Anjita foundation

Anjita foundation Anjita foundation is non-profit Organization working for Early Childhood Development services.

  Taasisi ya Anjita foundation  ambayo ni mratibu wa wanachama wa Tanzania ECD Network  Mkoa wa Pwani, iliratibu mkutano...
28/03/2026


Taasisi ya Anjita foundation ambayo ni mratibu wa wanachama wa Tanzania ECD Network Mkoa wa Pwani, iliratibu mkutano wa 3 wa robo wa mtandao uliofanyika tarehe 26/03/2026.

Jumla ya wanachama 9 walishiriki mkutano huo, wakitoka katika Halmashauri za Kibaha Manispaa, Bagamoyo na Kisarawe.

Mkutano huo ulijadili na kufikia maazimio yafuatayo:
✔ Kuwa na muundo mmoja wa utoaji wa taarifa za utekelezaji wa miradi ya wanachama
✔ Kuandaa mafunzo ya kuimarisha mifumo ya taasisi
✔ Kuendeleza ushirikiano kati ya wanachama, jamii, wadau na serikali kwa ujumla

Tunaendelea kushirikiana kwa pamoja ili kuleta maendeleo endelevu katika jamii.

KARIBUNI WANANCHI NA WADAU WOTE TUKAENDELEE KUWEKEZA KWA WATOTO.
24/03/2026

KARIBUNI WANANCHI NA WADAU WOTE TUKAENDELEE KUWEKEZA KWA WATOTO.

  Halmashauri ya wilaya ya Chalinze kwa kushirikiana na taasisi ya  imefanya mkutano na wananchi wa kitongoji cha Majeng...
08/03/2026



Halmashauri ya wilaya ya Chalinze kwa kushirikiana na taasisi ya imefanya mkutano na wananchi wa kitongoji cha Majengo kata Bwiringu siku ya tarehe 3 Machi, 2026 shule ya msingi Mdaula B. Mkutano huo ulilenga ushirikishwaji wa jamii katika utekelezaji wa mradi wa Malezi centre unaofadhiliwa na wenye lengo la kujenga kituo cha kijamii cha kulelea watoto wadogo mchana katika kitongoji cha Majengo.

Viongozi mbalimbali wa serikali walishiriki mkutano huo akiwemo Afisa Ustawi wa jamii wa wilaya, Mheshimiwa Diwani wa kata ya Bwiringu, Mwenyekiti na mtendaji wa kitongoji cha Majengo, wajumbe wa kamati ya maendeleo ya kitongoji cha Majengo, Mwalimj mkuu wa shule ya msingi Mdaula B, taasisi ya Anjita na wananchi wa kitongoji hiko.

Katika mkutano huo maadhimio mkjawapo yaliyofanyika ni uundwaji wa kamati itakayosimamia ujenzi wa kituo na kutoa eneo shule ya msingi Mdaula B kwaajili ya ujenzi huo wenye kuleta maslahi kwa watoto wetu.

Naye Mkurugenzi wa taasisi ya Anjita ameahidi kutoa ushirikiano wote kwa lengo la kukamilisha mradi huo kwa ushirikiano mkibwa na wananchi, wadau na serikali kwa ujumla.

Taasisi ya   imeungana na serikali, wadau na wananchi wote katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.  itaendelea kuta...
08/03/2026

Taasisi ya imeungana na serikali, wadau na wananchi wote katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani. itaendelea kutambua mchango mkubwa wa wanawake wote duniani katika kuleta maendeleo endelevu. Kupitia mradi wa Mwanamke na Ujuzi, kwa mwaka wa fedha 2026/2027 taasisi ya anjita itaendelea kuwezesha akina mama Vijana 150 katika fani mbalimbali za ujuzi kwa lengo la kuwawezesha akina mama vijana hao kujiajiri na kuajiriwa sehemu mbalimbali.

 inaungana na wadau wote katika kushiriki maadhimisho ya siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi, 2026. Katika mkoa wa P...
07/03/2026

inaungana na wadau wote katika kushiriki maadhimisho ya siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi, 2026. Katika mkoa wa Pwani maadhimisho hayo yatafanyika Ikwiriri -Rufiji, hivyo tunawaalika wadau na wananchi wote kushiriki maadhimisho hayo muhimu.


