ActionAid Tanzania

ActionAid Tanzania ActionAid Tanzania is a member of ActionAid International, an agency striving to end poverty and injustices from Tanzania and beyond

Kwa siku mbili mfululizo, tumepata fursa ya kuambatana na ugeni kutoka Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania Embassy of Ire...
13/08/2026

Kwa siku mbili mfululizo, tumepata fursa ya kuambatana na ugeni kutoka Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania Embassy of Ireland in Tanzania katika ziara ya kukagua maendeleo ya Mradi wa Climate Smart Agriculture Project II (CSAP II), unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya ActionAid Tanzania na WFP WFP Africa , kwa ufadhili wa Ubalozi wa Ireland.

Katika ziara hii, tumetembelea Wilaya za Chamwino (Nhinhi) na Kongwa mkoani Dodoma, ambapo tumejifunza na kushuhudia kwa vitendo namna mradi unavyowezesha wakulima kupitia kilimo himilivu cha zao la mtama.

Miongoni mwa mambo tuliyoyaona ni matumizi ya umwagiliaji kwa njia ya matone (drip irrigation), juhudi za kuboresha upatikanaji wa lishe na uhifadhi wa chakula, uimarishaji wa vikundi vya wanawake vya kusaidiana, upatikanaji wa masoko ya mazao, pamoja na matumizi ya mashine katika kupura mtama baada ya kuvuna.

Mbinu na teknolojia hizi zinaendelea kuwasaidia wakulima kuongeza uzalishaji, kupunguza changamoto za baada ya mavuno, kuboresha lishe na kuongeza fursa za kipato, huku wakijenga ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi.



Katika mazingira ya mabadiliko ya tabianchi, kulinda mbegu za asili si suala la kilimo pekee bali ni suala la usalama wa...
10/08/2026

Katika mazingira ya mabadiliko ya tabianchi, kulinda mbegu za asili si suala la kilimo pekee bali ni suala la usalama wa chakula, uanuai wa kibayolojia, maarifa ya asili na nguvu ya wakulima.

Mbegu za asili zinaweza kusaidia jamii:
✅ Kuimarisha usalama wa chakula wakati wa misimu migumu
✅ Kupunguza utegemezi wa mbegu za biashara zenye gharama kubwa
✅ Kulinda uanuai wa mazao na mazingira
✅ Kuimarisha nafasi ya wanawake k**a walinzi wa mbegu
✅ Kuhifadhi maarifa ya kilimo yaliyorithishwa kwa vizazi

Lakini ili mifumo hii iwe imara, tunahitaji kuwekeza katika mifumo ya mbegu inayosimamiwa na wakulima, benki za mbegu za jamii, kilimo ikolojia, na upatikanaji wa mbegu kwa wanawake na wakulima vijana.

👉 Swipe kujifunza kwa nini kulinda mbegu za asili ni hatua muhimu katika kujenga mifumo ya chakula inayostahimili mabadiliko ya tabianchi.

💬 Je, katika jamii yako kuna mbegu za asili ambazo zimehifadhiwa na kutumika kwa vizazi? Tuambie kwenye comments.

_______________________________

In the face of climate change, protecting indigenous seeds is not just an agricultural issue; it is about food security, biodiversity, indigenous knowledge, and the power of farmers.

Indigenous seeds can help communities:

✅ Strengthen food security during difficult seasons
✅ Reduce dependence on costly commercial seeds
✅ Protect crop diversity and the environment
✅ Strengthen the role of women as seed custodians
✅ Preserve farming knowledge passed down through generations

But for these systems to remain strong, we need to invest in farmer-managed seed systems, community seed banks, agroecology, and access to seeds for women and young farmers.

👉 Swipe to learn why protecting indigenous seeds is an important step towards building food systems that are resilient to climate change.

💬 Does your community have indigenous seeds that have been preserved and used for generations? Tell us in the comments.



Leo tunawasherehekea siku ya wakulima; walinzi wa chakula chetu na watunzaji wa mbegu zetu. Kupitia  , tunaendelea kutet...
08/08/2026

Leo tunawasherehekea siku ya wakulima; walinzi wa chakula chetu na watunzaji wa mbegu zetu. Kupitia , tunaendelea kutetea ulinzi wa mbegu za asili na haki za wakulima.

====================

Today, we celebrate farmers; the guardians of our food and custodians of our seeds. Through , we continue to advocate for the protection of indigenous seeds and farmers’ rights.



  ActionAid International ——For years, farmers watched their traditional seeds disappear. Janeth decided they were worth...
08/08/2026

ActionAid International
——
For years, farmers watched their traditional seeds disappear.

Janeth decided they were worth fighting for.

Now, she helps preserve indigenous seeds, strengthen local food systems, and inspire other women to lead.

Learn more about how protecting seeds became a way of protecting an entire community's future.

Read more via the link in our bio.

Kwa vizazi vingi, wakulima wamehifadhi, kuboresha na kubadilishana mbegu za asili ambazo zimeendelea kulisha familia zet...
05/08/2026

Kwa vizazi vingi, wakulima wamehifadhi, kuboresha na kubadilishana mbegu za asili ambazo zimeendelea kulisha familia zetu na kulinda bioanuwai ya Tanzania.

Leo, mbegu hizi zinakabiliwa na changamoto zinazohatarisha uwepo wake. Ndiyo maana tunazindua kampeni ya ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa mbegu za asili, kuhamasisha ulinzi wa haki za wakulima, na kuhamasisha sera zinazotambua na kuimarisha mifumo ya mbegu inayosimamiwa na wakulima.

📍 Tuungane katika safari hii ya kulinda mbegu zetu ili kulinda kesho yetu.

