13/05/2026
WALINDE WATOTO KWA VITENDO, SIO KWA MANENO! 📢
Je, unajua kuwa takribani 85% ya bajeti ya ulinzi wa watoto nchini inategemea wafadhili wa nje? 😮
TGNP imeshirikiana na wadau wa maendeleo jijini Dodoma kuwakumbusha Wabunge na Serikali kuwa wakati umefika wa kuongeza uwekezaji wa ndani katika Bajeti yenye Mrengo wa Kijinsia (GRB).
Wabunge kupitia Kamati za PAC na LAAC wameahidi kusimamia hili ili kuhakikisha:
✅ Wizara zote zinatenga bajeti ya ulinzi wa mtoto.
✅ Fedha zilizopangwa zinatolewa kwa wakati.
✅ Halmashauri zinaimarisha mifumo ya ulinzi wa watoto shuleni na nyumbani.
"Tuzidai wizara zote zibebe suala la ulinzi wa mtoto katika bajeti zao," — Mhe. Aeshi Hilali (Makamu Mwenyekiti wa PAC).
Nini maoni yako? Unafikiri ni sekta gani inapaswa kupewa kipaumbele zaidi katika kumlinda mtoto? Tuandikie hapa chini. 👇
World Vision Tanzania Bunge la Tanzania fans UNFPA Tanzania Plan International Tanzania Child Dignity, Growth and Protection Initiative Deo Koyanga Temba