04/08/2026
Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu; wala hakuuachilia ulimwengu wa kale, bali alimhifadhi Nuhu, Mjumbe wa haki na watu wengine saba, hapo alipoleta Gharika juu ya ulimwengu wa wasiomcha Mungu.
Mistari hii; Petro alifunuliwa jambo kubwa sana Jinsi Mungu anavyoutazama uasi na ukengeufu wa mtu, hana hasara kukuondoa na ufe katika dhambi yako haijalishi nafasi yako.
Wale malaika walioasi mbinguni, aliwatupa shimoni akawatia katika vifungo vya giza hadi siku ya kutupwa Jehanamu, unaoneje? Angewahurumia wabaki labda wangebadilika huko mbinguni, labda watubu! Akawatupilia mbali!
Unaoneje wale wa kipindi cha Nuhu, walivyoanza ukengeufu, uzinzi ulitamalaki, ikazariwa mijitu isiyomithilika ya hovyo, michafu hadi Mungu alihuzunika kwanini aliwaumba wanadamu, akapunguza hata miaka ya kuishi hadi miaka 120, lakini wapi hayakukoma ! Multiplication ya uzao muovu ilizidi sana, akaamua kuifuta dunia kwa gharika! Mijitu miovu, michafu, mizinzi, ilifutiliwa haikuoneka tena! Ni watu 8 tu wenye haki waliokolewa.
Unaoneje? kule Sodoma na Gomora, akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya iwe ishara kwa watu watakaokuwa hawamchi Mungu baada ya haya: akamwokoa Lutu yule mwwnye haki aliyehuzunishiwa na wale walawiti, wafilaji, wahalifu. Aliwauwa wote hakusaza mtu kule.
Unaoneje wewe, una thamani kuzidi wale katika kuumbwa kwako, Mungu hana hasara, anaweza kukuondoa na uchafu wako usipotubu na Kuiamini Injili na Kuokoka.
Unatuona k**a wajinga fulani hivi tunapokutahadharisha na ukengeufu wako, acha uzinzi huo, acha ulawiti, acha ushoga huo, usagaji, ufisadi,na uchafu wako uthiomithilika, kumbuka miaka yako ya kuishi hapa duniani is so limited, una miaka mingi ya kuishi baada ya kufa hapa duniani utateseka milele baada ya hukumu.
Ningekupa na mfano mwingine wa watu karibu 600,000 au zaidi waliofia jangwani, walipomuasi Mungu kwa sheria ya Musa, unaoneje? Aliwaokoa kwa Pharao, akawaua wote Jangwani kwa kukengeuka kwao, akawaacha wana wao tu kuingia Kaanani na wale wawili tu Joshua na Karebu.
Nakutahadhalisha; Okoka sasa, la! Mungu hana hasara.
2Pet.2:4-7.
JM Mwakalebela.