14/08/2024
TALAKA AU KUACHANA KUNAWAATHIRI ZAIDI WATOTO.
Sehemu Ya 3
Tukiwa tunaelekea mwishoni mwa mada hii napenda tumalizie Kwa kuangalia mambo tunayopaswa kufanya baada ya kuachana au kutalikiana.
Unaweza ukajiuliza kwanini natumia maneno haya kuachana na kutalikiana. Talaka ni Kwa watu walioona na kuachana namaanisha watu walioishi pamoja bila kufunga ndoa.
I think hapo tunaelewana.
K**a ilivyo imani yangu siku zote ni kwamba kuachana sio vita. Hivyo kuachana kwa wazazi hakupaswi kuwa ndio mwisho wa ushirikiano wao katika malezi ya watoto wao.
Hata baada ya kuachana au kutalikiana wazazi wanapaswa kushirikiana katika majukumu ya kuwalea watoto wao kana kwamba bado wanaishi pamoja, japo ni kweli kwamba sio rahisi k**a tunavyoweza kutamka.
Sio rahisi kwasababu wazazi walioachana au kutalikiana hawatumii muda wao pamoja. Kila mtu anakuwa na harakati zake.
Na wazazi wengine wanataka kuwashirikisha watoto ugomvi wao. Wanawaeleza watoto wao juu ya ubaya wa baba au juu ya ubaya wa mama. Kosa hili maranyingi linafanywa na wazazi wa k**e, yaani kina mama.
Hii inaweza kupelekea mtoto akawa na chuki au dharau dhidi ya mzazi wake mwingine baada ya kulishwa sumu kuhusu madhaifu ya huyo mzazi.
Natoa rai yangu kwa wazazi, tusifanye ujinga huo. Tuwaache watoto wafurahie upendo wa pande zote mbili hata baada ya sisi kuachana au kutalikiana.
Kutalikiana kunaruhusiwa hata katika maandiko matakatifu lakini, tutalikiane kwa sababu za msingi na sio kwasababu ya fashion au kuchokana tu.
Maandiko yaasema...
MATHAYO 19:7,9
"Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini."
Bila shaka, huenda mengi zaidi yakahitajika kuliko kuvumilia tu katika ndoa ambayo haina furaha.
Muhimu tusiwatese watoto hata mara baada ya sisi wazazi kuachana au kutalikiana na maisha yetu yasiwe ya magomvi na uhasama usio na maana yoyote.
Tusiendeane kwa waganga ili kuharibiana maisha wala tusifanyiane visa ili kutuondoa kwenye njia sahihi za mafanikio tena ikiwezekana tusaidiane ili kila mmoja afanikiwe katika maisha yake.
Mafanikio ya wazazi ndio mafanikio ya watoto wetu.
Ahsante kwa kufuatilia mada hii na sina shaka k**a utaielewa mada hii basi utaenda kuwa mzazi ambaye ni mfano wa kuigwa katika jamii zetu.
Mungu awabariki sana.
A Dream By George G Francis
Join us 👇
Tanzania ChildFind Foundation
゚