Tanzaniaredcross

Tanzaniaredcross The Tanzania Red Cross Society (TRCS) was established as an independent National Society (NS) by an Act of Parliament No. 71 of December, 1962. www.trcs.or

Tawi la Mkoa wa Pwani limeungana na wanachama pamoja na volunteers kuadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kupitia shughul...
11/05/2026

Tawi la Mkoa wa Pwani limeungana na wanachama pamoja na volunteers kuadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo upandaji wa miti, usafi wa mazingira na uchangiaji wa damu.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika Wilaya ya Rufiji ndani ya Ukumbi wa FDC-Ikwiriri, yakihusisha wanachama na wadau mbalimbali wa Tanzania Red Cross Society.

Tanzania Red Cross Society Dodoma Branch imeadhimisha Siku ya Red Cross Day 2026 kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo upa...
11/05/2026

Tanzania Red Cross Society Dodoma Branch imeadhimisha Siku ya Red Cross Day 2026 kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo upandaji wa miti, ugawaji wa vifaa vya shule kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Mlezi pamoja na chakula cha pamoja kwa wanachama na volunteers.

Maadhimisho hayo yalifanyika katika Ofisi ya Tawi la Dodoma na kuhudhuriwa na wanachama pamoja na volunteers. Aidha, vyeti vya pongezi vilitolewa kwa voluntia,mtoa huduma ya kwanza na mhamasishaji bora wa mwaka.

:

Mkoa wa Manyara umeadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kwa matendo ya huruma, ikiwemo kutoa sabuni, sukari na zawadi mba...
09/05/2026

Mkoa wa Manyara umeadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kwa matendo ya huruma, ikiwemo kutoa sabuni, sukari na zawadi mbalimbali kwa wagonjwa hospitalini pamoja na kufanya usafi katika vituo vya afya.

Wilaya za Simanjiro, Hanang, Kiteto na Babati zimeshiriki kikamilifu katika shughuli hiyo ya kibinadamu. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa TRCS Mkoa wa Manyara, Wakili Moses Basilla, hatua hiyo ni heshima kwa muasisi wa Red Cross Duniani, Dr. Henry Dunant, aliyeasisi dhana ya kusaidia wenye uhitaji.

TRCS Mkoa wa Arusha imeadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kwa kutoa msaada wa vyakula na mahitaji katika Kituo cha Wato...
09/05/2026

TRCS Mkoa wa Arusha imeadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kwa kutoa msaada wa vyakula na mahitaji katika Kituo cha Watoto Yatima cha Shalom, Karatu.

Shughuli hiyo iliongozwa na Bi. Dora Samson Mushi, akisisitiza umuhimu wa upendo, mshikamano na kusaidia makundi yenye uhitaji katika jamii.

Tawi la Mkoa la Tanzania Red Cross Society Kigoma kwa kushirikiana na wanachama pamoja na voluntia, limeadhimisha Siku y...
09/05/2026

Tawi la Mkoa la Tanzania Red Cross Society Kigoma kwa kushirikiana na wanachama pamoja na voluntia, limeadhimisha Siku ya Red Cross Duniani kwa kufanya usafi na kutoa majitoleo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Maweni - Kigoma.

Aidha, wanachama na voluntia walitembelea na kutoa majitoleo katika Nyumba ya Kulea Wazee Silabu – Kibirizi, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza huduma za kibinadamu na kuonesha upendo kwa jamii.

Katika maadhimisho ya Wiki ya Red Cross Duniani, wanachama wa Tanzania Red Cross Society (TRCS) kutoka mikoa mitatu ya U...
09/05/2026

Katika maadhimisho ya Wiki ya Red Cross Duniani, wanachama wa Tanzania Red Cross Society (TRCS) kutoka mikoa mitatu ya Unguja wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mkoa wa Kaskazini Unguja (MNEC) Ndugu Mohd Ali Sheha, walifanya zoezi la upandaji wa mikoko katika kijiji cha Bumbwini, Shehia ya Mafufuni Zanzibar.

Zoezi hilo lilihusisha ushiriki wa wanachama wa TRCS, maafisa kutoka Idara ya Misitu Zanzibar, Mamlaka ya Mazingira Zanzibar (ZEMA) pamoja na wananchi wa Shehia ya Mafufuni.

Jumla ya mikoko 2,000 ilipandwa sambamba na kupatikana kwa wanachama wapya 25 kutoka Shehia ya Mafufuni.

TRCS inaendelea kuhamasisha utunzaji wa mazingira na kushirikiana na jamii katika kulinda rasilimali za asili kwa maendeleo endelevu.

08/05/2026

Kwa miaka 64, Tanzania Red Cross Society imeendelea kusimama upande wa ubinadamu, kutoa matumaini, msaada na huduma kwa ...
08/05/2026

Kwa miaka 64, Tanzania Red Cross Society imeendelea kusimama upande wa ubinadamu, kutoa matumaini, msaada na huduma kwa jamii zenye uhitaji nchini kote.

Tunapoadhimisha Siku ya Red Cross Duniani 2026, tunaendelea kuunganishwa na kauli mbiu ya mwaka huu:
“UNITED IN HUMANITY"

Asanteni kwa kuwa sehemu ya safari hii ya utu, kujitolea na kuokoa maisha kwa zaidi ya miongo sita.

Happy 64th Anniversary Tanzania Red Cross Society!

     RedCrossTanzaniaTRCS64HumanityInActionWorldRedCrossDayServingHumanityNguvuYaUtuVolunteerForHumanityAlwaysThereYears...
07/05/2026






RedCrossTanzania
TRCS64
HumanityInAction
WorldRedCrossDay
ServingHumanity
NguvuYaUtu
VolunteerForHumanity
AlwaysThere
YearsOfImpact
TogetherForHumanity

Katika Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya Red Cross Duniani,  Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Bi. Dora Samson Mushi ameongoza ...
07/05/2026

Katika Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya Red Cross Duniani, Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Bi. Dora Samson Mushi ameongoza kampeni ya “IJUE RED CROSS" pamoja na mafunzo ya Huduma ya Kwanza kwa viongozi na makamishna wa TANAPA Makao Makuu pamoja na viongozi wa waongoza watalii wa Hifadhi za Arusha.

Uhamasishaji huo umefanyika katika Ukumbi wa Olasiti Garden ambapo washiriki wameonesha kuguswa na umuhimu wa huduma za Red Cross na mafunzo ya Huduma ya Kwanza.

Baada ya mafunzo hayo, TANAPA imeonesha utayari wa kushirikiana na Tanzania Red Cross Society kwa:
Kufundishwa Huduma ya Kwanza kwa wafanyakazi wa Hifadhi za Taifa nchi nzima.
Kuwa mabalozi wa TRCS kwa wadau mbalimbali hususan makampuni ya waongoza watalii.

Mwenyekiti wa Mkoa anawashukuru viongozi pamoja na voluntia wote walioshiriki kufanikisha tukio hili muhimu.

Kauli mbiu 2026: UNITED IN HUMANITY

Address

Mikocheni Mwaikibaki Road
Dar Es Salaam

Telephone

+255765132555

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzaniaredcross posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Tanzaniaredcross:

Share