Mwanamke na Uongozi

Mwanamke na Uongozi A Tanzanian NGO strives to promote Women's full, effective participation and equal opportunities for leadership at all levels of decision making.

Eid Mubarack kwetu soteMwenyezi Mungu azijaze nyoyo zetu amani, furaha na baraka tele katika siku hii tukufu. Asanteni k...
27/05/2026

Eid Mubarack kwetu sote

Mwenyezi Mungu azijaze nyoyo zetu amani, furaha na baraka tele katika siku hii tukufu.

Asanteni kwa kuwa sehemu ya safari yetu. Tupendane, tushirik**ane na tuendelee kushirikana pamoja.

Kupitia warsha hii, tumepata nafasi ya kukutana na wanawake na mabinti kutoka sehemu mbalimbali na kuzungumza kwa uwazi ...
25/05/2026

Kupitia warsha hii, tumepata nafasi ya kukutana na wanawake na mabinti kutoka sehemu mbalimbali na kuzungumza kwa uwazi kuhusu afya ya hedhi, changamoto wanazokutana nazo na namna wanavyoendelea kuwa imara kila siku.

Majadiliano yetu yameonyesha kuwa bado wanawake wengi wanahitaji elimu sahihi, mazingira salama na jamii inayoweza kusikiliza bila hukumu. Lakini pia tumeshuhudia nguvu kubwa ya wanawake kuinuana, kupeana maarifa na kuwa sehemu ya mabadiliko chanya kwa wengine.

Tunaamini mazungumzo k**a haya yanaweza kuwafikia wanawake wengi zaidi, kuvunja ukimya na kujenga jamii yenye uelewa na msaada kwa kila mwanamke.

Wasichana wengi hukosa mazingira rafiki ya kujisitiri, hukumbwa na aibu, kukosa vifaa salama vya hedhi, pamoja na kukati...
25/05/2026

Wasichana wengi hukosa mazingira rafiki ya kujisitiri, hukumbwa na aibu, kukosa vifaa salama vya hedhi, pamoja na kukatishwa masomo kwa muda kutokana na maumivu au hofu ya kunyanyapaliwa. Licha ya changamoto hizi, wameendelea kuwa jasiri, kusaidiana wenyewe kwa wenyewe, kutafuta elimu sahihi na kupaza sauti zao ili jamii iweze kuelewa na kuwapa msaada wanaouhitaji.

Kupitia warsha hii, tumejifunza kuwa kila msichana anastahili kupata elimu sahihi ya afya ya hedhi, mazingira salama shuleni na nafasi ya kutimiza ndoto zake bila vikwazo vinavyotokana na hedhi. Tuendelee kushirikiana kuwafikia wasichana wengi zaidi na kuvunja ukimya kuhusu

Kila mwaka  tunaadhimisha  Mwezi wa Hedhi Salama Duniani,tuendelee kukumbuka kwamba  afya ya uzazi ni sehemu muhimu ya m...
20/05/2026

Kila mwaka tunaadhimisha Mwezi wa Hedhi Salama Duniani,tuendelee kukumbuka kwamba afya ya uzazi ni sehemu muhimu ya maisha, utu na ni afya kwa kila msichana na mwanamke. Hedhi si aibu, si udhaifu, wala si sababu ya kunyimwa nafasi ya Elimu, kazi au kushiriki kikamilifu kwenye nafasi ya Uongozi katika jamii. Bado wasichana wengi wanakosa taarifa sahihi, vifaa salama vya hedhi na mazingira rafiki kutokana na unyanyapaa uliopo kwenye jamii zetu. Ni wakati wa kuvunja ukimya, kuelimisha bila hofu na kujenga jamii inayothamini afya na heshima ya mwanamke.

Tushirikiane kuhakikisha kila msichana anapata haki ya hedhi salama, elimu sahihi ya afya ya uzazi na kujiamini kila siku.


Kumekua na wimbi kubwa la taarifa zisizo sahihi mitandaoni kwa kila mmoja kuzungumzia issue za uzazi..!! Lakini wengi wa...
18/05/2026

Kumekua na wimbi kubwa la taarifa zisizo sahihi mitandaoni kwa kila mmoja kuzungumzia issue za uzazi..!!

Lakini wengi wamekua wakizungumza kwa nadharia bila kua na Taaluma sahihi ya wanachokizungumzia..!

Karibu katika event ya her flow gathering..! Kujifunza na kupata majibu ya changamoto zozote za uzazi ulizokua unajiuliza bila kupata majibu sahihi📌

Karibu tujifunze namna huru..! Tuongeze networking
kwa ada ya tsh 30,000/= tu

Namba ya malipo 0752820316
Mpesa jina : Mwanamke na Uongozi.

Kumbuka zimebaki siku 5 tu, karibuni sana sote tujumuike pamoja

Mwambie rafiki yako, amwambie rafiki yake 🥰🥰

Hedhi Salama ni jukumu letu sote


Karibu kwenye Her Flow Gathering Tunayo furaha kukukaribisha kwenye gathering yetu itakayofanyika tarehe 23/05/2026, sik...
16/05/2026

Karibu kwenye Her Flow Gathering

Tunayo furaha kukukaribisha kwenye gathering yetu itakayofanyika tarehe 23/05/2026, siku ya Jumamosi, Shummy Taste.