===========================

For generations, farmers have saved, improved, and exchanged indigenous seeds that have continued to nourish our families and safeguard Tanzania's agrobiodiversity.

Today, these seeds face growing challenges that threaten their survival. That is why we are launching the OurSeedsOurHeritage campaign to raise awareness about the importance of indigenous seeds, promote the protection of farmers' seed rights, and advocate for policies that recognize and strengthen farmer-managed seed systems.

📍 Join us on this journey to protect our seeds and secure our future.




31/07/2026

Filamu hii inaelezea safari ya Mradi wa DTV, ikionesha hali na changamoto ambazo watoto wenye ualbino walikuwa wanakabiliana nazo katika kupata elimu bora na jumuishi kabla ya kuanza kwa mradi, pamoja na mabadiliko makubwa yaliyopatikana kupitia ushirikiano wa wadau mbalimbali.

Mwanzoni mwa mradi, watoto wengi wenye ualbino walikumbana na changamoto mbalimbali, zikiwemo ubaguzi na unyanyapaa, ukosefu wa mazingira jumuishi ya kujifunzia, upungufu wa vifaa muhimu vya kujifunzia, pamoja na vikwazo vingine vilivyoathiri elimu na ustawi wao. Kupitia Mradi wa DTV, changamoto hizi zilishughulikiwa kwa kushirikiana kwa karibu na watoto, wazazi, walimu, shule, mamlaka za serikali za mitaa na jamii kwa ujumla ili kuimarisha ujumuishaji, kuendeleza mifumo ya usaidizi, na kuboresha upatikanaji wa elimu bora kwa watoto wenye ualbino.

Filamu hii inaonesha mafanikio muhimu yaliyopatikana kupitia mradi, ikiwasilisha simulizi za kweli za mabadiliko na athari chanya zilizogusa maisha ya watoto wenye ualbino pamoja na jamii zinazowazunguka. Inaonesha jinsi ushirikiano, kujitolea na mbinu za ujumuishaji zinavyoweza kujenga mazingira ya kujifunzia yanayomwezesha kila mtoto kufikia ndoto na uwezo wake.

Filamu hii inabaki kuwa ushahidi wa maendeleo yaliyopatikana na ukumbusho kwamba kujenga mfumo wa elimu jumuishi kunahitaji dhamira na ushirikiano endelevu kutoka kwa wadau wote. Kwa pamoja, tunaweza kuhakikisha kuwa hakuna mtoto anayeachwa nyuma.

Kila mtoto anastahili fursa ya kujifunza, kushiriki kikamilifu, na kufikia uwezo wake wote.

27/07/2026

Makala hii inaturudisha katika maisha ya watoto wenye ualbino kabla ya kuanza kwa Mradi wa DTV, ikionesha changamoto walizokuwa wanakabiliana nazo kila siku katika kupata elimu bora na jumuishi. Kuanzia mazingira yasiyokidhi mahitaji ya kujifunzia, upatikanaji mdogo wa vifaa saidizi vya kujifunzia, hadi ubaguzi, unyanyapaa na kutengwa katika jamii, filamu hii inaangazia vikwazo vilivyowazuia watoto wengi wenye Ualbino kupata fursa sawa za elimu k**a wenzao.

Kupitia simulizi za kweli, mahojiano na matukio halisi yaliyorekodiwa, filamu hii inaonesha umuhimu wa kuwa na mfumo wa elimu jumuishi unaolinda haki, utu na uwezo wa kila mtoto.

Filamu hii ya awali (baseline documentary) inatukumbusha sababu zilizopelekea kuanzishwa kwa Mradi wa DTV na kuweka msingi wa kuelewa mabadiliko na athari ambazo mradi ulilenga kuleta kwa watoto wenye ualbino, familia zao, shule na jamii kwa ujumla.

Today, ActionAid Tanzania brought together partners and stakeholders in Dodoma for the inception meeting of the Seeds of...
22/07/2026

Today, ActionAid Tanzania brought together partners and stakeholders in Dodoma for the inception meeting of the Seeds of Resilience project.

The meeting marked the beginning of a collaborative journey to strengthen food systems, empower women and youth, and promote solutions that help farming communities adapt to the impacts of

========================

Leo, ActionAid Tanzania imewakutanisha wadau na washirika jijini Dodoma katika Mkutano wa Uzinduzi wa Mradi wa Seeds of Resilience.

Mkutano huu umeashiria mwanzo wa safari ya ushirikiano inayolenga kuimarisha mifumo ya chakula inayostahimili mabadiliko ya tabianchi, kuwawezesha wanawake na vijana, pamoja na kuhamasisha matumizi ya mbinu za zinazosaidia jamii za wakulima kukabiliana na athari za .

Invitation for Bids! ActionAid Tanzania invites interested individuals and organizations to submit bids for the purchase...
10/07/2026

Invitation for Bids!

ActionAid Tanzania invites interested individuals and organizations to submit bids for the purchase of quality used motor vehicles. Visit our offices for inspection and bidding details. Don't miss this opportunity!

Call: +255 754 850 275 for more information

Preparations are underway in Chemba District for the handover of Agricultural tools and production equipment to   benefi...
09/07/2026

Preparations are underway in Chemba District for the handover of Agricultural tools and production equipment to benefiting from the Climate Smart Agriculture Project ( ) supported by and WFP Africa

The event is officiated by the District Executive Director, marking another important step in strengthening climate-resilient agriculture and supporting farmers to improve productivity and livelihoods.


Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 13:00

Telephone

+255754744443

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ActionAid Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to ActionAid Tanzania:

Share