10/06/2026
Jumamosi (Juni 6, 2026), tulishiri katika "Hafla ya Utoaji wa Zawadi kwa Washindi wa Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari." Hafla hiyo ilifanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo walimu 35 kote nchini walitambuliwa kwa ubora na ubunifu wao katika ufundishaji. ilishiriki katika hafla hiyo ili kuunga mkono juhudi za Serikali za kuimarisha stadi za kusoma na kuandika.
Hafla hiyo iliandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu. Mgeni rasmi, Prof. Riziki Shemdoe (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, aliwahimiza walimu kutumia mbinu bunifu za ufundishaji na matumizi ya teknolojia ili kuwasaidia wanafunzi kukuza uwezo wa kufikiri kwa kina na kutatua changamoto, stadi ambazo ni muhimu katika karne ya 21.
Tunawapongeza washindi wote, juhudi zenu ni mwanga unaoangaza mustakabali wa elimu nchini.
Tunajivunia ushirikiano wetu na serikali na wadau wa elimu nchini katika kuimarisha ujifunzaji na kuhakikisha kila mtoto anajifunza, anakua na kustawi.