Mzungumzaji wetu atakuwa ni Shamira Mshangama, ambaye atakuwepo kushiriki nasi mawazo, uzoefu na mazungumzo yenye kujenga kuhusu maendeleo na Uongozi wa Wanawake.

🎟️ Kiingilio ni Shilingi 30,000 tu
Hakikisha unalipia mapema ili kuhifadhi nafasi yako.

Wahi sasa, Nafasi ni chache



15/05/2026

Mwanamke na Uongozi kwa kushirikiana na Afya Yangu Foundation tunakualika kwenye tukio maalum la “Her Flow Gathering” Jukwaa hili litakuwa la kipekee sana kuwakutanisha mabinti na wanawake kwa mazungumzo ya wazi, ya karibu na yenye kujenga.

🎯 Lengo letu ni:
Kujadili kwa kina masuala ya Hedhi Salama, Uongozi, Sisterhood, pamoja na Afya ya Uzazi kwa ujumla, ili kujenga uelewa sahihi na kuimarisha nafasi ya mwanamke katika jamii ya leo.

💬 Katika siku hii utapata fursa ya:

* Kujifunza na kupata maarifa sahihi
* Kushirikiana uzoefu na wanawake wengine
* Kujenga kujiamini na kujitambua k**a mwanamke
* Kujadili changamoto za hedhi na namna ya kuzitatua kwa pamoja
* Kujifunza kwa uwazi kuhusu afya ya uzazi

🎲 Zaidi ya yote:
Tutashiriki michezo mbalimbali (games) itakayochochea kujifunza kwa njia ya kufurahia na kuongeza uzoefu.

🍽️ Na siku hiyo;
Tutakula, tutakunywa, na kusherehekea pamoja Mwezi wa Wanawake Duniani, tukihamasisha umuhimu wa Hedhi Salama.

⚠️ Kumbuka: Nafasi ni chache sana
Wahi kujisajili kwa kulipia kupitia nambari: 0752820316
(Jina litaonekana: Mwanamke na Uongozi)

🤝 Karibu tusherekee pamoja, huku tukijenga mshik**ano na kuendeleza mazungumzo muhimu ya kijamii yanayomhusu mwanamke wa leo.



HER FLOW GATHERING 🌸Mwanamke na Uongozi kwa kushirikiana na Afya Yangu Foundation tunakualika kwenye tukio maalum la “He...
12/05/2026

HER FLOW GATHERING 🌸

Mwanamke na Uongozi kwa kushirikiana na Afya Yangu Foundation tunakualika kwenye tukio maalum la “Her Flow Gathering” Jukwaa hili litakuwa la kipekee sana kuwakutanisha mabinti na wanawake kwa mazungumzo ya wazi, ya karibu na yenye kujenga.

🎯 Lengo letu ni:
Kujadili kwa kina masuala ya Hedhi Salama, Uongozi, Sisterhood, pamoja na Afya ya Uzazi kwa ujumla, ili kujenga uelewa sahihi na kuimarisha nafasi ya mwanamke katika jamii ya leo.

💬 Katika siku hii utapata fursa ya:

* Kujifunza na kupata maarifa sahihi
* Kushirikiana uzoefu na wanawake wengine
* Kujenga kujiamini na kujitambua k**a mwanamke
* Kujadili changamoto za hedhi na namna ya kuzitatua kwa pamoja
* Kujifunza kwa uwazi kuhusu afya ya uzazi

🎲 Zaidi ya yote:
Tutashiriki michezo mbalimbali (games) itakayochochea kujifunza kwa njia ya kufurahia na kuongeza uzoefu.

🍽️ Na siku hiyo;
Tutakula, tutakunywa, na kusherehekea pamoja Mwezi wa Wanawake Duniani, tukihamasisha umuhimu wa Hedhi Salama.

⚠️ Kumbuka: Nafasi ni chache sana
Wahi kujisajili kwa kulipia kupitia nambari: 0752820316
(Jina litaonekana: Mwanamke na Uongozi)

🤝 Karibu tusherekee pamoja, huku tukijenga mshik**ano na kuendeleza mazungumzo muhimu ya kijamii yanayomhusu mwanamke wa leo.



Kila mtoto ana haki, ana ndoto, na anastahili upendo na nafasi sawa na wengine ya kusonga mbele.Tuwapende, tuwaunge mkon...
11/05/2026

Kila mtoto ana haki, ana ndoto, na anastahili upendo na nafasi sawa na wengine ya kusonga mbele.Tuwapende, tuwaunge mkono, na tuwe sababu ya tabasamu lao leo na kila siku.

Happy Monday to you all🎉

Address

Sinza A
Dar Es Salaam

Telephone

+255752820316

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwanamke na Uongozi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Mwanamke na Uongozi:

Share