YUNA Tanzania

YUNA Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from YUNA Tanzania, Nonprofit Organization, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Youth of United Nations Association (YUNA) Tanzania , Bi. Suzane Sylvester akiambatana na Bw. Richard Thom...
28/05/2026

Mwenyekiti wa Youth of United Nations Association (YUNA) Tanzania , Bi. Suzane Sylvester akiambatana na Bw. Richard Thomas, Mwenyekiti wa YUNA - UDOM Chapter
Wameungana na wanadiplomasia na viongozi mbalimbali nchini kuhudhuria Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2026/2027 iliyowasilishwa na Mhe. Dkt. Mahmoud Thabit Kombo bungeni Dodoma siku ya tarehe 26 Mei 2026.

Ushiriki huu una umuhimu mkubwa kwa vijana kwani unatoa nafasi ya kuelewa dira ya Tanzania katika diplomasia, ushirikiano wa kimataifa, ajenda za vijana, pamoja na fursa zinazotokana na mahusiano ya kikanda na kimataifa.

Kuhudhuria kwake kunachagiza zaidi ushiriki wa vijana katika masuala ya diplomasia , uongozi, sera za kimataifa na maamuzi ya kitaifa, huku tukijenga kizazi chenye uelewa wa diplomasia na mchango wa vijana katika maendeleo ya Taifa.

YUNA Tanzania inawatakia heri na baraka ninyi pamoja na wapendwa wenu katika maadhimisho haya ya sikukuu ya Eid Al-Adha....
27/05/2026

YUNA Tanzania inawatakia heri na baraka ninyi pamoja na wapendwa wenu katika maadhimisho haya ya sikukuu ya Eid Al-Adha.

​Katika kuadhimisha siku hii adhimu ya kutoa dhabihu, tusherehekee kwa kuziishi nguzo kuu za upendo, ukarimu, na mshik**ano katika jamii yetu. Siku hii itujaze sote roho ya kujitolea na kuwajali wengine, hasa wale wenye uhitaji mkubwa zaidi.

​Kheri na amani vitawale katika nyumba zenu!
​Eid Mubarak! ✨

​YUNA Tanzania extends warm wishes to you and your loved ones on this blessed occasion of Eid Al-Adha.
​As we mark this sacred day of sacrifice, let us embody the core values of compassion, selflessness, and unity within our communities.May this day inspire us all to give back, support one another, and spread kindness wherever we go.

​Wishing you and your family a celebration filled with peace, joy, and prosperity.
​Eid Mubarak! ✨



Recently, we had the privilege to enrolled in the capacity building programme by the Foundation for Civil Society (FCS) ...
27/04/2026

Recently, we had the privilege to enrolled in the capacity building programme by the Foundation for Civil Society (FCS) in partnership with UNICEF . The focus was on the Organizational Capacity Assessment (OCA) a vital tool for ensuring that youth and women led CSOs are structured for long term impact and transparency.

​Through this session, we learned how to utilize institutional "health checks" to enhance our governance, financial accountability, and strategic planning. Strengthening these core areas allows us to be more effective, sustainable, and professional in our advocacy for the youth of Tanzania.

​Stronger institutions. Greater impact. A better future for all.





Governance
VolunteerismIsOurSpirit

Kutana na Caroline Malewo k**a mchokoza mada wa pili wa mjadala wetu wa leo!Ndugu Caroline Malewo ni media personality m...
22/04/2026

Kutana na Caroline Malewo k**a mchokoza mada wa pili wa mjadala wetu wa leo!

Ndugu Caroline Malewo ni media personality mwenye uzoefu katika tasnia ya mawasiliano na uwasilishaji wa mada mbalimbali. Ana mchango mkubwa katika kuchochea mijadala yenye uelewa, ubunifu na ushiriki mpana wa jamii kupitia majukwaa ya mawasiliano na vyombo vya habari.

Tunaamini uzoefu na umahiri wake katika tasnia ya media utakuwa chachu muhimu ya majadiliano yenye tija na yenye kujenga katika mjadala wetu wa leo.

Usikose kuungana nasi kuanzia saa 12 hadi saa 2 usiku kwa mazungumzo yenye nguvu na yenye kujenga!

Jiunge nasi kupitia link iliyopo kwenye Bio yetu👆 au link hapa chini
https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Ni heshima kwetu leo kuungana na Joseph Brighton Malekela k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!Joseph B...
22/04/2026

Ni heshima kwetu leo kuungana na Joseph Brighton Malekela k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!

Joseph Brighton Malekela ni Mkurugenzi wa Taasisi ya The African Leadership Initiative for Impact , kiongozi kijana mwenye dira na mchambuzi wa masuala ya maendeleo anayejikita katika uwezeshaji wa vijana, usalama na amani, uongozi bora, na ushiriki wa vijana katika kujenga uchumi wa taifa.

