Numet Tanzania

Numet Tanzania Chama Cha wafanyakazi wa Tasnia ya Nishati na Madini Tanzania (National Union of Mine and Energy workers of Tanzania) - NUMET. Namba ya Usajili ni 029.

Chama kilianzishwa tarehe 01.10.2011, na kusajiliwa tarehe 20.02.2013. Tuna wanachama 3500 nchini.

Group photos members with Guest of Honor , May Day 2026
09/05/2026

Group photos members with Guest of Honor , May Day 2026

09/05/2026
May Day 2026, Sengerema
09/05/2026

May Day 2026, Sengerema

09/05/2026
We are Hiring
23/04/2026

We are Hiring

General Manager, Mwenyekiti na Katibu wa tawi la NUMET North Mara Gold Mine Ltd, wakifurahia jambo baada ya kusaini CBA ...
23/03/2026

General Manager, Mwenyekiti na Katibu wa tawi la NUMET North Mara Gold Mine Ltd, wakifurahia jambo baada ya kusaini CBA mpya mwaka 2026. Masilahi bora ya wafanyakazi ndo kipaumbele namba moja cha NUMET.

North Mara Gold Mine and NUMET did it again this year . CBA Review 2026.
23/03/2026

North Mara Gold Mine and NUMET did it again this year . CBA Review 2026.

Mwongozo wa maadhimisho ya Mei Mosi 2026.  NUMET tutafanya Maadhimisho kitaifa katika maeoneo mawili. 1. Kwa kushirikian...
28/02/2026

Mwongozo wa maadhimisho ya Mei Mosi 2026. NUMET tutafanya Maadhimisho kitaifa katika maeoneo mawili. 1. Kwa kushirikiana na serikali, tutafanya maadhimisho yetu Mkoani Njombe. Na , 2. kwa lengo la kuhakikisha wafanyakazi wengi wanashiriki, tutakuwa na maadhimisho ya Kitaifa mjini Sengerema.

Kwa maelezo zaidi, soma mwongozo.

*Utangulizi* Karibu tena ndugu Mwanachama wa Numet katika channel yetu ya ijue sheria ya Kazi. Kwa sehemu kubwa tumeicha...
16/12/2025

*Utangulizi*

Karibu tena ndugu Mwanachama wa Numet katika channel yetu ya ijue sheria ya Kazi. Kwa sehemu kubwa tumeichambua sheria ya kazi katika maeneo mbalimbali na kueleza dhana kadhaa kuhusiana na ajira. Mfululizo huu unaoanza kwenye makala ya leo tutakuwa tukijibu hoja na maswali mbalimbali yanayohusiana na ajira ambayo niliyapokea kwa njia ya Simu, e-mail na kuwashauri wadau,wanachama wetu husika. Ili kutoa mwanga kwa wanachama wote nimeona tuyajadili maswali haya na kuyatolea ufafanuzi.

Lengo langu ni kusaidia kwa kadri inavyowezekana wadau,wanachama wa sheria ya ajira yaani mwajiri na mfanyakazi kutimiza wajibu wao ili kupata haki zao. Karibu kwenye channel yetu ya NUMET ya leo inayokwenda kujibu swali linalosema:-

*JE, MWAJIRI ANAWEZA KUCHELEWESHA MSHAHARA ZAIDI YA SIKU NGAPI KISHERIA?*
(Ufafanuzi wa sheria kwa mfanyakazi na mwajiri)
Mishahara ni sehemu muhimu ya mkataba wa ajira. Ndiyo maana Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (The Employment and Labour Relations Act) imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara. Mpaka kufikia mwaka huu 2025, Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6 ya 2004 imerekebishwa. Kwa sheria ya sasa yaani Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, Sura 366, Toleo la Marejeo la mwaka 2023 na marekebisho yake ya 2025, kifungu kinachozungumzia Malipo ya Ujira/Mshahara (Payment of Remuneration) ni kifungu cha 28 ambacho kina vifungu vidogo vitano.

Aidha, Kifungu cha 28 (1) (a) cha ELRA SURA 366 YA 2023 ambacho katika ELRA Na. 6 ya 2004 kilikuwa kifungu cha 27 (1) (a) kinasema kwamba Mwajiri atalazimika kumlipa muajiriwa malipo yoyote ya ujira ambayo muajiriwa anastahili wakati wa masaa ya kazi kwenye eneo la kazi katika SIKU YA MALIPO ILIYOKUBALIWA.

Hii maana yake ni kwamba. Katika mkataba wa ajira, moja ya masuala ambayo Mwajiri anapaswa kukubilina na Muajiriwa ni pamoja na tarehe ya malipo ya ujira/mshahara.

1. sheria inasema mshahara lazima ulipwe ndani ya siku ngapi?

Kifungu cha 27(1) cha ELRA, 2004 kinasema:
Mwajiri lazima amlipe mfanyakazi kila baada ya siku 30 (yaani kila mwezi) au kulingana na makubaliano yaliyoko kwenye mkataba k**a italipwa kila wiki au kila baada ya siku 14 n.k. makubaliano yaliyopo kwenye mkataba ndio mwongozo.

Maana yake ni kuwa mshahara wa mwezi haupaswi kuzidi siku 30 bila kulipwa.

Hivyo,k**a tarehe ya malipo ni kila tarehe 25, basi ni lazima ulipwe kabla au siku hiyo na si wiki mbili baadaye au mwezi mwingine.