28/02/2026
Taasisi ya  kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa  Wilaya ya Mkuranga wamefanya kikao cha tathmini ya mapi...
14/02/2026

Taasisi ya kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mkuranga wamefanya kikao cha tathmini ya mapitio ya utekelezaji wa shughuli za Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT–MMMAM) tarehe 11.2.2026.
Kikao hicho kililenga kutathmini hatua zilizofikiwa katika kuimarisha huduma za Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto, hususani katika maeneo ya ulinzi na usalama wa mtoto, afya, lishe, malezi yenye mwitikio pamoja na fursa za ujifunzaji wa awali katika jamii.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Afisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Mkuranga, Bi. Happiness Kikowe, aliwasilisha matumizi ya ECD Score Card inayotumika kufuatilia na kupima utekelezaji wa shughuli za MMMAM.
Bi. Happiness alieleza namna ya ujazaji sahihi wa taarifa, ukusanyaji wa takwimu muhimu na taratibu za uwasilishaji wa taarifa kupitia mfumo wa score card, akisisitiza umuhimu wa takwimu sahihi katika kupanga na kuboresha huduma za watoto.
Katika uwasilishaji wa taarifa ya robo ( Oktoba hadi Disemba, 2025), mafanikio yaliyobainishwa ni pamoja na:
Kutoa elimu kwa vituo 56 vya DCC kuhusu kuelimisha wazazi/walezi wenye watoto wa miaka 5 kuwasajili darasa la awali, kuimarisha uelewa wa jamii juu ya masuala ya malezi na makuzi ya watoto ngazi ya kaya na jamii.
Aidha, Bi. Happiness aliwakumbusha na kuwasisitiza washiriki kuendelea kuelimisha jamii pamoja na Wakuu wa Vitengo/ idara kuona namna ya kuwezesha/ kusaidia shughuli zaa Malezi na Makuzi kupitia shughuli wanazozitekeleza kila siku, akisisitiza kuwa suala la malezi ni la mtambuka na linahitaji ushirikiano wa sekta zote.
Nae Afisa Maendeleo ya jamii, alisisitiza kuwa serikali inaendelea kushirikiana na wadau ili kuhakikisha watoto wanapata mazingira bora ya Malezi, Makuzi na Maendeleo yao ya awali.
Katika kikao hicho , Afisa Ustawi wa jamii aliwasilisha tena mradi wa Malezi center unaofadhiliwa na TECDEN wenye kulenga kujenga kituo 1 cha kijamii cha kulelea watoto wadogo mchana kinatarajiwa jengwa katika kata ya mkuranga wilayani humo.

Tarehe 13 Februari 2026, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kwa kushirikiana na taasisi ya  iliendesha mkutano wa robo mw...
14/02/2026

Tarehe 13 Februari 2026, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kwa kushirikiana na taasisi ya iliendesha mkutano wa robo mwaka wa mapitio ya utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT–MMMAM).

Mkutano huo uliwakutanisha wajumbe wa Kamati ya PJT–MMMAM ya wilaya, wawakilishi wa wadau mbalimbali pamoja na wazazi, kwa lengo la kutathmini utekelezaji wa shughuli, kujadili changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha huduma za Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM).

Akizungumza katika mkutano huo, Afisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Kisarawe, Bi. Mwandili Rangi, aliwasilisha mfumo wa ECD Score Card unaotumika kufuatilia na kupima utekelezaji wa shughuli za MMMAM katika ngazi ya wilaya. Aliwaelekeza washiriki kuhusu namna sahihi ya ujazaji wa taarifa, ukusanyaji wa takwimu na utaratibu wa uwasilishaji wa taarifa kila robo mwaka, akisisitiza umuhimu wa takwimu sahihi katika kufanya maamuzi na kupanga mipango yenye tija.

Katika uwasilishaji wa taarifa ya robo ya Oktoba hadi Desemba 2025, shughuli zilizotekelezwa ni pamoja na:
1. Utoaji wa elimu mahakamani kuhusu masuala ya malezi, ulinzi na haki za mtoto.
2. Utoaji wa elimu kwa wazazi, wajawazito na walezi wanaofika kliniki kuhusu umuhimu wa upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa.
3. Utoaji wa elimu ya ulinzi na usalama wa mtoto katika shule tano (5) za msingj.

Aidha, moja ya maazimio muhimu ya mkutano huo ni kuanza kujaza na kuwasilisha taarifa za Score Card kwa kila Mkuu wa Kitengo/Idara ili kuongeza uwajibikaji, ushirikiano wa kisekta na ufanisi katika utekelezaji wa programu.

Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe inaendelea kuonesha dhamira ya dhati katika kuimarisha huduma za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kupitia ushirikiano wa wadau na jamii kwa ujumla, kwa lengo la kuhakikisha kila mtoto anapata mwanzo bora wa maisha.


Anjita Organization Undergoes Training of Trainers ( ToTs)  Soft and VSLA Skills. is currently participating in a five-d...
11/02/2026

Anjita Organization Undergoes Training of Trainers ( ToTs) Soft and VSLA Skills.

is currently participating in a five-day capacity-building training started on 9th Februsry, 2026.The trsining is being facilitated by Swisscontact, focusing on Soft Skills development and Village Savings and Loan Association (VSLA) methodologies comprised 16 ToTs.

The primary objective of the training is to equip trainers with essential soft skills and practical knowledge on VSLA implementation, enabling them to effectively support and empower beneficiaries of the Young Mothers jnder EmpowerHer through Skills ( EHS) Project. By strengthening the capacity of trainers, the program seeks to ensure the delivery of high-quality, impactful training to young women and girls.

