TAWLA Tanzania Women Lawyers Association

TAWLA Tanzania Women Lawyers Association Over the years, it has been our quest to ensure that TAWLAs vision and mission are carried out and our core values upheld.

TAWLA is a Non-Governmental Organization (NGO) which was formed primarily as a guild to promote and advance legal and constitutional rights of women.The aims and objectives of the organization is to advocate for gender equality, promotion of human dignit. Some of our commendable achievements include:

1. Reaching over 2 million people by raising awareness on legal rights through media awareness c

ampaigns both on the radio and television, and training paralegals to be better equipped to serve our communities.

2. TAWLA provides legal aid directly to over 2,000 women and children per year.

3. Directly working for legal reform in Tanzania, including giving women the right to own property with the passage of the Land Act and revising the Sexual Offenses Act to give women protection from Gender Based Violence.

4. Coordinating the Gender Land Task Force (GLTF)

5. Assisting women by promoting will writing to speed the resolution of inheritance issues as well as assisting women in probate matters.

6. Mobilizing lawyers to help vulnerable people through legal aid clinics

7. Creating a network of 570 women lawyers

TAWLA continues to provide legal aid services to women, campaign for women and children's human rights, advocate for good governance, and create forums for women lawyers to build their professional capabilities in the hopes of ensuring greater representation for women in government.

Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) tumefanya mafunzo ya kuongezea ujuzi wadau wa sekta ya utoaji haki (Justi...
02/06/2026

Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) tumefanya mafunzo ya kuongezea ujuzi wadau wa sekta ya utoaji haki (Justice sector actors) katika masuala ya Ukatili wa kijinsia kwenye Halmshauri ya wilaya Arusha.

Wadau walioshiriki ni pamoja na viongozi wa serikali za mitaa, wasaidizi wa Kisheria, Afisa ustawi wa jamii, Dawati la polisi la jinsia na watoto, na Mawakili wa Serikali waendesha mashtaka.

Mafunzo hayo shirikishi yalilenga kutambua majukumu ya wadau hao, kuimarisha ushirikiano baina yao na kuimarisha misingi ya kulinda utu wa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia wakati wakitoa taarifa, upelelezi na uendeshaji wa kesi.


Katika jitihada za kuboresha upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria na kuongeza ufikaji wa huduma hizo kwa jamii ku...
02/06/2026

Katika jitihada za kuboresha upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria na kuongeza ufikaji wa huduma hizo kwa jamii kupitia utekelezaji wa mradi wa Sauti ya Haki chini ya programu ya Wezesha Binti, Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) tumekabidhi pikipiki kwa taasisi tatu za wasaidizi wa kisheria ambazo ni MAPAO, KIPAFO na WAPAO.

Hatua hii inalenga kuimarisha uwezo wa taasisi hizo kufikia wananchi kwa urahisi zaidi, hususan katika maeneo ya vijijini na yaliyo mbali, ili kuhakikisha huduma za msaada wa kisheria zinapatikana kwa wakati na kwa ufanisi.


Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) tulifanya kikao kifupi na wadau wa mradi wa WEZESHA BINTI kutoka Enabel k...
02/06/2026

Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) tulifanya kikao kifupi na wadau wa mradi wa WEZESHA BINTI kutoka Enabel kwa lengo la kujadili maendeleo ya utekelezaji wa programu, mafanikio yaliyofikiwa pamoja na changamoto zilizojitokeza katika kipindi cha utekelezaji.

Kikao hicho kilichohusisha wasaidizi wa kisheria kutoka Kibondo, Kasulu na Kigoma, pia kilihudhuriwa na baadhi ya wanufaika ambao walitoa ushuhuda kuhusu namna walivyofaidika na huduma za msaada wa kisheria zilizotolewa.

Miongoni mwa matokeo yaliyobainishwa ni kuongezeka kwa uelewa wa haki za kisheria kwa wanawake na watoto wa k**e, kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria, pamoja na utatuzi wa baadhi ya migogoro ya kifamilia, ardhi na ukatili wa kijinsia kupitia usaidizi wa wasaidizi wa kisheria.


Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) kwa kushirikiana na shirika la wasaidizi wa kisheria la MAPAO chini ya pr...
02/06/2026

Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) kwa kushirikiana na shirika la wasaidizi wa kisheria la MAPAO chini ya program ya WEZESHA BINTI tulifanya majadiliano ya wadau katika manispaa ya Kigoma kwa lengo la kutambua changamoto za kijamii na kiutendaji zinazopelekea kuwepo kwa matukio ya ukatili wa kijinsia na kuja na mipango ya kuhakikisha changamoto hizo zinaendelea kushughulikiwa.

Majadiliano hayo yalihusisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa jamii, watendaji wa serikali za mitaa, wazee maarufu, viongozi wa dini pamoja na wadau wengine muhimu wa maendeleo.

