25/01/2024
TAFADHALI JIANDIKISHE KUSHIRIKI,ASANTE
PWANI MEDICATION AWARENESS ORGANIZATION (PWAMAO)
JINA LA MRADI: KWA PAMOJA TUONGEZE MTAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA
WALENGWA: WAMILIKI WA DUKA LA DAWA MUHIMU, LAB, FAMASI, MARTENITY CLINIC NA ZAHANATI.
UTAMBULISHO
Shirika la Pwamao lilianzishwa mwaka 2009 na kusajiliwa mwaka 2019 kwa namba za usajili 15NGO/R/0645, Shirika hili lilianzishwa kwa madhumuni yafuatayo:-
1. Kutoa elimu ya afya
2. Kuhamasisha uzingatiaji wa ubora wa dawa na utunzaji mazingira
3. Kuongeza tija katika biashara ya Duka la Dawa Muhimu (DLDM) kwa kutoa mafunzo ya biashara, vitendea kazi na kuwaunganisha wamiliki wa asasi za mitaji/Fedha pia wasambazaji wa dawa na vifaa tiba.
4. Kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya dawa.
5. Kutoa elimu jinsi ya kuendesha duka la dawa muhimu(DLDM), Lab, Famasi, Martenity Clinic na Zahanati Kidigitali.
JAMBO LINALOPELEKEA MRADI KUFANYIKA
Swala la ukosefu wa dawa kwenye maduka ya dawa muhimu, zahanati na martenity clinic limekosa ufumbuzi kwa muda mrefu jambo ambalo linapelekea kudumaa kwa utoaji wa huduma za afya.
Kwa kuliona hilo PWAMAO tukishirikiana na wadau wengine wa afya tumeona vyema kutafuta ufumbuzi wa jambo hili kwa kuwaunganisha wadau wa afya na wasambazaji wa dawa na maduka ya jumla, taasisi za fedha (benki) kwa kutoa mikopo nafuu kwa wahitaji wa huduma hii.
PROGRAMU ZITAKAZOTUMIKA
1. Kuandaa mikutano ya wadau na kutambulisha mradi
2. Kwa kushirikiana na makampuni ya simu kupitia huduma za fedha tutaunda vikundi vikundi vidogo vya vikoba vya mtandaoni ambapo huduma za kifedha za mitandaoni zitatumika kupokelea marejesho ambapo kampuni husika itakuwa na mwakilishi wake atakae kua anaona kila hatua za miamala ya huduma za kifedha
3. Kwa kushirikiana na mamlaka za serikali tutahamasisha wadau wa afya kutumia huduma hii ya mikopo ya dawa ili tuweze kuwafikia wahitaji
4. Malipo yatakuwa kila siku kupitia huduma za kifedha za makampuni ya simu.
5. Kutoa elimu ya ujasiliamali na kutunza kumbukumbu za biashara kwa wadau wa afya kidigitali.
MALENGO YA MRADI
· Kupunguza ukosefu wa dawa kwenye maduka ya dawa na vituo vyote vya kutolea huduma.
· Kukuza mitaji ya wadau wa afya kupelekea kwa upatikanaji wa huduma ya uhakika.
· Kuendesha Biashara Kidigitali Kutumia Mifumo.
Tarehe ya Uzinduzi wa Mradi: 03/02/2024
Mahali: Venue Flex Garden,Kiguza
Muda:Saa 4 asubuhi Hadi saa 8 mchana
Mawasiliano: 0759 303 030 / 0682 432 429
JINA LA MRADI: KWA PAMOJA TUONGEZE MTAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA WALENGWA: WAMILIKI WA DUKA LA DAWA MUHIMU, LAB, FAMASI, MARTENITY CLINIC NA ZAHANATI. UTAMBULISHO Shirika la Pwamao lilianzishwa mwaka 2009 na kusajiliwa mwaka 2019 kwa namba za usajili 15NGO/R/0645, Shirika hili lilianzishwa kwa madhumu...