TUICO Tanzania

TUICO Tanzania Sisi ni TUICO. Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri. Miaka 30 ya Kutetea Haki, Utu, na Kazi za Staha!✊🏿

08/06/2026

Tunaendelea Kuimarisha matumizi ya mfumo wa TUICO-MIS na mfumo wa e-Utatuzi wa CMA ili kuboresha huduma kwa wafanyakazi.

📍 Mwanza

Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) kinaendelea kuimarisha matumizi ...
07/06/2026

Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) kinaendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma kwa wanachama.

Tarehe 6-7 Juni 2026 mkoani Mwanza, Makatibu wa Mikoa na Makatibu Wasaidizi wa Mikoa kutoka Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi walishiriki Semina ya Matumizi ya Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Chama (TUICO-MIS).

Mfumo huu ni sehemu ya mageuzi ya kidigitali yanayolenga kuboresha usimamizi wa taarifa za wanachama, shughuli za chama, mikataba ya pamoja ya kazi, na takwimu muhimu za kiutendaji.

Kadri shughuli za chama zinavyoendelea kukua, matumizi ya mifumo ya kidigitali yanakuwa muhimu zaidi katika kuongeza ufanisi, uwazi, na utoaji wa huduma bora kwa wanachama.

TUICO itaendelea kuwekeza katika teknolojia na kujenga uwezo wa watendaji wake ili kuhakikisha huduma kwa wanachama zinaendana na mahitaji ya ulimwengu wa kazi unaobadilika kwa kasi.

03/06/2026 Morogoro,Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) imeendesha  ...
05/06/2026

03/06/2026 Morogoro,
Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) imeendesha semina ya mafunzo kwa Viongozi wapya wa matawi ya Benki ya TCB .

Viongozi wapya wa Matawi ya TUICO katika Benki ya TCB tarehe 03/07/2026 walihitimisha Semina Elekezi inayolenga kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi kwa ufanisi.

Mafunzo hayo yalihitimishwa kwa kuwapatia vyetu viongozi wote walio udhuria mafunzo hayo kwa muda wa siku tatu.

Viongozi wapya wa Matawi ya TUICO katika Benki ya TCB leo wakiwa kwenye muendelezo Semina Elekezi inayolenga kuwajengea ...
02/06/2026

Viongozi wapya wa Matawi ya TUICO katika Benki ya TCB leo wakiwa kwenye muendelezo Semina Elekezi inayolenga kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi kwa ufanisi.

Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) na TANELEC Limited wamesaini Mka...
02/06/2026

Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) na TANELEC Limited wamesaini Mkataba wa Hali Bora za Kazi.

TANELEC ni kampuni inayozalisha transifoma, vifaa vya umeme na miundombinu ya usambazaji wa nishati, ikihudumia Tanzania na masoko mbalimbali barani Afrika.

Kusainiwa kwa mkataba huu kunathibitisha dhamira ya pande zoete mbili kuimarisha maslahi ya wafanyakazi, kukuza mazingira bora ya kazi, na kuendeleza mahusiano yenye tija na utulivu.

Kwa TUICO, majadiliano ya pamoja ni nyenzo muhimu ya kulinda na kutetea haki na maslahi ya Wanachama. Kwa kampuni, mahusiano mazuri kazini ni msingi wa kuongeza tija, ufanisi, na maendeleo endelevu ya biashara.

Mshikamano Daima.

01/06/2026

Viongozi wapya wa Matawi ya TUICO katika Benki ya TCB leo wameanza Semina Elekezi inayolenga kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi kwa ufanisi.

Viongozi wapya wa Matawi ya TUICO katika Benki ya TCB leo wameanza Semina Elekezi inayolenga kuwajengea uwezo wa kutekel...
01/06/2026

Viongozi wapya wa Matawi ya TUICO katika Benki ya TCB leo wameanza Semina Elekezi inayolenga kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao ya kiuongozi kwa ufanisi.

Mafunzo hayo kwa siku ya leo yalihusisha mada mbili muhimu: Nadharia ya Uongozi na Historia ya Vyama vya Wafanyakazi.

Kupitia mada ya Nadharia ya Uongozi, washiriki walijifunza kuhusu dhima ya Uongozi katika chama cha wafanyakazi, sifa za uongozi bora, umuhimu wa kujituma na kujitoa katika utumishi, kujitambua, kudhibiti hisia, kusikiliza na kuelewa wengine pamoja na namna ya kujenga mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wanachama.

Katika mada ya Historia ya Vyama vya Wafanyakazi, washiriki walipata uelewa kuhusu chimbuko la vyama vya wafanyakazi, misingi yake, maendeleo yake na mchango wake katika kulinda na kutetea haki na maslahi ya wafanyakazi.

Mafunzo haya yanatarajiwa kuwawezesha viongozi hao kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi na kuimarisha uwakilishi wa wanachama katika maeneo yao ya kazi.

22/05/2026 Dar es salaaam,Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) imeend...
22/05/2026

22/05/2026 Dar es salaaam,
Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) imeendesha semina ya mafunzo kwa wanafunzi wa Chuo cha TIA

Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uelewa wanafunzi kuhusiana na dhima nzima ya Chama cha Wafanyakazi na Umuhimu wa Mfanyakazi kujiunga na Chama ,
Hii nikuwaanda Wanafunzi na ulimwengu wa Ajira najinsi gani Chama cha Wafanyakazi K**a TUICO kitatumika kuimarisha ajira zao , haki zao na Usalama wao mahala pa kazi.

Pia walipata kufahamu Chimbuko na historia ya vyama vya Wafanyakazi K**a TUICO . Unaweza ukatembelea tovuti zetu kupata historia nzima ya TUICO. www.tuico.or.tz

MATUKIO KATIKA PICHA:DAY 2 JUKWAA LA USHIRIKA
21/05/2026

MATUKIO KATIKA PICHA:

DAY 2 JUKWAA LA USHIRIKA

21/05/2026

MWINULLA: TUICO wanafanya kazi nzuri. Elimu haina mwisho.

Address

Mtaa Wa TUICO
Ilala

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Telephone

+255222866960

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TUICO Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category