15/04/2020
Doforlife
Jiponye kupitia Mambo 10 na mepesi kabisa!!
01. Kumbuka chakula Cha asili kinaongeza Kinga ya Mwili Dhidi ya magonjwa mbalimbali
02. Kuepuka nyama nyekundu hasa unapokuwa mtu mzima (zaidi ya miaka 29) kwa kuwa nyama nyekundu inaongeza mafuta (cholesterols) Mwilini, Sambamba na chakula chenye kiwango kikubwa Cha sukari, ama kilichoondolewa virutubisho vyake vya asili Kisha kuongezewa utamu, K**a vile, soda, wali mweupe, chocolate, burns, keki n.k
03. Kula matunda pekee, kwa utaratibu mfano usile matunda ya ndizi na maziwa kwa pamoja, nzuri zaidi Ni bore utenge mlo ulio na matunda pekee bila chakula mfano unaweza ukala matunda yenye rangi nyeupe, jano, na nyekundu kwa pamoja bila chakula.
04. Zingatia kula mtama, uwele, na kunwya rozera ( maua ya Dodoma).
05. Epuka kuipendelea chakula kilichounguzwa kwa mafuta hasa ya yatokanayo na wanyama ili kupunguza uwezekano wa kuugua kansa
06. Epuka matumizi mabaya ya Dawa za hospital ama kutumia madawa ya kulevya na vichocheo mbalimbali kwa ajili ya kupunguza maumivu ama Msongo wa Mawazo. K**a una Maumivu/ unajihisi kuumwa muoane mtaalamu wa afya aliye na vipimo ili akusaidie, ama fika kituo Cha afya, na hospitalini.
K**a una Msongo wa Mawazo juu ya Mambo fulani ambayo hayajaenda sawa, tujilidhishe kupitia mawasiliano yetu ama fika kwa wataalamu wa ushauri na Saha walio karibu na wewe.
07. Fanya mazoezi ili kurejesha uhai wa afya yako ya Mwili na Akiri, pia unaboresja uwezo wa maamuzi yaliyo sahihi, na hormones zako kufanya Kazi vizuri.
08. Ulevi, uvutaji sigara na tabia zingine zinazoambatana na hayo huzoretesha afya, heshima na uwezo wa kufanya Kazi.
09. Kunywa maji kwa kiasi Cha uzito wako/masaa 24 + nusu Lita kwa siku itakufanya Mwili wako ujisikie shwari kabisa, au pengine inaweza inategemea na Hali ya hewa, na kwa wale walio na Kazi ngumu Sana wanaweza kunywa maji kila Mara na kadri iwezekanavyo
10. Hakuna Mazoea kwenye afya yako, Mwili upe kila kinachohitaji na Sio tamaa ya ajili yako.
Tamaa inauwa haijalishi Ni haraka ama polepole; "Linda afya yako jivunie kuwa halisi"