24/02/2026
Hatimaye hali ya sintofahamu iliyokuwepo kwa zaidi ya miezi mitatu katika Mtaa wa Afya Kata ya Ludete Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro mkoani Geita imefikia tamati, baada ya familia ya aliyekuwa balozi wa nyumba kumi Shina namba 18, Costantini Juakali, kusamehewa na kurejeshwa rasmi katika jamii iliyokuwa imemtenga.
Hatua hiyo imetokana na juhudi za Mkuu wa Wilaya ya Geita, Hashim Komba, aliyechukua hatua ya kufika moja kwa moja mtaani hapo akiambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, kusikiliza hoja za pande zote na kusimamia upatikanaji wa suluhu.