Fawopa-Tanzania

Fawopa-Tanzania 🌍For Benefit to all together
đź“–Founded on 18th April 2004 in Tanzania

An NGO based in Mtwara - Tanzania : Building Poverty free and Sustainable Local communities with justice and Equality for, Women, Youths and Children.

Leo ni siku ya NGO duniani, Shirika la FAWOPA tunafurahia siku hii kwakuwa kupitiakazi zetu kwa kipindi cha miaka 20 tum...
27/02/2026

Leo ni siku ya NGO duniani, Shirika la FAWOPA tunafurahia siku hii kwakuwa kupitia
kazi zetu kwa kipindi cha miaka 20 tumefanikiwa kuchangia utekelezaji wa Dira ya taifa 2025, hasa hasa katika kuboresha Maisha ya watu, Tumekuwa na juhudi kubwa katika kuchechemua na kushawishi utungaji wa sera bora, Kutoa elimu ya maswala mbalimbali ya kijamii na maendeleo, Kuunganisha wananchi na fursa mbalimbali zilizopo, na zaidi tunafurahi kuwa sehemu ya msaada kwa Wanawake, Watoto na Vijana wengi nchini Tanzania.

Tunajivunia mafanikio makubwa katika maeneo ya Elimu na Uwezeshaji wa Kiuchumi kati ya maeneo yetu manne ya kipaumbele;
1- Elimu: Kwa kipindi hicho tumeweza kuwasaidia watoto na Vijana elfu 1706 kupata, msaada wa vifaa vya Shule (Stationeries), Mentorship, Lishe na ufadhili wa masomo katika ngazi mbalimbali za kielimu (Fawopa tunatoa kipaumbele kikubwa katika elimu na tunaamini kuwa, Mabadiliko ya kuondokana na umasikini, maradhi na ujinga yanaanzia kwenye Elimu)
2- Uwezeshaji wa Kiuchumi: Tumeweza kuwafikia na kuwawezesha Vijana na Wanawake, 12794 kupitia elimu ya ujasiriamali, mitaji, sambamba na kuwawezesha kuzitambua na kuzitumia fursa mbalimbali katika maeneo yao.

Siku, hii inatupa nafasi ya kujitafakari, na kutafakari mchango wetu katika kujenga, Taifa lenye maendeleo jumuishi ambalo rasilimali zilizopo zinatumika kikamilifu kwa manufaa ya watu wote, na vizazi vijavyo.

Tunaendelea kuwashukuru na kuwakaribisha wadau wetu wa maendeleo ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha kazi zetu, Mafanikio haya ni yakwetu sote, Tunatarajia ushirikiano zaidi.

Siku hii inamaana gani kwako?


Fawopa-Tanzania  inaungana na Ujumbe wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania kutoa pongezi za dhati Kwa Wakili Onesmo Olenguru...
29/01/2026

Fawopa-Tanzania inaungana na Ujumbe wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania kutoa pongezi za dhati Kwa Wakili Onesmo Olengurumwa kwa kutajwa kuwa miongoni mwa wagombea bora duniani katika nafasi ya Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya watetezi wa haki za binadamu duniani.

K**a wadau wa Haki za Binadamu, Nchini Tanzania Tunathamini Mchango wa Onesmo katika kuendeleza na kulinda haki za binadamu na watetezi wake nchini Tanzania na kwingineko, Tunamtakia kila la Kheri

Tanzania Human Rights Defenders Coalition

Ujumbe wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania unatoa pongezi za dhati Kwa Wakili Onesmo Olengurumwa kwa kutajwa kuwa miongoni mwa wagombea bora duniani katika nafasi ya Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya watetezi wa haki za binadamu duniani.

Ni utambuzi muhimu wa dhamira yake ya muda mrefu katika kuendeleza na kulinda haki za binadamu na watetezi wake nchini Tanzania na kwingineko.

———

The EU Delegation to Tanzania warmly congratulates Adv. Onesmo Olengurumwa on being ranked among the top global candidates for the mandate of UN Special Rapporteur on the situation of human rights defenders.

A powerful recognition of his long-standing commitment to advancing and protecting human rights and their defenders in Tanzania and beyond.

Hello, EveryoneWe are now on  LinkedIn Please follow us, www.linkedin.com/company/fawopatzAhsante.
06/01/2026

Hello, Everyone
We are now on LinkedIn
Please follow us, www.linkedin.com/company/fawopatz
Ahsante.

FAWOPA TZ | We believe in 'Shared Prosperity' where Development is Community-led, Sustainable & Inclusive that's Faidika Wote Pamoja | FAWOPA - Faidika Wote Pamoja is a local, women and youth-led non-governmental organization established in 2004 in Mtwara Region, Southern Tanzania. F...

