TAEFI

TAEFI A youth lead a non-governmental organization dedicated to providing education and support on epilepsy.

Our vision is to become the number one youth platform in Tanzania that advocate, support, research and provide new therapies and education for epilepsy.

maswali mengi yaliyokosa majibu.Kila siku, wapambanaji wa kifafa huishi na hali ya kutokujua:Itatokea lini? Wapi? Nitapa...
11/05/2026

maswali mengi yaliyokosa majibu.
Kila siku, wapambanaji wa kifafa huishi na hali ya kutokujua:
Itatokea lini? Wapi? Nitapata msaada? Watanionaje?
Hii si hofu ya kubuni ni maisha yetu ya kila siku.
Lakini ukweli ni huu:
Kifafa si aibu. Ni hali ya kiafya.
Tunahitaji kubadilisha mtazamo:
๐Ÿ”น Elewa
๐Ÿ”น Saidia
๐Ÿ”น Kubali
Jamii ikibadilika, hofu inapungua.

๐Ÿ’œ

Leo tunasherehekea nguvu ya mama ๐ŸŒMama si tu mlezini daktari wa kwanza, mlinzi, na moyo wa familia.Kwa familia zenye wap...
10/05/2026

Leo tunasherehekea nguvu ya mama ๐ŸŒ
Mama si tu mlezi
ni daktari wa kwanza, mlinzi, na moyo wa familia.
Kwa familia zenye wapambanaji wa kifafa, mama huwa:
โœ”๏ธ Mtu wa kwanza kugundua dalili
โœ”๏ธ Msimamizi wa matibabu kila siku
โœ”๏ธ Nguzo ya faraja wakati wa degedege
โœ”๏ธ Sauti ya kupambana na unyanyapaa
Kuna mapambano mengi mama hupitia kimya kimyaโ€ฆ
lakini bado anaendelea kusimama imara kwa ajili ya watoto wake.
Tunawaona. Tunawathamini. Tunawashukuru ๐Ÿ’œ
๐Ÿ‘‰ Leo, tunakuambia mama โ€œAHSANTEโ€ kwa kila alichofanya hata yale ambayo hukuwahi kuyaona.

๐Ÿ’œ

Kazi ni haki, siyo upendeleo.Katika kuadhimisha International Workers' Day, tunakumbushana kuwa watu wanaoishi na kifafa...
01/05/2026

Kazi ni haki, siyo upendeleo.
Katika kuadhimisha International Workers' Day, tunakumbushana kuwa watu wanaoishi na kifafa wana uwezo wa kufanya kazi kikamilifu k**a wengine wote.
Changamoto siyo uwezo wao
๐Ÿ‘‰ Ni uelewa wa jamii
๐Ÿ‘‰ Ni mazingira ya kazi
๐Ÿ‘‰ Ni mtazamo wa waajiri
Tusibague. Tushirikishe. Tusaidie.
๐ŸŸฃ Mtu mwenye kifafa akiwa mazingira salama na support sahihi, anaweza kudeliver k**a wengine.

๐Ÿ’œ

04/04/2026

๐Ÿ”ฅ Ndoa si ya watu wawili tuโ€ฆ ni muunganiko wa historia mbili za familia ikiwemo afya.
Unapochagua mwenza, unachagua pia mazingira aliyokulia, misingi yakeโ€ฆ na background ya kiafya ya familia yake.
Je, umejiuliza:
โœ”๏ธ Kuna magonjwa ya kurithi kwenye familia?
โœ”๏ธ Kuna hali endelevu (chronic conditions) k**a kifafa, kisukari au presha?
โœ”๏ธ Familia inauelewa gani wa ku-support hali hizi?
๐Ÿ’ก Haya si mambo ya kuogopa ni mambo ya kuyajua mapema ili kufanya maamuzi sahihi na kujenga ndoa imara.
Usikose mjadala huu:
๐Ÿ“บ Kipindi ni KILINGE CHA FAMILIA
๐Ÿ—“๏ธ April 5
โฐ Saa 3:00 Usiku
๐Ÿ“ก Channel ni UTV
โš ๏ธ Ukichagua bila kujua, unaingia bila mkakati.
Chagua kwa uelewa.

We showed up as runners.We stood out as epilepsy fighters. ๐Ÿ’œ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธGrateful for the invitation to the Run for Your Heart Ma...
02/04/2026

We showed up as runners.
We stood out as epilepsy fighters. ๐Ÿ’œ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ
Grateful for the invitation to the Run for Your Heart Marathon by Saifee Hospital Tanzania.
Thank you for valuing our health and for supporting awareness that goes beyond one condition.
Together, we raise awareness. Together, we build healthier communities.



๐Ÿ’œ

๐Ÿ’œ PURPLE DAY ๐Ÿ’œUnyanyapaa dhidi ya kifafa bado changamoto.Watu bado wanatengwa.Watu bado wanaogopa kitu ambacho wanaweza ...
26/03/2026

๐Ÿ’œ PURPLE DAY ๐Ÿ’œ
Unyanyapaa dhidi ya kifafa bado changamoto.
Watu bado wanatengwa.
Watu bado wanaogopa kitu ambacho wanaweza kuelewa.
Hii haikubaliki.
Kifafa sio uchawi.
Kifafa sio laana.
Ni hali ya kiafya na jamii inapaswa kubadilika, sio mgonjwa kujificha.
๐Ÿšซ Acha dharau
๐Ÿšซ Acha ubaguzi
๐Ÿšซ Acha kueneza uongo
โœ… Elimika
โœ… Simama na wapambanaji
โœ… Tetea haki zao
Ukimya, unachangia tatizo.
Chukua hatua leo.
๐Ÿ’œ

