Shafii Islamic foundation

Shafii Islamic foundation Allah Akbar

Du’a Hii Inaweza Kukufanya Uwe Miongoni mwa Watu wa Peponi 🤍Kuna du’a moja…yenye nguvu sana…inayoweza kubadili mwisho wa...
16/04/2026

Du’a Hii Inaweza Kukufanya Uwe Miongoni mwa Watu wa Peponi 🤍

Kuna du’a moja…
yenye nguvu sana…
inayoweza kubadili mwisho wa maisha yako.

Siyo kwa sababu ya urefu wake…
bali ni kwa sababu ya unyenyekevu na ikhlasi yake.

🤲🏻 Du’a Yenyewe (Sayyidul Istighfar):

اللَّهُمَّ أَنْتَ رَبِّي، لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ، خَلَقْتَنِي وَأَنَا عَبْدُكَ، وَأَنَا عَلَى عَهْدِكَ وَوَعْدِكَ مَا اسْتَطَعْتُ، أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا صَنَعْتُ، أَبُوءُ لَكَ بِنِعْمَتِكَ عَلَىَّ وَأَبُوءُ لَكَ بِذَنْبِي، فَاغْفِرْ لِي، فَإِنَّهُ لاَ يَغْفِرُ الذُّنوُبَ إِلاَّ أَنْتَ

Allahumma anta Rabbi la ilaha illa anta, khalaqtani wa ana ‘abduka, wa ana ‘ala ‘ahdika wa wa‘dika mastata‘tu, a‘udhu bika min sharri ma sana‘tu, abu’u laka bini‘matika ‘alayya, wa abu’u bidhanbi faghfir li, fa innahu la yaghfiru adh-dhunuba illa anta.

Maana yake:

Ewe Allah, Wewe Ndiye Mola wangu,
hapana mola anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Wewe.

Umeniumba mimi, na mimi ni mja Wako,
nami niko juu ya agano Lako na ahadi Yako kwa kadiri ya uwezo wangu.

Najikinga Kwako kutokana na shari ya yale niliyoyafanya.
Nakiri neema Zako juu yangu, na nakuungama madhambi yangu.

Basi ninasamehe, kwani hakuna anayesamehe madhambi ila Wewe.

✨ Ahadi Yake:

Mtume ﷺ amesema:
“Mtu atakayeisoma (du’a hii) wakati wa mchana kwa kuwa na yakini nayo, kisha akafa siku hiyo kabla ya jioni, atakuwa miongoni mwa watu wa Peponi; na atakayeisoma usiku kwa kuwa na yakini nayo, kisha akafa kabla ya asubuhi, atakuwa miongoni mwa watu wa Peponi.”

(Sahih al-Bukhari 6306)

🕊️ Tafakari: Hebu fikiria… du’a moja pekee… inayoweza kukuhakikishia nafasi Peponi. Kinachohitajika tu… ni unyofu wa moyo (ikhlasi).

Wajue watu wa aina saba ambao wanaruhusiwa kutokufungwa mwezi mtukufu wa Ramadhan1- MGONJWAWanachuoni wanakubali kwamba ...
17/02/2026

Wajue watu wa aina saba ambao wanaruhusiwa kutokufungwa mwezi mtukufu wa Ramadhan

1- MGONJWA

Wanachuoni wanakubali kwamba inajuzu kwa mgonjwa kutofunga. Msingi wa hilo ni Aayah ambayo Mwenyezi Mungu Anasema

"Lakini ikiwa mmoja wenu ni mgonjwa au yuko safarini, basi ijumuishwe katika siku nyengine." [al-Baqarah 2:184]

2- MSAFIRI

Kuruhusiwa kutofunga haimaanishi kwamba k**a unaweza kufunga basi usifunge ila k**a unaona unaweza kufunga basi funga na ukiikosa funga utailipa baadaye kuisha kwa ramadhani.

3- WAZEE

Na ama wale wanaoweza kufunga kwa shida, (kwa mfano, mzee), wana hiari ya kufunga au) kulisha Miskin (kila siku)" (al-Baqarah 2:184).

Ibn Abbas (radhi za Allah ziwe juu yake) amesema kuwa Aya hii haijabatilisha kufunga, na inawahusu wazee na vikongwe wasioweza kufunga, hivyo basi kwakuwa hawatoweza funga basi kwa kila siku wamlishe masikini mmoja.

4- WALIOKUMBWA NA JANGA LA NJAA.

Wale ambao nchi zao zina patwa majanga ya njaa au mtu anashikwa na njaa kali kiasi kwamba anashindwa vumilia basi ulamaa wameona kwamba aache na ale chakula kwa kiasi chochote anachoweza.

5- WASIOFIKIA BALEGHE

Mtu huyu hajafikia umri wa kuanza kufanya ibada ila ni vizuri zaidi akajifunza ikiwa atataka.

