18/04/2026
MAANDALIZI YA ZIARA YA KITAIFA YA UFUATILIAJI UTEKELEZAJI WA PROGRAMU JUMUISHI YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO (PJT-MMAMM).
Leo, tarehe 18 Aprili 2026, kimefanyika kikao muhimu cha maandalizi ya ziara shirikishi inayolenga kufanya ufuatiliaji na kuona hatua za utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMAMM) ngazi na Mkoa na Halmashauri.
Kikao hicho kimeandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kwa kushirikiana na TECDEN, kikiwa ni sehemu ya maandalizi ya ziara itakayofanyika katika mikoa 11 ya ambayo ni: Mkoa wa Dar es Salaam, Lindi, Mwanza, Singida, Simiyu, Morogoro, Rukwa, Katavi, Tanga, na Njombe.
Kikao hiki kimejumuisha wadau kutoka wizara za kisekta na taasisi mbalimbali, ikiwemo: Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wadau wa Maendeleo: TECDEN, Children in Crossfire, na Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).
Lengo kuu la ziara hii inayokuja ni kuendelea kuchagiza na kuimarisha masuala yanayohusu watoto wenye umri wa kuanzia miaka 0 hadi 8. Kupitia ziara hii, serikali na wadau wanakusudia kuhakikisha kuwa ajenda ya malezi na makuzi inapewa kipaumbele cha juu katika mipango ya maendeleo na utengaji wa bajeti, ili kujenga msingi imara kwa mustakabali wa watoto wa Kitanzania.
TECDEN pamoja na wadau mbalimbali tunaendelea kushirikiana na serikali ili kuhakikisha kuwa masuala yote yanahusu malezi makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto yanapewa kipaumbele katika bajeti na mipango mbalimbali ya serikali. Hatua hii inachangia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050. "Watoto wote wa kika na kiume wapo kwenye mwelekeo sahihi wa kufikia ukuaji timilifu angalau kwa asilimia 90"