16/12/2025
*Utangulizi*
Karibu tena ndugu Mwanachama wa Numet katika channel yetu ya ijue sheria ya Kazi. Kwa sehemu kubwa tumeichambua sheria ya kazi katika maeneo mbalimbali na kueleza dhana kadhaa kuhusiana na ajira. Mfululizo huu unaoanza kwenye makala ya leo tutakuwa tukijibu hoja na maswali mbalimbali yanayohusiana na ajira ambayo niliyapokea kwa njia ya Simu, e-mail na kuwashauri wadau,wanachama wetu husika. Ili kutoa mwanga kwa wanachama wote nimeona tuyajadili maswali haya na kuyatolea ufafanuzi.
Lengo langu ni kusaidia kwa kadri inavyowezekana wadau,wanachama wa sheria ya ajira yaani mwajiri na mfanyakazi kutimiza wajibu wao ili kupata haki zao. Karibu kwenye channel yetu ya NUMET ya leo inayokwenda kujibu swali linalosema:-
*JE, MWAJIRI ANAWEZA KUCHELEWESHA MSHAHARA ZAIDI YA SIKU NGAPI KISHERIA?*
(Ufafanuzi wa sheria kwa mfanyakazi na mwajiri)
Mishahara ni sehemu muhimu ya mkataba wa ajira. Ndiyo maana Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (The Employment and Labour Relations Act) imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara. Mpaka kufikia mwaka huu 2025, Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6 ya 2004 imerekebishwa. Kwa sheria ya sasa yaani Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, Sura 366, Toleo la Marejeo la mwaka 2023 na marekebisho yake ya 2025, kifungu kinachozungumzia Malipo ya Ujira/Mshahara (Payment of Remuneration) ni kifungu cha 28 ambacho kina vifungu vidogo vitano.
Aidha, Kifungu cha 28 (1) (a) cha ELRA SURA 366 YA 2023 ambacho katika ELRA Na. 6 ya 2004 kilikuwa kifungu cha 27 (1) (a) kinasema kwamba Mwajiri atalazimika kumlipa muajiriwa malipo yoyote ya ujira ambayo muajiriwa anastahili wakati wa masaa ya kazi kwenye eneo la kazi katika SIKU YA MALIPO ILIYOKUBALIWA.
Hii maana yake ni kwamba. Katika mkataba wa ajira, moja ya masuala ambayo Mwajiri anapaswa kukubilina na Muajiriwa ni pamoja na tarehe ya malipo ya ujira/mshahara.
1. sheria inasema mshahara lazima ulipwe ndani ya siku ngapi?
Kifungu cha 27(1) cha ELRA, 2004 kinasema:
Mwajiri lazima amlipe mfanyakazi kila baada ya siku 30 (yaani kila mwezi) au kulingana na makubaliano yaliyoko kwenye mkataba k**a italipwa kila wiki au kila baada ya siku 14 n.k. makubaliano yaliyopo kwenye mkataba ndio mwongozo.
Maana yake ni kuwa mshahara wa mwezi haupaswi kuzidi siku 30 bila kulipwa.
Hivyo,k**a tarehe ya malipo ni kila tarehe 25, basi ni lazima ulipwe kabla au siku hiyo na si wiki mbili baadaye au mwezi mwingine.
2. Je, kuchelewa kwa siku chache kunaruhusiwa?
Sheria ya Tanzania HAITOI muda wa uvumilivu (tolelance) kwa mwajiri kuchelewesha mshahara
Yaani:
Hakuna sehemu sheria inasema”mwajiri anaweza kuchelewa siku 3’’
Hakuna inaseema mwajiri anaweza kuchelewa wiki moja’’
Hakuna muda maalumu wa kusema kuchelewa kwa saa kadhaa au siku chache ni sawa.
Sheria inasema tu mshahara ulipwe muda uliokubaliwa.
Muda wowote unaozidi siku za kawaida za malipo unachukuliwa k**a kuchelewesha.
Hata hivyo kwa vitendo ,waajiri wengine huchelewesha kwa saa au siku 1-3 kutokana na changamoto za kibenki. Hilo hilo kuonekana au kuchukuliwa k**a technical delay k**a:
Huwa halijirudii rudii,Nikwasababu za kiufundi, si makusudi
Mfanyakazi anataarifiwa.
Lakini kisheria kuchelewa ni kuchelewa – na mfanyakazi anaweza kulalamika k**a itakuwa sugu.
3. kuchelewesha mshahara bila sababu ni kosa?