6- MJAMZITO NA ANAYENYONYESHA

Ikiwa mjamzito anakhofia madhara makubwa kwa mtoto wake na ANAYENYONYESHA pia basi anaruhusiwa kuacha funga yake.

7- WENYE HEDHI NA NIFAASI

Nifaasi ni damu ya uzazi inayotoka baada ya kujifungua.
Hedhi ni damu ya mwezi kwa Mwanamke.

MALIPO YA FUNGA
Watu hawa wanaruhusiwa kuacha kufunga lakini pia wanahitaji kupata fadhila za mwezi mtukufu wa ramadhani sasa watapataje fadhila hizi? Kuna njia mbili ya kupata fadhila.

1- Kulipa funga walizokosa ikiwa alikuwa mgonjwa au Mjamzito nk... Basi atalazimika kulipa funga zake alizokosa.

2- Ikiwa hawezi lipa tokana na ugonjwa wake au hali yake basi atamlisha masikini mmoja kwa kila siku ya Funga.

*NASAHA MUHIMU*Haifai kwa Muislamu kusherehekea mwaka mpya wa Kikiristo (Miladi) kwa namna yoyote ile — iwe kwa maneno, ...
31/12/2025

*NASAHA MUHIMU*

Haifai kwa Muislamu kusherehekea mwaka mpya wa Kikiristo (Miladi) kwa namna yoyote ile — iwe kwa maneno, matendo, mapambo, fataki, au hata kuwatakia watu “Heri ya Mwaka Mpya.”

➡️ Hili ni *kujifananisha na makafiri*, jambo ambalo Mtume ﷺ alilikataza vikali: *"Atakayejifananisha na watu basi ni katika wao."* (Abu Dawud)

➡️ Aidha, ni *kuadhimisha sherehe zisizo za Kiislamu*, jambo ambalo linakatazwa kisheria, kwani Waislamu tuna idi zetu mbili tu: *Idi Al-Fitri* na *Idi Al-Adh-ha.*

➡️ Ni *kukufuru neema ya uongofu* kwa kuiga desturi za watu waliokengeuka na kutoamini.

➡️ Pia, kusherehekea mwaka mpya kunaambatana na *michezo, uchafu, ulevi, na mambo ya mchecheto* ambayo hayaendani na heshima ya Muislamu.

*USHAURI:*
➡️ Tumia muda huu kwa kufanya *muhasaba* (kujichunguza), kufanya toba, kuomba dua, na kuazimia kuwa Muislamu bora zaidi.
➡️ Kumbuka kuwa mwaka ukibadilika si sababu ya kusherehekea, bali ni *kukumbuka kuwa muda unakwenda na mauti yanakaribia*.

*ALLAH ATUPE UONGOFU NA ISTIQAMA.*
*Baarakallahu fikum.*

25/11/2025

JE MAHUSIANO YAKO YANAYUMBA YUMBA?

TAFUTA NJIWA MWEUPE KISHA MCHINJE NA UTOE MOYO WAKE BILA KUMNYONYOA HUYO NJIWA

TOA MOYO WAKE KISHA UHIFADHI KWENY KICHUPA.

TAFUTA MSAFALA WA SIAFU UKISHAUPATA SASA TOA MOYO WA NJIWA NAJINA LA MHUSIKA AMBALO UMEANDIKA KWENYE KARASI

MOYO WA NJIWA UWEKE KWENYE MSAFARA WA SIAFU KISHA NUIA VYOTE UTAKAVYO NUIA K**A DAKIKA TATU HIVI

BAADA YA HAPO UTOE MOYO WA NJIWA NA WALE SIAFU WALIOPO KWENY MOYO FUNGA KWENY KARATAS ULILOANDIK JINA LA MHUSIKA WAKO KISHA WEKA KWENY KICHUPA HAKIKISHA SIAFU HATOKI HATA MMOJA

RUDI NYUMBAN KISHA VUA NGUO ZOTE CHUMBANI KWAKO JIZUNGUSHIE MARA 7 KILE KICHUPA CHA MOYO PAMOJA NA WALE SIAFU.

TAFUTA SEHEM YENY MTI WA KIVULI NENDA USIKU KAKIZIKE KILE KICHUPA.

UTAKUJA KUNISHUKURU UKIFUATA HAYO MAELEZO

KWA MSAADA ZAIDI PAMOJA NA USHAURI MBALIMBALI NJOO INBOX

18/10/2025

Kila mtu anaye rafiki mmoja ambaye ndo kila kitu kwake, Mtume(saw)alipohamia Madina alihama pmj na Rafiki yake mkubwa, je ni nani?

14/10/2025
30/09/2025

(51) Sema: Halitusibu ila alilo tuandikia Allah
Yeye ndiye Mola wetu Mlinzi
Na Waumini wamtegemee Allah tu!
(Surat AtTaubah)

Address

Tabora
Igombe

Telephone

+255653426020

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shafii Islamic foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share