The EHSProject is a key initiative aimed at promoting economic empowerment among young women and girls in the Coast Region of Tanzania. Through improved access to financial literacy, savings groups, and inclusive financial services, the project supports participants in building sustainable livelihoods and enhancing their socio-economic well-being.

This training marks an important step in reinforcing Anjita Organization’s commitment to community development and women’s empowerment. The skills and knowledge gained are expected to significantly contribute to strengthening community-based savings groups and fostering long-term economic resilience among young women.



Tarehe 10 Februari 2026, Mkurugenzi wa Taasisi ya  , Bi. Janeth Christian Malela, alifanya mkutano wa kwanza na wataalam...
11/02/2026

Tarehe 10 Februari 2026, Mkurugenzi wa Taasisi ya , Bi. Janeth Christian Malela, alifanya mkutano wa kwanza na wataalamu wa ngazi ya serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze.

Mkutano huo uliwakutanisha wataalamu kutoka Kitengo cha Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Jamii pamoja na Ofisi ya Mhandisi wa Halmashauri. Lengo kuu la mkutano lilikuwa ni kuwasilisha mpango kazi na bajeti ya utekelezaji wa Mradi wa Malezi Center, unaofadhiliwa na Taasisi ya Tanzania ECD Network.

Mradi wa Malezi Center unalenga kujenga vituo vya kijamii vya kulelea watoto wadogo mchana katika Halmashauri za Wilaya ya Chalinze na Mkuranga. Kupitia mradi huu, ANJITA inalenga kuimarisha huduma za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto katika jamii, ili kuhakikisha watoto wanapata msingi imara wa ukuaji wao.

Taasisi ya ANJITA inaendelea kushirikiana kwa karibu na serikali na wadau mbalimbali ili kuhakikisha utekelezaji wa mradi huu unakuwa na tija kwa watoto, familia na jamii kwa ujumla.




Mkuranga

On 21st January 2026,  held a successful courtesy meeting with the Community Development Officer of Dunda Ward, Bagamoyo...
22/01/2026

On 21st January 2026, held a successful courtesy meeting with the Community Development Officer of Dunda Ward, Bagamoyo District. The purpose of the meeting was to officially present Phase II of the EmpowerHER Through Skills Project.

This new phase will focus on providing vocational skills development in weaving, knitting, and handcrafts to 50 young mothers aged 15–30 years, with the aim of promoting economic empowerment and self-reliance to Young Mothers in Bagamoyo District.

During the meeting, the Managing Director of , Ms.Janeth Christian Malela, elaborated on the project’s goals, implementation strategies, and the importance of collaborative partnerships with government institutions, private sector actors, and business groups to sustainably support young mothers.

As part of the visit, 40 training registration forms were handed over to the Community Development Officer of Dunda Ward to support the beneficiary recruitment process.

We appreciate the warm reception and continued cooperation as we work together to empower young mothers through practical skills and opportunities. 💪🏽✨


Bagamoyo DundaWard AnjitaOrganization

Taasisi ya  imeshiriki katika hafla ya utoaji wa hundi za mfano za mikopo ya asilimia kumi (10%) kwa wanawake, vijana na...
21/01/2026

Taasisi ya imeshiriki katika hafla ya utoaji wa hundi za mfano za mikopo ya asilimia kumi (10%) kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mtongani, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mhe. Hamoud Abuu Jumaa, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa mikopo hiyo, akibainisha kuwa ni chachu muhimu ya kuinua uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya Halmashauri. Aidha, amewataka wataalamu wa halmashauri kusimamia kwa karibu matumizi ya mikopo hiyo ili ihakikishe inaleta tija iliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Bi. Shukuru Lusanjala, amesema jumla ya vikundi 54 vitanufaika katika awamu ya kwanza ya mikopo hiyo. Kati ya vikundi hivyo, 34 ni vya wanawake, 13 vya vijana na 7 vya watu wenye ulemavu, hali itakayosaidia kupunguza changamoto ya ajira na kuongeza kipato cha kaya.

Naye mwakilishi wa Taasisi ya , Ndg. Perce Christian, ambaye ni Afisa Mwezeshaji katika Mradi wa Mwanamke na Ujuzi unaofadhiliwa na shirika la Swisscontact, ameishukuru Serikali kwa jitihada kubwa inazochukua katika kuinua uchumi wa kaya kupitia mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Ndg. Perce amesema Taasisi ya kupitia Mradi wa Mwanamke na Ujuzi itaendelea kuwajengea uwezo na kuwapatia ujuzi wanawake na vijana ili waweze kujitegemea kiuchumi ili wamudu mahitaji ya familia na watoto. Ameongeza kuwa kwa mwaka 2026, mradi huo unatarajiwa kuwafikia jumla ya akina mama Vijana 150 katika Halmashauri za Bagamoyo, Chalinze, Wilaya ya Kibaha pamoja na Manispaa ya Kibaha.

Address

Kibaha Pwani
Kibaha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Anjita foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Anjita foundation:

Share