Ndiyo. Kifungu cha 27(2) cha sheria kinasema :
Mwajiri hatakiwi kuchelewesha mshahara bila sababu ya msingi .
K**a anachelewa mara kwa mara bila taarifa au bila sababu halali hiyo ni uvunjaji wa mkataba wa ajira.
1. sheria inasema mshahara lazima ulipwe ndani ya siku ngapi?
Kifungu cha 27(1) cha ELRA, 2004 kinasema:
Mwajiri lazima amlipe mfanyakazi kila baada ya siku 30 (yaani kila mwezi) au kulingana na makubaliano yaliyoko kwenye mkataba k**a italipwa kila wiki au kila baada ya siku 14 n.k. makubaliano yaliyopo kwenye mkataba ndio mwongozo.
Maana yake ni kuwa mshahara wa mwezi haupaswi kuzidi siku 30 bila kulipwa.
Hivyo,k**a tarehe ya malipo ni kila tarehe 25, basi ni lazima ulipwe kabla au siku hiyo na si wiki mbili baadaye au mwezi mwingine.
2. Je, kuchelewa kwa siku chache kunaruhusiwa?
Sheria ya Tanzania HAITOI muda wa uvumilivu (tolelance) kwa mwajiri kuchelewesha mshahara
Yaani:
Hakuna sehemu sheria inasema”mwajiri anaweza kuchelewa siku 3’’
Hakuna inaseema mwajiri ‘’mwajiri anaweza kuchelewa wiki moja’’
Hakuna muda maalumu wa kusema kuchelewa kwa saa kadhaa au siku chache ni sawa.
Sheria inasema tu mshahara ulipwe muda uliokubaliwa.
Muda wowote unaozidi siku za kawaida za malipo unachukuliwa k**a kuchelewesha.
Hata hivyo kwa vitendo ,waajiri wengine huchelewesha kwa saa au siku 1-3 kutokana na changamoto za kibenki. Hilo hilo kuonekana au kuchukuliwa k**a technical delay k**a:
Huwa halijirudii rudii
Nikwasababu za kiufundi, si makusudi
Mfanyakazi anaarifiwa
Lakini kisheria kuchelewa ni kuchelewa – na mfanyakazi anaweza kulalamika k**a itakuwa sugu
3. kuchelewesha mshahara bila sababu ni kosa?Ndiyo. Kifungu cha 27(2) cha sheria kinasema :
Mwajiri hatakiwi kuchelewesha mshahara bila sababu ya msingi .
K**a anachelewa mara kwa mara bila taarifa au bila sababu halali hiyo ni uvunjaji wa mkataba wa ajira.
Mfanyakazi anahaki ya:
Kutoa malalamiko(grievance).
Kufungua shauri CMA endapo kuchelewa ni kitendo cha kujirudia rudia na bila taarifa yoyote (un fair labour practice)
4. sababu gani pekee zinakubalika kuchelewesha malipo?
Sheria inakubali sababu za msingi ikiwemo :
Changamoto ya kiufundi benki
Makosa ya mfumo wa payroll
Hali ya dharura isiyoepukika (force majeure)
Makubaliano ya maandishi pande zote mbili
Lakini mambo k**a haya hayakubaliki:
Mwajili kukosa hela.
Biashara mbaya.
kupunguza gharama kwa makusudi.
Mtazamo wa tulieni tutawalipa hela yenu ipo pale pale.
Hizo haziitwi sababu za msingi kisheria
5. *Mfanyakazi afanye nini* akicheleweshewa mshahara? Mara kwa mara?
*Hatua sahihi ni:*
Muulize mwajiri kwa maandishi kujua sababu na tarehe halisi ya malipo
Andika barua ya malalamiko
Wasilisha shauri commission for mediation and arbitration (CMA)
Kwa madai ya:Unfair practice
*MUHIMU KUJUA*
Mwajiri hana haki ya kisheria kuchekewesha mshahara zaidi ya siku za kawaida za malipo bila sababu ya msingi.
*Tutaendelea wiki Ijayo* na elimu hii
Asanteni sana.
"United we bargain, divided we beg"
Kumbuka ‘kutokujua sheria si utetezi iwapo utatenda kosa lolote’ tafuta maarifa sahihi ya kisheria yakusaidie kufanya maamuzi sahihi kila siku Muhimu.
Nakutakia siku njema ndugu yangu.
Wako
Marco Zawadi Numet Taifa Idara ya Elimu na Mafunzo