Wana Foundation

Wana Foundation Advocating for Empowering youth with life skills, Inspiring good deeds and Creating lasting community impact.

Devoted;
To share smile, happiness and confidence with the children in need

To create a new version of students that will be able to change the world

04/06/2026
Eid al Adha Mubarak🕌☪️
27/05/2026

Eid al Adha Mubarak🕌☪️

24/05/2026

Hatuboi wala hatuchoshi just being WANA. If you ask me what I see in this video, I will tell you that “I see the shared laughs, genuine connection and mutual joy.”

What do you see here?!🤷🏾‍♂️

🫡

Wiki hii mioyo yetu imebeba maumivu ambayo hayaelezeki kwa maneno kiasi kwamba wengine tumeshindwa hata kulia. Tumempote...
16/05/2026

Wiki hii mioyo yetu imebeba maumivu ambayo hayaelezeki kwa maneno kiasi kwamba wengine tumeshindwa hata kulia. Tumempoteza ndugu yetu mpendwa Yohana Edwin (MC Mwakapalila a.k.a Mtumwa Asiye na Faida) kwa ajali. Mwakapalila alikuwa mwanga kwa wengi, sauti ya faraja kwa wenye huzuni, mfano wa kijana bora na nguzo imara kwetu.

Alikuwa mtu mwenye upendo wa kweli. Alipenda watu kwa moyo safi bila ubaguzi. Alikuwa kiongozi ambaye hakutafuta sifa bali alitafuta kuona watu wakisimama, wakitabasamu na wakiamini tena kwenye maisha. Alikuwa sehemu ya vijana waliowasha taa za matumaini kwa watu wengi waliokuwa wameyapoteza. Wapo wengi leo wanalia kimya kimya kwa sababu waliwahi kuguswa na wema wake, ushauri wake, upendo wake, msaada wake na moyo wake wa kipekee sana.

Ni ngumu kuamini kuwa sauti ya Mtumwa Asiye na Faida k**a alivyopenda kuitwa haitasikika tena, ucheshi na tabasamu lake hatutaliona tena na mikono yake haitainuliwa tena kusaidia wengine. Kifo kimetuibia mtu muhimu sana. Jamii ya wana-Mbeya imepoteza shujaa, marafiki tumepoteza rafiki wa kweli, familia ya MIMI NINA WATU na WANA FOUNDATION tumepoteza kipande cha moyo wetu.

Kuna watu huishi miaka mingi lakini hawaachi alama. Lakini MC Mwakapalila katika muda wake mfupi kwenye uso wa dunia ameacha historia ya upendo, utu na matendo makubwa yasiyofutika mioyoni mwa watu. Hakika Mauti imevikwa taji leo.

Pumzika kwa amani my Brother since childhood, Classmate, Mdau wa Matendo Mema na Kiongozi wa kweli. Ninamshukuru Mungu kwaajilili ya maisha yako na mara zote nilikupa maua yako kwa maneno ya kinywa changu kila uliposhiriki Events za WANA CHARITY. Umeondoka kwenye uso wa nchi lakini jina lako, matendo yako na upendo wako vitaendelea kuishi ndani yetu milele.

Safiri salama MC Mwakapalila🕊️😭

Jana tarehe 03/05/2026 Tukiwa na ndugu zetu AGF Songwe tulifanikiwa kukabidhi sadaka ya magodoro kwenye kituo cha watoto...
04/05/2026

Jana tarehe 03/05/2026 Tukiwa na ndugu zetu AGF Songwe tulifanikiwa kukabidhi sadaka ya magodoro kwenye kituo cha watoto wenye changamoto mbalimbali za kiafya kilichopo Ituha, Mbeya. Sadaka hii ni ahadi tuliyoitoa miezi kadhaa nyuma tulipotembelea kituoni hapo.

Mungu awabariki sana familia ya AGF Songwe na wote waliokuwa sehemu ya kufanikisha jambo hili. Mungu ayakumbuke maisha yenu.

MATENDO MEMA NI IBADA
Let’s keep doing good together

30/04/2026

Helping one person might not change the whole world, but it could change the world for that one person.

