Inades Formation Tanzania

Inades Formation Tanzania Inades-Formation Tanzania, Serving the Common Good

Katika kusherekea siku ya Mazingira Duniani Leo tar 5Juni 2026, Shirika la INADES-Formation Tanzania limeungana na wanaf...
05/06/2026

Katika kusherekea siku ya Mazingira Duniani Leo tar 5Juni 2026, Shirika la INADES-Formation Tanzania limeungana na wanafunzi, walikua na wanakijiji wa Kisima Cha Ndege na.kupanda miti takribani 200 katika shule ya Sekondari ya Kisima Cha Ndege.

Afisa Kilimo wa Shirika la INADES-Formation Tanzania ambaye alimuwakirisha Mkurugenzi wa shirika hilo Bi. Jacqueline Nicodemus amesema Shirika linaunga mkono Dira ya Serikali ya 2050 ya kuwajibika kuikijanisha Tanzania.



Shirika la INADES-Formation Tanzania limemkabidhi tuzo na zawadi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Agnes Meena, ...
05/06/2026

Shirika la INADES-Formation Tanzania limemkabidhi tuzo na zawadi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Agnes Meena, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa wa Serikali katika kuboresha ustawi wa mnyama kazi punda pamoja na kufanikisha Maadhimisho ya Siku ya Punda Duniani yaliyofanyika kitaifa katika eneo la Mgusu, mkoani Geita.

Akikabidhi tuzo hiyo, Jacqueline Nicodemus, Mkurugenzi wa INADES-Formation Tanzania, ameipongeza Serikali kwa ushiriki wake katika maadhimisho hayo na kuishukuru kwa juhudi zinazoendelea za kuhakikisha wananchi wanapata elimu kuhusu umuhimu wa kumlinda, kumtunza na kumstawisha punda.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo pia amekutana na kufanya mazungumzo na Msajili wa Baraza la Vetinari Tanzania, Ndugu. Amani Kilemile, kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili katika kuboresha mfumo wa utoaji huduma za afya za mifugo nchini.

Mazungumzo hayo yalijikita katika kuendeleza juhudi za pamoja za kuhakikisha wafugaji wanapata huduma bora za kitaalamu na zinazochangia ustawi wa mifugo pamoja na maendeleo ya sekta ya mifugo kwa ujumla.



Shirika la INADES-Formation Tanzania linawatakia heri Siku ya Mazingira Duniani. "Pamoja tunatimiza Dira ya Taifa yakuik...
05/06/2026

Shirika la INADES-Formation Tanzania linawatakia heri Siku ya Mazingira Duniani. "Pamoja tunatimiza Dira ya Taifa yakuikijanisha Tanzania ifikapo 2050."



‎Shirika la INADES-Formation Tanzania leo lilipata fursa ya kumueleza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano ...
04/06/2026

‎Shirika la INADES-Formation Tanzania leo lilipata fursa ya kumueleza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Hamad Masauni, kuhusu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na shirika hilo alipofanya ziara katika banda la Shirika hilo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika Viwanja vya Jakaya Kikwete, Dodoma.

‎Afisa wa Mafunzo kwa Masafa wa shirika hilo, Daisy Mola, alimueleza Waziri kuhusu kazi za shirika katika utunzaji wa mazingira, kilimo endelevu na matumizi ya mbegu za asili zinazovumilia ukame na magonjwa na mradi wa kuboresha ustawi wa mnyama kazi punda, miradi ikiwa inatekelezwa mikoa ya Dodoma, Iringa na Singida kwa ufadhili wa mashirika ya Bread for the World na Brooke East Africa.

‎Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Waziri Masauni alilipongeza shirika kwa mchango wake katika kulinda na kuhifadhi mazingira, akisema juhudi hizo zinaunga mkono Dira ya Taifa ya kuikijanisha Tanzania ifikapo mwaka 2050.

