21/06/2025
Natumaini tupo wazima.
Tujikumbushe!
Leo ningependa tujifunze mambo 4 muhimu kabla ya kuanzisha mradi wako wa ngurue.
1.ENEO LA KUANZISHA MRADI WAKO
-Lazima upate eneo na Chagua eneo zuri ambalo halitakuwa ghubza ktk mradi wako.
-Usiweke mradi sehemu yenye upinzani wa Imani ya kidini au kwenye mlipuko wa magonjwa Kila wakati.
*2.MAHITAJI NA MATAKWA YA SOKO*.
-Lazima ujue mradi wako unahitaji kuwa wa namna gani je utazalisha watoto na kuuza au utakuwa unanenepesha na kuuza wakiwa wakubwa wanyama. Pia lazima ujue utauzia wapi (soko) siyo unafuga halafu hujui Kwa kuwapeleka.
3.AINA YA NGURUE UTAKAOFUGA
-Hapa lazima uzingatie mbegu utakayoichagua iendane na mazingira ya soko ulilonalo. Zipo mbegu nyingi k**a Duroc, large white , landrace, Camborough,saddleback,chotara na nyinginezo nyingi.
*4.UPATIKANAJI WA VYAKULA NA BEI ZAKE*
-Lazima ujue hapo kwenye eneo lako vyakula vipo? na bei zake zipoje je zipo chini au zipo juu. Namaanisha vyakula vya makundi yote wadogo,wenye mimba wanaonenepeshwa etc ukifahamu itakurahisishia ktk mfugo wako.
*5.UWEPO WA TAALUMA AU UZOEFU WA UFUGAJI WA NGURUE*
-Kabla hujafuga lazima ujiulize je unautaalamu wowote ktk ufugaji wa ngurue k**a huna je yupo mtaalamu ktk eneo lako ambae anaweza kukusaidia? Usifuge k**a bado huna utaalam au hakuna mtaalamu au mtu mwenye uzoefu wakuweza kukusaidia.
*MUHIMU;*
Aina nyingi za mbegu tulizonazo zimekaa Kwa muda mrefu hivyo zimepoteza vina Saba vyake kutokana na muingiliano wa vizazi mbali mbali.