International Epilepsy Day 2026 ilikuwa zaidi ya maadhimisho  ilikuwa ni wito wa kitaifa wa kuchukua hatua.Tarehe 9 Febr...
16/02/2026

International Epilepsy Day 2026 ilikuwa zaidi ya maadhimisho ilikuwa ni wito wa kitaifa wa kuchukua hatua.
Tarehe 9 Februari 2026, katika Ukumbi wa Ummy Mwalimu, Muhimbili National Hospital Upanga, wadau wa afya, mashirika ya kiraia, na viongozi wa serikali walikusanyika kuimarisha mjadala wa kitaifa kuhusu afya ya mfumo wa neva na ujumuishi wa kijamii.
Chini ya kaulimbiu: โ€œEpilepsy Care in Tanzania: Time for Action to Reduce Stigmaโ€, msisitizo ulikuwa wazi unyanyapaa bado ni kikwazo kikubwa kinachowazuia watu wengi kupata uchunguzi wa mapema, matibabu sahihi, na huduma endelevu.
Maadhimisho haya yalizinduliwa rasmi na Naibu Waziri wa Afya, Florence Samizi, ambaye alisisitiza umuhimu wa kuimarisha utoaji wa huduma, kuwekeza kwenye elimu kwa umma, na kuondoa kabisa ubaguzi dhidi ya watu wanaoishi na kifafa.
Ni wakati wa kusonga mbele kwa mkakati ulioratibiwa, sera imara, na utekelezaji unaoonekana.
Kupunguza unyanyapaa si chaguo โ€” ni wajibu wa kitaifa.

๐Ÿ’œ


09/02/2026

Epilepsy Day,
Kifafa si laana wala uchawiโ€”ni hali ya kiafya inayohitaji uelewa, heshima, na msaada wa kweli.
Sikiliza kabla ya kuhukumu, kujifunza kabla ya kuamini uvumi, na kuchukua hatua badala ya kukaa kimya.

Ninasimama kuvunja unyanyapaa, kulinda haki, na kujenga jamii salama na jumuishi kwa watu wote wanaoishi na kifafa.
Elimu ni nguvu. Hatua ni sasa.

Epilepsy Day,  Kifafa si laana wala uchawi ni hali ya kiafya inayohitaji uelewa, heshima, na msaada wa kweli.Sikiliza ka...
09/02/2026

Epilepsy Day,
Kifafa si laana wala uchawi ni hali ya kiafya inayohitaji uelewa, heshima, na msaada wa kweli.
Sikiliza kabla ya kuhukumu, kujifunza kabla ya kuamini uvumi, na kuchukua hatua badala ya kukaa kimya.

Ninasimama kuvunja unyanyapaa, kulinda haki, na kujenga jamii salama na jumuishi kwa watu wote wanaoishi na kifafa.

Elimu ni nguvu. Hatua ni sasa.
๐Ÿ’œ
BreakTheStigma

SHINE Project ni mradi uliotekelezwa na Comunitร  Solidali nel Mondo (COM-SOL TZ) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na P...
19/08/2025

SHINE Project ni mradi uliotekelezwa na Comunitร  Solidali nel Mondo (COM-SOL TZ) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na PORALG, ukiungwa mkono na Italian Agency for Development Cooperation (AICS) kuanzia mwaka 2023 hadi sasa.

Mradi huu umejikita katika:
โœ… Kushughulikia changamoto za kifafa (epilepsy) na lishe duni (malnutrition), hasa kwa watu wenye ulemavu.
โœ… Kuimarisha huduma katika kliniki maalum nne zinazotoa huduma za kifafa na lishe.
โœ… Kutoa mafunzo kwa mfumo wa cascade katika mikoa 10 ya Tanzania kwa wahudumu wa afya na wadau wa jamii.
โœ… Kuandaa mapendekezo ya sera na vitendo kwa ajili ya huduma jumuishi za afya.

Mnamo 18 Julai 2025, TAEFI ilishiriki katika Final Conference ya SHINE Project jijini Dar es Salaam. Ushiriki huu ni hatua muhimu kwani unawakilisha sauti za watu wanaoishi na kifafa na changamoto za ulemavu katika mjadala wa kitaifa kuhusu huduma jumuishi za afya.

Kupitia ushirikiano na wadau mbalimbali, tunajivunia kuona mapendekezo ya mwisho ya mradi huu yakizinduliwa rasmi, yakilenga kuimarisha huduma za kifafa na lishe nchini.

๐Ÿ‘‰ TAEFI itaendelea kusimama pamoja na wapambanaji wa kifafa kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma.

๐Ÿ’œ


Happy International Youth Day! ๐ŸŒ๐Ÿ’œLeo tunasherehekea nguvu na mchango wa vijana duniani kote hasa wale wanaothubutu kuvun...
12/08/2025

Happy International Youth Day! ๐ŸŒ๐Ÿ’œ
Leo tunasherehekea nguvu na mchango wa vijana duniani kote hasa wale wanaothubutu kuvunja vikwazo na kufuata ndoto zao licha ya changamoto. Kupitia miradi yetu wa SPEAK UP, STANDING STRONG , tunaendelea kuwajengea uwezo wanafunzi wenye changamoto ya kifafa, tukiwapa maarifa, ujasiri, na nafasi za kujitambua.

Kila kijana ana sauti na thamani. Wakati vijana wenye changamoto wakipata msaada na fursa, dunia inapata viongozi wapya wenye maono na moyo wa kubadilisha jamii. ๐Ÿ’ชโœจ

Kwa vijana wote, Tunaweza!




Address

Kigamboni

Telephone

+255754839583

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAEFI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to TAEFI:

Share