25/11/2025

Moreover, Kungwis play a crucial role in raising GBV awareness among adolescent girls and the wider community. Their mentorship is vital particularly during this end of year period (Including the ) which is transitional period as girls graduate from primary and secondary school. Without this intervention, many girls face the risk of early pregnancy and marriage, cycles often characterized by high rates of domestic violence.
We deeply appreciate the support of AKF and Canada’s International Development – Global Affairs Canada in empowering our Kungwis and transforming our community.

The impact is visible: we are seeing reduced dropouts, fewer early pregnancies, and lower mortality rates in our implementation areas. We couldn't ask for better partners in this mission.

Siku ya Kimataifa ya Mtoto Duniani 2025: Sauti Yangu, Haki Zangu!Leo, Novemba 20, Fawopa-Tanzania tunaungana na ulimweng...
20/11/2025

Siku ya Kimataifa ya Mtoto Duniani 2025: Sauti Yangu, Haki Zangu!

Leo, Novemba 20, Fawopa-Tanzania tunaungana na ulimwengu kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto Duniani kwa kaulimbiu: "My day, my rights" (Siku Yangu, Haki Zangu).

Kwa Pamoja tunawahimiza wazazi na walezi wote:
1- Kuendelea kutoa Fursa ya Kuwasikiliza watoto: Watoto wana mtazamo na sauti yenye thamani, hivyo ni Muhimu Kuwa Sikiliza na Kuwapa nafasi ya kujieleza bila woga ili kuweza kuwapatia msaada stahiki!

2- Pia tunawahimiza wazazi kuendelea Kutilia mkazo swala la elimu, kwa kuhakikisha tunatenga muda kufuatilia maendeleo ya watoto, kupata muda wa kuwatembelea mashuleni, na Kuzungumza nao kuhusu namna elimu itakavyoweza kubadilisha maisha yao hapo baadae Mtoto aliyeelimika ni mbegu ya kujenga ustawi kwa taifa.

Kwa pamoja, Tuendelee kushirikiana kulinda na kutetea haki za kila mtoto.



CC: Photo: From Aga Khan Foundation AGECS Project documentation, Photo Captured by Rich Townsend, Children playing on the Beach Sand, in Msangamkuu ward- Mtwara

We are happy that, Fawopa has been one of the organization participating in, 3rd event of Lightup Impact days event, Org...
23/10/2025

We are happy that, Fawopa has been one of the organization participating in, 3rd event of Lightup Impact days event, Organized in Nairobi Kenya, 22-23-October 2025, Our two Staff (Magreth Mrope and Justin Kabelege, has been supported by Aga Khan Foundation, to attend this event, which has been so instrumental in shifting power of our young staff, in shaping the future of our work in Advancing Gender Equality, and Climate Justice.

Jana tarehe 1, na Leo Tarehe 2, Octoba Ulikuwa ni Wakati Mzuri, Kutembelewa na Waandishi wa Habari Kutoka Shirika la Uta...
02/10/2025

Jana tarehe 1, na Leo Tarehe 2, Octoba Ulikuwa ni Wakati Mzuri, Kutembelewa na Waandishi wa Habari Kutoka Shirika la Utangazaji la Taifa - TBC Taifa, ambao walitutembelea kusikia namna tunavyotekeleza majukumu yetu, K**a asasi ya Kiraia moja wapo iliyopewa kibali na Tume Huruya TaifayaUchaguzi kutoa elimu ya mpiga kura (Voters Education) na kutizima uchaguzi k**a waangalizi huru (Independent election observers) zikiwa zimebaki siku 26 tu ili tufike siku ya tarehe 29, mwezi Octoba, ambayo itakuwa ni siku ya kupiga kura.

Tutaendelea kushiriki nawe sehemu ya mazungumzo yetu, kupitia kwa Mkurugenzi wetu katika post zinazofuata, usikae mbali.

Tume Huruya TaifayaUchaguzi

Jukwaa la Mwaka la NGOs ni sehemu mahsusi inayotukutanisha wadau wa sekta ya NGO Nchi Nzima Kujadili mafanikio changamot...
10/08/2025

Jukwaa la Mwaka la NGOs ni sehemu mahsusi inayotukutanisha wadau wa sekta ya NGO Nchi Nzima Kujadili mafanikio changamoto, Kuweka Mikakati na Mapendekezo ya Maboresho ya Kazi zetu Kwa Viongozi Mbalimbali wa Kisekta na Serikali!
Mwaka Huu 2025, Jukwaa la NGOs linatuwezesha Kufanya Tathmini ya Mchango wa Sekta ya NGO kwa Kipindi cha Miaka mitano 2020-2025 wakati tukijiandaa kuelekea Uchaguzi Mkuu
Fawopa-Tanzania Tumewakilishwa na Mkurugenzi wetu Ndugu Baltazar Komba Katika Jukwaa hili!
Karibu Tuungane Pamoja, Kuanzia Tarehe 11 had 13 Agosti!

Address

Dar Es Salaam
63114

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fawopa-Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share