2. Je, kuchelewa kwa siku chache kunaruhusiwa?
Sheria ya Tanzania HAITOI muda wa uvumilivu (tolelance) kwa mwajiri kuchelewesha mshahara
Yaani:
Hakuna sehemu sheria inasema”mwajiri anaweza kuchelewa siku 3’’

Hakuna inaseema mwajiri anaweza kuchelewa wiki moja’’

Hakuna muda maalumu wa kusema kuchelewa kwa saa kadhaa au siku chache ni sawa.

Sheria inasema tu mshahara ulipwe muda uliokubaliwa.

Muda wowote unaozidi siku za kawaida za malipo unachukuliwa k**a kuchelewesha.

Hata hivyo kwa vitendo ,waajiri wengine huchelewesha kwa saa au siku 1-3 kutokana na changamoto za kibenki. Hilo hilo kuonekana au kuchukuliwa k**a technical delay k**a:

Huwa halijirudii rudii,Nikwasababu za kiufundi, si makusudi

Mfanyakazi anataarifiwa.

Lakini kisheria kuchelewa ni kuchelewa – na mfanyakazi anaweza kulalamika k**a itakuwa sugu.

3. kuchelewesha mshahara bila sababu ni kosa?

Ndiyo. Kifungu cha 27(2) cha sheria kinasema :

Mwajiri hatakiwi kuchelewesha mshahara bila sababu ya msingi .

K**a anachelewa mara kwa mara bila taarifa au bila sababu halali hiyo ni uvunjaji wa mkataba wa ajira.

1. sheria inasema mshahara lazima ulipwe ndani ya siku ngapi?

Kifungu cha 27(1) cha ELRA, 2004 kinasema:
Mwajiri lazima amlipe mfanyakazi kila baada ya siku 30 (yaani kila mwezi) au kulingana na makubaliano yaliyoko kwenye mkataba k**a italipwa kila wiki au kila baada ya siku 14 n.k. makubaliano yaliyopo kwenye mkataba ndio mwongozo.

Maana yake ni kuwa mshahara wa mwezi haupaswi kuzidi siku 30 bila kulipwa.

Hivyo,k**a tarehe ya malipo ni kila tarehe 25, basi ni lazima ulipwe kabla au siku hiyo na si wiki mbili baadaye au mwezi mwingine.

2. Je, kuchelewa kwa siku chache kunaruhusiwa?
Sheria ya Tanzania HAITOI muda wa uvumilivu (tolelance) kwa mwajiri kuchelewesha mshahara
Yaani:
Hakuna sehemu sheria inasema”mwajiri anaweza kuchelewa siku 3’’
Hakuna inaseema mwajiri ‘’mwajiri anaweza kuchelewa wiki moja’’
Hakuna muda maalumu wa kusema kuchelewa kwa saa kadhaa au siku chache ni sawa.
Sheria inasema tu mshahara ulipwe muda uliokubaliwa.

Muda wowote unaozidi siku za kawaida za malipo unachukuliwa k**a kuchelewesha.
Hata hivyo kwa vitendo ,waajiri wengine huchelewesha kwa saa au siku 1-3 kutokana na changamoto za kibenki. Hilo hilo kuonekana au kuchukuliwa k**a technical delay k**a:
Huwa halijirudii rudii
Nikwasababu za kiufundi, si makusudi
Mfanyakazi anaarifiwa
Lakini kisheria kuchelewa ni kuchelewa – na mfanyakazi anaweza kulalamika k**a itakuwa sugu
3. kuchelewesha mshahara bila sababu ni kosa?Ndiyo. Kifungu cha 27(2) cha sheria kinasema :
Mwajiri hatakiwi kuchelewesha mshahara bila sababu ya msingi .
K**a anachelewa mara kwa mara bila taarifa au bila sababu halali hiyo ni uvunjaji wa mkataba wa ajira.

Mfanyakazi anahaki ya:
Kutoa malalamiko(grievance).

Kufungua shauri CMA endapo kuchelewa ni kitendo cha kujirudia rudia na bila taarifa yoyote (un fair labour practice)

4. sababu gani pekee zinakubalika kuchelewesha malipo?
Sheria inakubali sababu za msingi ikiwemo :

Changamoto ya kiufundi benki
Makosa ya mfumo wa payroll
Hali ya dharura isiyoepukika (force majeure)
Makubaliano ya maandishi pande zote mbili

Lakini mambo k**a haya hayakubaliki:

Mwajili kukosa hela.

Biashara mbaya.

kupunguza gharama kwa makusudi.

Mtazamo wa tulieni tutawalipa hela yenu ipo pale pale.

Hizo haziitwi sababu za msingi kisheria

5. *Mfanyakazi afanye nini* akicheleweshewa mshahara? Mara kwa mara?

*Hatua sahihi ni:*

Muulize mwajiri kwa maandishi kujua sababu na tarehe halisi ya malipo

Andika barua ya malalamiko

Wasilisha shauri commission for mediation and arbitration (CMA)
Kwa madai ya:Unfair practice

*MUHIMU KUJUA*
Mwajiri hana haki ya kisheria kuchekewesha mshahara zaidi ya siku za kawaida za malipo bila sababu ya msingi.

*Tutaendelea wiki Ijayo* na elimu hii
Asanteni sana.

"United we bargain, divided we beg"

Kumbuka ‘kutokujua sheria si utetezi iwapo utatenda kosa lolote’ tafuta maarifa sahihi ya kisheria yakusaidie kufanya maamuzi sahihi kila siku Muhimu.

Nakutakia siku njema ndugu yangu.

Wako

Marco Zawadi Numet Taifa Idara ya Elimu na Mafunzo

Address

P. O. Box 11956, Capripoint Mwanza
Mwanza

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

+255763415557

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Numet Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Numet Tanzania:

Share