Umoja wa Waandishi wa Vitabu Tanzania - uwavita

Umoja wa Waandishi wa Vitabu Tanzania - uwavita UWAVITA ni chama cha kitaifa kinachowaunganisha waandishi wote wa vitabu Tanzania. Kuanzishwa 1974 | Kusajiliwa 1979.
(1)

Tunawashukuru  kwa kutambua juhudi na mchango wa UWAVITA katika kuimarisha ujumuishi katika tasnia ya uandishi wa vitabu...
17/04/2026

Tunawashukuru kwa kutambua juhudi na mchango wa UWAVITA katika kuimarisha ujumuishi katika tasnia ya uandishi wa vitabu Tanzania ambapo UWAVITA ilifanikiwa kuonesha vitabu vya watoto vya nukta nundu katika Tamasha la Kimataifa la Vitabu Tanzania lililoandaliwa na PATA.

Hongera UWAVITA!
Hongereni Waandishi!

UWAVITA KIDEDEA!Wanachama wa UWAVITA katika picha za matukio tofauti tofauti.Tunaendelea kumpongeza Bi. Amina Mohammed, ...
14/04/2026

UWAVITA KIDEDEA!

Wanachama wa UWAVITA katika picha za matukio tofauti tofauti.

Tunaendelea kumpongeza Bi. Amina Mohammed, akipokea kijiti kutoka kwa mshindi wa mwaka jana Bi. Tune Salim. Wote wakitokea UWAVITA, washindi wa kategoria ya Hadithi za Watoto!

Tuzonyerere Taasisiyaelimutanzania Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

UWAVITA KIDEDEA!Hongera Bi. Amina Mohammed, ukipokea kijiti kutoka kwa mshindi wa mwaka jana Bi. Tune Salim. Wote wakito...
14/04/2026

UWAVITA KIDEDEA!

Hongera Bi. Amina Mohammed, ukipokea kijiti kutoka kwa mshindi wa mwaka jana Bi. Tune Salim. Wote wakitokea UWAVITA, washindi wa kategoria ya Hadithi za Watoto!

Tuzonyerere Taasisiyaelimutanzania Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Miongo 5 Tangu Kuasisiwa.
11/04/2026

Miongo 5 Tangu Kuasisiwa.

SEMINA YA HAKIMILIKIKwenu wanachama wa UWAVITATarehe: 11 Machi 2026Ukumbi: Eco Sanaa Hub (CDEA), Mbezi BeachMuda: 3:00 a...
09/03/2026

SEMINA YA HAKIMILIKI
Kwenu wanachama wa UWAVITA
Tarehe: 11 Machi 2026
Ukumbi: Eco Sanaa Hub (CDEA), Mbezi Beach
Muda: 3:00 asubuhi
Karibuni sana.

Furaha Tele!
14/02/2026

Furaha Tele!

Tutakuwepo!
13/02/2026

Tutakuwepo!

Yaliyojiri Siku ya Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Vitabu Tanzania 2025, Maktaba Kuu. Umoja wa Waandishi wa Vitabu ...
21/11/2025

Yaliyojiri Siku ya Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Vitabu Tanzania 2025, Maktaba Kuu.

Umoja wa Waandishi wa Vitabu Tanzania ulipata fursa ya kushiriki maonesho haya ya kimataifa ya vitabu nchini yaliyoandaliwa na umoja wa Wachapishaji Vitabu Tanzania (PATA). Mgeni Rasmi akiwa ni Mheshimiwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi.

Mgeni rasmi alipata nafasi ya kutembelea banda la UWAVITA - banda namba 12 na kupelekea vitabu vya waandishi wa UWAVITA kutia fora! Pamoja na vitabu vyengine, palikuwa na "Kamusi ya Kisumbwa-Kiswahili-Kingereza ya Prof. KK Kahigi", kitabu cha Ushairi cha Omary Baajun "Olives, Watermelon & Kufiyyeh: Poems for Palestine", pia kitabu cha "Rafiki yangu Kipepeo" cha Gwiji Hussein Wamaywa alivyopewa k**a zawadi.

Kwa upekee kabisa aliguswa na vitabu vya Nukta nundu akisema, aliwahi Kusoma na wanafunzi wenye changamoto ya uoni, hivyo kupatikana kwa machapisho hayo ni jambo zuri.

UWAVITA ilipata dakika chache za kusema jambo kuhusu Umoja wetu. Mheshimiwa Waziri amepongeza sana juhudi za waandishi katika kuandika na kuchapa machapisho.

Aidha, kwa upekee kabisa, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi alimpa maua yake Mwalimu Richard Mabala, ambaye ni mwanachama na miongoni mwa walezi wa UWAVITA.

Mwenyekiti wa PATA naye alitoaa maombi kadhaa:
- Isaidie uuandaaji wa Sera ya vitabu na usomaji wa vitabu Tanzania.
- Udhamini wa kudumu toka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na Wizara ya Elimu.
- Uwezeshwaji wa Wajumbe kutoka Tanzania katika Maonesho ya Vitabu Duniani.
- Ipitishe vifaa vya tozo ya vibebeo vya kazi za machapisho.
- Ukumbi wa Maonesho ya Vitabu katika Sports Arena.
- Maktaba ya Kimataifa ya Kiswahili na Duka la vitabu.

Imetolewa na;
Ofisi ya Katibu Mkuu
UWAVITA

Tupo Banda Namba 12 Mkabala na Mkahawa.
20/11/2025

Tupo Banda Namba 12 Mkabala na Mkahawa.

Muendelezo wa Orodha Iliyopita.
20/11/2025

Muendelezo wa Orodha Iliyopita.

Orodha ya Baadhi ya Vitabu Vitakavyopatikana Katika Maonesho ya Kimataifa ya Vitabu, Maktaba Kuu. Tupo Banda Namba 12.
20/11/2025

Orodha ya Baadhi ya Vitabu Vitakavyopatikana Katika Maonesho ya Kimataifa ya Vitabu, Maktaba Kuu. Tupo Banda Namba 12.

Tutashiriki
18/11/2025

Tutashiriki

Address

Haile Selassie
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Umoja wa Waandishi wa Vitabu Tanzania - uwavita posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Umoja wa Waandishi wa Vitabu Tanzania - uwavita:

Share