27/02/2026
Leo ni siku ya NGO duniani, Shirika la FAWOPA tunafurahia siku hii kwakuwa kupitia
kazi zetu kwa kipindi cha miaka 20 tumefanikiwa kuchangia utekelezaji wa Dira ya taifa 2025, hasa hasa katika kuboresha Maisha ya watu, Tumekuwa na juhudi kubwa katika kuchechemua na kushawishi utungaji wa sera bora, Kutoa elimu ya maswala mbalimbali ya kijamii na maendeleo, Kuunganisha wananchi na fursa mbalimbali zilizopo, na zaidi tunafurahi kuwa sehemu ya msaada kwa Wanawake, Watoto na Vijana wengi nchini Tanzania.
Tunajivunia mafanikio makubwa katika maeneo ya Elimu na Uwezeshaji wa Kiuchumi kati ya maeneo yetu manne ya kipaumbele;
1- Elimu: Kwa kipindi hicho tumeweza kuwasaidia watoto na Vijana elfu 1706 kupata, msaada wa vifaa vya Shule (Stationeries), Mentorship, Lishe na ufadhili wa masomo katika ngazi mbalimbali za kielimu (Fawopa tunatoa kipaumbele kikubwa katika elimu na tunaamini kuwa, Mabadiliko ya kuondokana na umasikini, maradhi na ujinga yanaanzia kwenye Elimu)
2- Uwezeshaji wa Kiuchumi: Tumeweza kuwafikia na kuwawezesha Vijana na Wanawake, 12794 kupitia elimu ya ujasiriamali, mitaji, sambamba na kuwawezesha kuzitambua na kuzitumia fursa mbalimbali katika maeneo yao.
Siku, hii inatupa nafasi ya kujitafakari, na kutafakari mchango wetu katika kujenga, Taifa lenye maendeleo jumuishi ambalo rasilimali zilizopo zinatumika kikamilifu kwa manufaa ya watu wote, na vizazi vijavyo.
Tunaendelea kuwashukuru na kuwakaribisha wadau wetu wa maendeleo ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha kazi zetu, Mafanikio haya ni yakwetu sote, Tunatarajia ushirikiano zaidi.
Siku hii inamaana gani kwako?