Ameendelea kuwa sauti yenye ushawishi katika kuhamasisha kizazi cha vijana kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo binafsi na ya jamii kwa ujumla.

Usikose kuungana nasi kuanzia saa 12 hadi saa 2 usiku kwa mazungumzo yenye nguvu na yenye kujenga!

Jiunge nasi kupitia link iliyopo kwenye Bio yetu 👆 au link hapa chini:
https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Ni heshima kwetu leo kuungana na Nuria Mshare k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!Nuria Mshare ni kion...
22/04/2026

Ni heshima kwetu leo kuungana na Nuria Mshare k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!

Nuria Mshare ni kiongozi kijana mwenye maono, anayejikita katika masuala ya maendeleo ya vijana, uongozi shirikishi, na uwezeshaji wa jamii kupitia fursa mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Ameendelea kuwa sauti muhimu katika kuhamasisha vijana kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa maendeleo na maamuzi yanayowahusu.

Usikose kuungana nasi kuanzia saa 12 hadi saa 2 usiku kwa mazungumzo yenye nguvu na yenye kujenga!

Jiunge nasi kupitia link iliyopo kwenye Bio yetu 👆 au link hapa chini:
https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Ni heshima kwetu Leo kuungana na Mbunge wa Viti maalumu wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania Mheshimiwa Mary Daniel Surati k*...
22/04/2026

Ni heshima kwetu Leo kuungana na Mbunge wa Viti maalumu wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania Mheshimiwa Mary Daniel Surati k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!

Ndugu Mary Daniel Surati ni Mbunge wa Serengeti na kiongozi mahiri anayejikita katika kuwakilisha wananchi na kusimamia masuala ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Ana uzoefu mkubwa katika uongozi wa umma na amekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha maendeleo jumuishi na ushirikishwaji wa wananchi, hususan vijana na jamii kwa ujumla..

Usikose kuungana nasi kuanzia saa 12 hadi saa 2 usiku kwa mazungumzo yenye nguvu na yenye kujenga!
Jiunge nasi kupitia link iliyopo kwenye Bio yetu👆 au link hapa chini
https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Tunayo furaha kuwa Ndugu Judith Urio ni mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!Judith Urio ni kiongozi mahiri ...
22/04/2026

Tunayo furaha kuwa Ndugu Judith Urio ni mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!

Judith Urio ni kiongozi mahiri wa vijana na mtaalamu wa maendeleo ambaye amejipambanua katika kukuza ushiriki wa vijana kwenye maendeleo endelevu.

Yeye ni Mwenyekiti wa Bodi wa Policy Forum na pia Mkuu wa Idara ya Vijana UNA Tanzania, ambapo anaongoza juhudi za kuwawezesha vijana kiuchumi na kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika maamuzi ya kijamii na kisera.

Usikose kuungana nasi kuanzia saa 12 hadi saa 2 usiku kwa mazungumzo yenye nguvu na yenye kujenga!

Jiunge nasi kupitia link iliyopo kwenye Bio yetu👆 au link hapa chini
https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Tunayo furaha kuwa na  k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!Ndugu Arif ni Mratibu wa Jukwaa la Kimataif...
22/04/2026

Tunayo furaha kuwa na k**a mmoja wa wazungumzaji wetu kwenye mjadala wa leo!

Ndugu Arif ni Mratibu wa Jukwaa la Kimataifa , akiwa na uzoefu katika masuala ya uongozi na uwezeshaji wa vijana. Amejikita katika kuhamasisha mabadiliko chanya na endelevu kupitia ushirikishwaji wa vijana na jamii kwa ujumla.

Usikose kuungana nasi kuanzia saa 12 hadi saa 2 usiku kwa mazungumzo yenye nguvu na yenye kujenga!

Jiunge nasi kupitia link iliyopo kwenye Bio yetu👆 au link hapa chini
https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Kutana na  mchokoza mada kwenye mjadala wetu wa leo!Paul Amara ni mtangazaji mahiri wa luninga na redio hapa nchini Tanz...
22/04/2026

Kutana na mchokoza mada kwenye mjadala wetu wa leo!

Paul Amara ni mtangazaji mahiri wa luninga na redio hapa nchini Tanzania.Ataungana nasi leo kuanzia saa 12 jioni hadi saa 2 usiku kuhakikisha mjadala unakuwa na matokeo chanya.

Jiandae kwa hoja zenye nguvu, maswali ya kuchochea fikra, na mazungumzo yenye tija. Usipange kukosa!

Kushiriki tumia link iliyopo kwenye Bio yetu 👆 au link hii

https://meet.google.com/akn-pbsd-syy

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when YUNA Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share