Kikao hicho kilitoa fursa muhimu ya kubadilishana uzoefu, kujadili mbinu za pamoja za kushughulikia changamoto hizo, na kuimarisha mifumo ya rufaa na utoaji wa msaada wa kisheria.


TTAWLA Tanzania Women Lawyers Associationtumeendelea kuwafikia wananchi wa sehemu mbalimbali na kutengeneza vinara wa us...
02/06/2026

TTAWLA Tanzania Women Lawyers Associationtumeendelea kuwafikia wananchi wa sehemu mbalimbali na kutengeneza vinara wa usawa wa kijinsia.

Kupitia Mpango Mkakati wetu mpya (2026-2030), tunawashirikisha wanaume na wavulana k**a chachu ya uchechemuzi dhidi ya ukatili wa kijinsia na utetezi wa haki za wanawake.

Pamoja tunaweza kujenga jamii yenye haki na usawa

https://youtu.be/SXCbNKMqvu0


Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania(TAWLA) kupitia ofisi yetu ya...

Wanachama wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) walishiriki kikamilifu katika mbio za Wakili Marathon zilizo...
01/06/2026

Wanachama wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) walishiriki kikamilifu katika mbio za Wakili Marathon zilizofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, mkoani Dodoma. Mbio hizi zilizoratibiwa na Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA), zilikuwa na lengo la kimkakati la kuchangisha fedha ili kuimarisha na kusogeza huduma za msaada wa kisheria karibu zaidi na wananchi wa Tanzania.

Katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba, alibainisha kuwa mbali na kuhamasisha utamaduni wa mazoezi kwa afya bora na kupinga tabia bwete, marathon hii ni chombo muhimu cha ukusanyaji wa rasilimali zitakazowezesha upatikanaji wa haki na msaada wa kisheria bila malipo kwa jamii.

Akiongoza jopo la Wanachama wetu, Mkurugenzi wetu Da Tike Mwambipile ameshiriki mbio hizo k**a sehemu ya wadau wakuu na thabiti wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini. Ushiriki wake unasisitiza dhamira ya taasisi yetu katika kushirikiana na sekta nzima ya sheria nchini kuleta mabadiliko chanya na endelevu kwa wananchi.




Mwili wepesi, afya njema na haki karibu zaidi na wananchi.K**a wadau muhimu wa afya ya jamii na upatikanaji wa haki, Cha...
01/06/2026

Mwili wepesi, afya njema na haki karibu zaidi na wananchi.

K**a wadau muhimu wa afya ya jamii na upatikanaji wa haki, Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) kupitia Wanachama wetu tumepata wasaa wa kipekee wa kushiriki katika mbio za Wakili Marathon zilizofanyika Mei 31, 2026 katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Mbio hizi zilizoandaliwa na Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA), zilibeba kaulimbiu ya “Msaada wa Kisheria Karibu zaidi na Watanzania.” Akizungumza kwenye tukio hilo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba, alisisitiza kuwa lengo kuu la marathon hii ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kuimarisha na kusogeza huduma za msaada wa kisheria karibu zaidi na wananchi, sambamba na kuhamasisha utamaduni wa kufanya mazoezi.

Sisi k**a TAWLA, tunaamini kuwa kuuboresha mwili kupitia mazoezi ni nguzo ya kupinga tabia bwete na magonjwa yasiyoambukiza (NCDs), lakini kikubwa zaidi, tunaunga mkono kwa dhati jitihada hizi za kuchangisha rasilimali zitakazosaidia kutoa msaada wa kisheria kwa jamii zenye uhitaji.




The Tanzania Women Lawyers Association (TAWLA), as part of the CAMMAC coalition, had the honor of attending the Excellen...
01/06/2026

The Tanzania Women Lawyers Association (TAWLA), as part of the CAMMAC coalition, had the honor of attending the Excellence in Journalism Awards Tanzania (EJAT).

We extend our heartfelt gratitude to MSI () for inviting and involving us as part of this coalition. MSI proudly sponsored the crucial category of Sexual and Reproductive Health and Rights (SRHR) journalism. Our collaboration with MSI and MST continues to strengthen our collective impact in advocating for health rights and justice in our communities.

Congratulations to MSI for this impactful sponsorship, and a big congratulations to all the award-winning journalists.





30/05/2026

Relive the moments as they happened. ✨


The future is digital, inclusive, and financially independent! At TAWLA, we are advancing our technology to transform ho...
29/05/2026

The future is digital, inclusive, and financially independent!

At TAWLA, we are advancing our technology to transform how we deliver services, resolving legal issues remotely while equipping women with the critical investment and wealth-creation strategies they need to thrive (Daily News).




Address

TAWLA House, Plot 33, Ilala Sharif Shamba
Dar Es Salaam
9460

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

+255 22 2862865

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAWLA Tanzania Women Lawyers Association posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to TAWLA Tanzania Women Lawyers Association:

Share