WANA FOUNDATION
Learn. Servere. Impact!

WANA CHARITY
Just Us For Love


Tarehe 25/04/2026 katika kuadhimisha Siku ya Matendo Mema baada ya kutoka kwa watoto yatima pia tulifanikiwa kutembelea ...
27/04/2026

Tarehe 25/04/2026 katika kuadhimisha Siku ya Matendo Mema baada ya kutoka kwa watoto yatima pia tulifanikiwa kutembelea nyumba yetu tunayoijenga katika kijiji cha Simambwe ikiwa ni sadaka yetu kwa ndugu yetu mwenye ulemavu. K**a tunavyoona kwenye picha tumejipiga piga tumefikia hapo na sasa tunatakiwa tuiezeke ili jamaa aingie kwenye nyumba yake. KARIBU SANA UWE SEHEMU YA KUFANIKISHA NDOTO HII KWA NDUGU HUYU. Lakini pia tulifika kumuona ndugu yetu Fredy naye tukamsalimia na kumpelekea Sahemu ya Sadaka Unga na Mchele.🙏🏾❤️

Kiukweli Mungu awabariki woooote! Na pia tujitahidi kurudisha muamko ule wa WANA CHARITY, tumepunguza sana kasi.

Asante nyingi kwa na walipendezesha sana siku yetu.

WANA CHARITY
JUST US FOR LOVE

Tarehe 25/04/2026 WANA CHARITY tulipata neema ya kutembelea kituo cha watoto cha Raising Orphanage Center, Simambwe - Mb...
26/04/2026

Tarehe 25/04/2026 WANA CHARITY tulipata neema ya kutembelea kituo cha watoto cha Raising Orphanage Center, Simambwe - Mbeya.

Kwanza kabisa kwa niaba ya watoto na walezi wao ninawashukuru wote kwa michango yenu, maombi yenu na sadaka zenu na zaidi sana kwa muda wenu wale wote mliofika kituoni kwaajili ya watoto.

Mungu awabariki sana na ayakumbuke maisha yenu, familia zenu, watoto wenu na uzao wenu siku zote. Sadaka hizi zikayabebe maisha yenu na zifanyike alama na ukumbusho mbele za Mungu na zaidi sana zikalete majibu kwenye maisha yenu.

Shukrani kwa na kwa kutupa nafasi ya kuwa sehemu ya mamilioni ya watu walioshiriki maadhimisho ya miaka 20 ya Siku ya Matendo Mema Duniani. Asante!

WANA CHARITY MBEYA
JUST US FOR LOVE❤️

K**a sehemu ya kuadhimisha siku ya Matendo Mema Duniani, Tarehe 25/04 Mimi na Wewe k**a Familia tutaungana pamoja kwenda...
13/04/2026

K**a sehemu ya kuadhimisha siku ya Matendo Mema Duniani, Tarehe 25/04 Mimi na Wewe k**a Familia tutaungana pamoja kwenda Kituo cha Watoto cha Raising Orphanage Center tukiwa na Sadaka yetu k**a Token ya Upendo. Halafu baada ya kuwaonyesha Upendo wetu watoto then tutaungana pamoja na kutembelea Nyumba tuliyokubaliana kumjengea ndugu yetu Fredy ambaye ni Mlemavu. Tutaenda kuona imefikia wapi.

Weka Sadaka yako k**a Token ya Upendo.
M-Pesa: 0746156319
Jina: Frank Mwainyekule

Wana Charity
Just Us For Love

Partners: & AGF Songwe

Honored to participate in the Good Deeds Day Leadership Conference. It was a valuable opportunity to connect, learn and ...
09/03/2026

Honored to participate in the Good Deeds Day Leadership Conference. It was a valuable opportunity to connect, learn and reflect on how we can strengthen the future of our organization, collaborate with the organizations around us and better serve and inspire our community. Together we continue building partnerships that inspire Good Deeds, Growth, Leadership and Lasting impact.

Good Deeds Day 20th Anniversary👏🏾


@

Address

Mbeya

Telephone

+255692328552

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wana Foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Wana Foundation:

Shortcuts

Share