28/05/2026
Mwenyekiti wa Youth of United Nations Association (YUNA) Tanzania , Bi. Suzane Sylvester akiambatana na Bw. Richard Thomas, Mwenyekiti wa YUNA - UDOM Chapter
Wameungana na wanadiplomasia na viongozi mbalimbali nchini kuhudhuria Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2026/2027 iliyowasilishwa na Mhe. Dkt. Mahmoud Thabit Kombo bungeni Dodoma siku ya tarehe 26 Mei 2026.
Ushiriki huu una umuhimu mkubwa kwa vijana kwani unatoa nafasi ya kuelewa dira ya Tanzania katika diplomasia, ushirikiano wa kimataifa, ajenda za vijana, pamoja na fursa zinazotokana na mahusiano ya kikanda na kimataifa.
Kuhudhuria kwake kunachagiza zaidi ushiriki wa vijana katika masuala ya diplomasia , uongozi, sera za kimataifa na maamuzi ya kitaifa, huku tukijenga kizazi chenye uelewa wa diplomasia na mchango wa vijana katika maendeleo ya Taifa.