27/05/2026
Leo tarehe 26 Mei 2026, KIEF kwa kushirikiana na wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TeNMeT) tumekutana Sea Shells Hotel, Millennium Tower, Dar es Salaam kwa kikao cha Community of Practice (CoP).
Mada Kuu ilikuwa ni: Changamoto za Mabadiliko ya Tabia ya Nchi katika Sekta ya Elimu nchini Tanzania.
Kikao hiki cha CoP kimewaleta pamoja wataalamu na wadau wa elimu kujadili kwa kina jinsi mabadiliko ya tabia ya nchi yanavyoathiri upatikanaji wa elimu bora miundombinu kuharibiwa na mafuriko, ratiba za masomo kuvurugika, na usalama wa chakula mashuleni.
Hatua zinazofuata: Kukamilisha ripoti ya research na kuandaa mapendekezo ya Action Plan kwa ajili ya wadau wa elimu nchini.
Elimu himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabia ya nchi inawezekana kupitia ushirikiano.
DarEsSalaam