08/09/2026
Mjasiriamali: Tabia gani isiyofaa ungependa kuwaomba radhi wateja?.....
Rafiki yangu, tabia moja ambayo mjasiriamali anapaswa kuomba radhi kwa wateja wake ni kuwapuuza baada ya kupata pesa zao.
Mteja hakupaswi kuhisi kwamba ulikuwa unamhitaji mpaka aliponunua, halafu baada ya hapo humjali tena.
Ukimchelewesha, usipomjibu, ukimpa bidhaa isiyo sahihi au ukikosea huduma, kubali kosa na sema “samahani.” Usitafute visingizio.
“Mteja anaweza kusamehe kosa lako, lakini ni vigumu kusahau namna ulivyomtendea ulipokosea.”
Mjasiriamali, jiulize:
Ni tabia gani katika huduma yako ambayo k**a ungekuwa mteja, ungependa muuzaji akuombe radhi?
Mabadiliko ya biashara yanaweza kuanza na “Samahani, nilikosea. Nifanye nini kurekebisha?”
Mimi nafundisha ujasiriamali, karibu tuyajengeeee!