Al haq TV

Al haq TV MWANGAZA KWA KILA MTU

05/06/2026
05/06/2026

Rais Samia Suluhu Hassan ameeleza kuwa Tanzania haiko chini ya vikwazo vyovyote, na kwamba serikali inaendelea kujipanga kuchochea maendeleo.

01/06/2026

Vurugu zimeripotiwa kutokea katika Manispaa ya Kigoma Ujiji baada ya ajali iliyohusisha Dereva wa bodaboda anaejulikana kwa jina maarufu PISI KALI kugongwa na gari katika Mtaa wa Shirika.

Kwa mujibu wa taarifa za awali, tukio hilo limezua hasira kwa Madereva wa bodaboda ambao waliokusanyika eneo la ajali wakipinga tukio hilo, katika hali ya ghasia, inadaiwa baadhi yao walilichoma moto gari hilo wakiamini Dereva mwenzao amefariki papo hapo.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limefika eneo la tukio na kuanza kuwatawanya Watu hao huku likidhibiti hali ya usalama na kurejesha utulivu katika eneo hilo.

Polisi wamesema uchunguzi unaendelea kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo pamoja na kuthibitisha hali ya afya ya Dereva wa bodaboda aliyegongwa huku wakiwataka Wananchi kuwa watulivu na kuepuka kujichukulia sheria mkononi.

16/05/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila, amewataka Vijana wasiharibu maisha yao kwa Siasa na propaganda za chuki, badala yake wajikite katika jitihada kwa kuwa ndio siri pekee ya mafanikio katika maisha yao.

Chalamila amesisitiza maisha si mepesi k**a wengi wanavyodhani ni magumu na hayako kwenye propaganda ya vinywa na maneno mengi, bali lazima kupitia magumu ili kufanikiwa.

Chalamila ameeleza hayo leo, Mei 16, 2026 wakati akizungumza katika Kongamano la Vijana wa Vyuo Vikuu lililobeba ujumbe wa Never Again, ambapo amesema, "pamoja na kupata elimu mnayoipata leo, mchawi wa kweli ni kujimudu kimaisha na namna pekee ya kujimudu kimaisha ni kuyatafsiri maisha kwa namna ya kipekee," amesema Chalamila.

Pamoja na hayo, Chalamila ameambatanisha maneno yake hayo na nasaha kwa Vijana kuwa, inasikitisha kuona Vijana wanaonyesha chuki dhidi ya Watu sio kwa sababu waliwakosea bali kwa kuwa wamepewa nafasi za Uongozi Serikalini.

16/05/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Mwanza unaboreshwa na kujengwa katika hadhi ya kimataifa ili kuendana na hadhi ya jiji la Mwanza k**a kitovu muhimu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa.

Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu hoja ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza iliyowasilishwa na Mbunge wa Magu, Mhe. Boniventura Kiswaga, katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwenye Kikao cha 28 cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 13, leo Mei 13, 2026.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza na imeendelea kufanya jitihada mbalimbali kuhakikisha unakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa pamoja na kukidhi viwango vya kimataifa.

“Zipo jitihada ambazo zimekuwa zikifanyika kuhakikisha kwamba uwanja wa ndege wa Mwanza unaendana na hadhi ya Mwanza k**a kitovu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea na mazungumzo ya kuongeza eneo la uwanja huo ili kuwezesha upanuzi wa njia ya kurukia ndege (runway) pamoja na maboresho mengine muhimu ya miundombinu.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu amesema Serikali imekubaliana kujenga jengo jipya la abiria litakalokuwa na hadhi ya kimataifa na kuendana na mahitaji ya muda mrefu ya uwanja huo.

“Imekuja kukubalika kwamba tujenge jengo ambalo halitahitaji kubomolewa tena baada ya muda mfupi, bali jengo lenye hadhi na viwango vya viwanja vya ndege vya kimataifa,” amesema.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea na mpango huo sambamba na utekelezaji wa miradi mingine ya viwanja vya ndege nchini, huku akisisitiza kuwa dhamira ya kuifanya Mwanza kuwa kitovu kikubwa cha uchumi kupitia usafiri wa anga ipo pale pale.

Waziri Mkuu amesema Serikali itafanya kikao maalumu na wabunge wa Mkoa wa Mwanza pamoja na wizara husika ili kuondoa changamoto zilizokuwa zikikwamisha utekelezaji wa mradi huo na kuruhusu hatua zinazofuata kuendelea.

16/05/2026

Mwananchi mmoja aitwaye Athuman Ahmed Hassan, mkazi wa Kata ya Pai, Kijiji cha Ikova wilayani Kondoa, amelalamikia Jeshi la Polisi kwa madai ya kuchukua mali zake zote kufuatia tuhuma za wizi zilizomtuhumu. Akizungumza kwa masikitiko, Athuman amesema tukio hilo lilitokea tarehe 24 mwezi wa kwanza mwaka huu, ambapo askari walifika nyumbani kwake na kubeba vitu vyote vya biashara pamoja na mali za ndani.

Amesema alikuwa akijishughulisha na biashara ya duka pamoja na mashine ya kusaga na kukoboa nafaka, lakini polisi walichukua kila kitu hadi chakula na magodoro, hali iliyomwacha yeye na familia yake katika mazingira magumu ya maisha.

Athuman ameongeza kuwa yeye ndiye anayewatunza wadogo zake wanne wanaosoma baada ya wazazi wao kufariki dunia, na kwa sasa hana uwezo tena wa kuihudumia familia hiyo kutokana na kupoteza vitega uchumi vyake vyote. Ameiomba serikali pamoja na Mheshimiwa Waziri Mkuu kusaidia kupata haki yake na kurejeshewa maisha yake ya kawaida.

Address

SLP 319
Mwandiga

Telephone

+255754850604

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Al haq TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Al haq TV:

Share