11/05/2026
Kikao cha mashauriano na kuweka mkakati wa urasimishaji wa tansia ya ukalimani wa lugha ya alama Tanzania huku naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu wa Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Ummy H. Nderiananga Akisisitiza umuhimu wa kuharakisha mwongozo huo wa urasimishaji wa tasnia ya Ukalimani wa Lugha Ya Alama Tanzania
Kikao kilichoandaliwa na Chama Cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) na kuhudhuriwa na viongozi wa shirikisho la Vyama Vya Watu wenye ulemavu (SHIVYAWATA) , Wabunge, Wawakilishi kutoka Wizara ya Habari na Mawasiliano, Ofisi ya Waziri Mkuu, Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA), pamoja na waandishi wa habari.
Aidha Mh. Ummy Ndereananga amesema kua serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali kuandaa miongozo na kanuni zitakazo saidia kusimamia taaluma hiyo, huku akihimiza jamii kuongeza uelewa wa matumizi ya Lugha Ya Alama ili kuondoa vikwazo vya mawasiliano
Washiriki wa kikao hicho wakiwemo Wabunge wameitaka serikali kuipa kipaumbele tasnia hiyo, wakisisitiza umuhimu wa wa ajira kwa wakalimani wa Lugha ya alama katika sekta zote, pamoja na kuimarisha mafunzo ya utambuzi wa taaluma hiyo ili kuiboresha