‎Pia alitambua mchango wa kampeni ya upandaji miti ya “Panda Mti, Tuilinde Kesho” iliyoanzishwa Januari 2026 na Shirika hilo, ambayo inalenga kupanda miti 500,000 ifikapo mwaka 2027, tayari ikiwa imepanda miti 19,758 katika wilaya za Bahi, Chemba na Kondoa



Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Dr. Jafar Rajab Seifu akitia sahihi kitabu cha wageni alipotembelea banda la ...
03/06/2026

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Dr. Jafar Rajab Seifu akitia sahihi kitabu cha wageni alipotembelea banda la Shirika la INADES-Formation Tanzania katika maonesho ya siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

Naibu Waziri huyo alipongeza shirika hilo kwa utekelezaji wa shughuli zake mbalimbali katika Mikoa ya Iringa, Dodoma na Singida hasa zile zinazolenga utunzaji wa mazingira k**a vile upandaji wa miti, kilimo endelevu na kilimo kwa kutumia mbegu za asili zinazovumilia ukame na kutunza mazingira.

Alisema shughuli hizo zinaenda sambamba na dira ya taifa ya 2050 ya kukijanisha Tanzania.



Baadhi ya wadau mbalimbali wakitembelea banda la INADES-Formation Tanzania wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Du...
03/06/2026

Baadhi ya wadau mbalimbali wakitembelea banda la INADES-Formation Tanzania wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoendelea katika viwanja vya Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.

Kupitia banda hilo, wadau walipata fursa ya kujifunza mbinu mbalimbali za kilimo endelevu zinazozingatia uhifadhi na utunzaji wa mazingira kupitia vitabu vya matunzo kwa njia ya Masafa.

Pia walijifunza upandaji na utunzaji wa miti, matumizi ya mbegu za asili zinazostahimili ukame, pamoja na teknolojia rafiki kwa mazingira zinazochangia kuongeza uzalishaji wa kilimo huku zikihifadhi rasilimali za asili kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.



Katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, INADES-Formation Tanzania inaendelea kuonesha dhamira yake ya kuhifadhi ma...
02/06/2026

Katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, INADES-Formation Tanzania inaendelea kuonesha dhamira yake ya kuhifadhi mazingira kupitia kampeni za upandaji miti na uhamasishaji wa jamii kuhusu utunzaji wa rasilimali asilia.

Kupitia shughuli hizi, shirika linachangia juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, kurejesha uoto wa asili, na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika kujenga Tanzania ya kijani na endelevu. Ushiriki huu unaendana na maono ya taifa ya kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.




INADES-Formation Tanzania inaunga mkono na kutekeleza dira ya Serikali ya Tanzania ya kuijenga nchi yenye mazingira ende...
01/06/2026

INADES-Formation Tanzania inaunga mkono na kutekeleza dira ya Serikali ya Tanzania ya kuijenga nchi yenye mazingira endelevu na yenye ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi ifikapo mwaka 2050 kwa kuhamasisha upandaji miti, uhifadhi wa mazingira, kilimo mseto, na matumizi endelevu ya rasilimali

Kupitia miradi yake ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kampeni za kijamii za upandaji miti, shirika linaendelea kushirikisha jamii, taasisi na viongozi wa maeneo mbalimbali katika juhudi za kuifanya Tanzania kuwa ya kijani, salama na yenye mazingira bora kwa kizazi cha sasa na kijacho.



Friday, the 29th May, 2026, will go down in history as INADES-Formation Togo officially launched the INADES Academy Togo...
31/05/2026

Friday, the 29th May, 2026, will go down in history as INADES-Formation Togo officially launched the INADES Academy Togo – Kouloumi, a space dedicated to training, agricultural innovation, hands-on learning, and opportunities for young people and rural communities. 🌾🐐💧

Spanning agriculture, livestock farming, rural entrepreneurship, and sustainable development, this center aims to be a true hub of transformation and hope.

INADES Academy: Cultivating the skills of tomorrow!



outh

‎This day reminds us as an organisation that fights climate change and improving the livelihoods of communities that eve...
31/05/2026

‎This day reminds us as an organisation that fights climate change and improving the livelihoods of communities that every action, whether planting trees, conserving water, managing waste responsibly, or protecting biodiversity contributes to a healthier and more sustainable planet.

‎Let us work together to promote environmental stewardship, combat climate change, and build a greener Tanzania.



Address

Dodoma

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Inades Formation Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Inades Formation Tanzania:

Share