11/11/2025
TANGAZO
==========
*RAISING AND AWAKENING ORGANIZATION (RAO)*
*TAARIFA KWA UMMA*
Raising and Awakening Organization (RAO), imesajiliwa chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 (Usajili Na. 00NGO/R/5083), inapenda kuwataarifu umma, makanisa, na wadau wote kuwa inaendesha mradi maalum unaoitwa *Raising Orphanage Center* – unaolenga kusaidia *watoto yatima, wajane, watu wenye ulemavu, wagonjwa, na watoto wanaoishi katika mazingira magumu*.
Kwa sasa, mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya *Dar es Salaam (Goba Kibululu)* na *Mbeya (Simambwe )*, huku kukiwa na mpango wa kuupanua katika maeneo mengine ya Tanzania Bara.
Tunaikaribisha jamii, taasisi, na washirika wote wenye mioyo ya huruma kushiriki nasi k**a *wawezeshaji, wahisani au washirika* katika dhamira hii ya kurejesha tumaini na kutoa msaada kwa makundi yaliyo katika uhitaji mkubwa.
*Tujenge jamii yenye huruma, upendo na ustahimilivu – kwa pamoja.*
*Makao Makuu:*
Goba Kibululu, Ubungo – Dar es Salaam
*Mawasiliano:*
Simu: +255 758 229529 / +255 683 406193
Barua pepe: [email protected] / [email protected]
*Kurasa za Facebook:*
- Raising Orphanage Center Rao – Goba Kibululu, Dar es Salaam
- Raising Orphanage Center – Silmambwe Mbeya Tanzania
*Instagram:*
- raising_watoto_yatima_mbeya
- raising_kituo_cha_watoto_yatima_goba_kibululu_dsm tz
*Kauli Mbiu:*
*"Kwa jamii yenye ustahimilivu – Tunamsha, Tunainua.