10/08/2025
Mapema leo, CYD tumepokea tuzo kutoka kwa Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi ( .hmwinyi ), Rais wa Awamu ya Nane wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kutambua mchango wetu katika kufanikisha upatikanaji wa huduma za usajili wa matukio ya kijamii kwa wananchi wote waliokidhi vigezo.
Ujio wa tuzo hii ni matokeo ya safari ya muda mrefu ya kushirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar kusogeza huduma hizi karibu na wananchi, kutatua changamoto zilizokuwepo, na kuboresha mifumo ili kila mmoja afikiwe bila ubaguzi.
Tuzo hii, iliyopokelewa na Mkurugenzi wetu Bw. Hashim Pondeza, ni ishara ya dhamira yetu ya kuendeleza haki na ujumuishi wa makundi yote katika safari ya kufikia maendeleo ya kweli. 🌍💙
Shukran kwa wadau wote ambao walifanya kazi nasi kwa ukaribu ili kufanikisha juhudi hizi;
Cc: