uwezo ili wawe sehemu ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii ya watu wenye sikoseli, hususan watoto ambao ndio kundi lenye uhitaji mkubwa wa ulinzi na huduma za karibu.


Tarehe 18-20/05  tulipata nafasi ya kufanya mafunzo kwa watoa huduma wa afya 25 kutoka Hospitali ya Rufaa ya mkoa Sekou-...
22/05/2026

Tarehe 18-20/05 tulipata nafasi ya kufanya mafunzo kwa watoa huduma wa afya 25 kutoka Hospitali ya Rufaa ya mkoa Sekou-Toure k**a sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Securing Health, Improving Lives.

Mafunzo haya yanatekelezwa na TASIWA kwa kushirikiana na Baylor Foundation Tanzania kupitia ufadhili wa Bristol Myers Squibb Foundation, yakiwa na lengo la kuimarisha usimamizi wa huduma za sickle cell na kuhakikisha watoto 400 wanaonufaika na bima ya afya kupitia mradi huu wanapata huduma bora, sahihi na kwa wakati.

Kupitia ushirikiano huu, tunaendelea kujenga mfumo imara wa huduma utakaochangia kupunguza vifo na kuboresha maisha ya watoto na vijana wenye sickle cell.

Sambamba na hilo, wazazi na walezi wa watoto hawa wamewezeshwa elimu ya ujasiriamali na kuunganishwa katika vikundi ili kuweka msingi endelevu wa huduma na kuwawezesha kuendelea kulipia bima za afya za watoto wao hata baada ya kipindi cha mradi kuisha.

Kwa pamoja tunaendelea kuhakikisha afya inalindwa na maisha yanaboreshwa. 💙


Address

Mwanza

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255757418888

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Sicklecell Warriors posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share