Mwl.Deo Kabuje

Mwl.Deo Kabuje Emitting beautiful positive vibes to educate,inspire, encourage and heal.

07/06/2026

ENDELEA KUSIMAMA

Wakati mwingine maisha hayana adabu kabisa.

Unaweza kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii sana lakini wapi mambo hayaendi.

Mshahara wako ni hautoshi,si boss wala ofisi yako wanatambua jitihada zako.

Hakuna marupurupu wala nyongeza ya mshahara yaani ni hivi vyuma vimekaza blaza.

ENDELEA KUSIMAMA

Haya mjomba unaamua kujichanganya unafungua kibiashara chako angalau ujikomboe kimaisha.

Hapo ndo kwanza mambo hayaendi mbaya zaidi unaongeza madeni juu biashara inakufa.

ENDELEA KUSIMAMA

Unakuwa mwaminifu kwa Mungu na wanadamu.

Haujawahi kuiba ,kutukana wala kumfanyia mtu ubaya wowote lakini bado maisha yanakupiga ngumi tena za uso.

ENDELEA KUSIMAMA

Pengine familia yako ndo imekuwa faraja kwako.

Ndo kwanza unamiaka mitatu kwenye ndoa na Mungu amewabariki kachalii kamoja unaitwa baba Ima.

Wife kuona life limechanganya anakwambia;

Hukunioa ili nipate shida hapa mjini anaondoka na mwanae na kurudi kwao.

ENDELEA KUSIMAMA

Kwanza pole kwa yote blaza ,na ushauri wangu kwako ni kwamba;
ENDELEA KUSIMAMA

~Mwl Deo Kabuje
+255767451108

06/06/2026

05/06/2026
27/05/2026

✝️❤

23/05/2026

Hasira inakua ndani ya mtu na ndio maana haitakiwi kukuaa kwa muda mrefu.

"Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;..
Waefeso 4:26

K**a utashindwa kuizuia hasira yako basi unaweza kupata madhara makubwa zaidi.

"Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako,
Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu"
Mhubiri 7:9

Jifunze kuachilia,usiwe mpumbavu.

Karibu sana kwenye kundi la watu waliomua kuwa na mioyo ya kuachilia.

~Mwl Deo Kabuje


16/05/2026

Kweli muhimu kuhusu fedha

15/05/2026

Mungu anatutaka kuwa na ukubwa wa kuwa tayari kuwa wadogo kutumiwa na yeye.

Mungu huwaita wale wenye utayari tu wa kutumiwa na yeye.

Mungu hakuiti kwa sababu ya elimu ,yako ,udhoefu wako au hata umaarufu wako.

Mungu anao uwezo wa kugeuza udhaifu wako ukawa nguvu.

1 Wakorintho 1:26-27

"Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu.

Mwl Deo Kabuje
+255 673 074 697

14/05/2026

Hakuna mlima ambao hauwezi kuupanda labda ukwamishwe na kiwango cha ufahamu wako.

Hakuna namna utafanikiwa zaidi ya kiwango cha ufahamu wako.

Ni ukweli utakaoujua ndio utakao kuweka huru...tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. Yoh 8:32

Sitoacha kukukumbusha kuwa ujuaji peke yake hautakuweka huru ikiwa hatutafanyia kazi yale yote unayoyajua.

Mwl Deo Kabuje
255 673 074 697

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255767451108

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwl.Deo Kabuje posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Mwl.Deo Kabuje:

Share