11/05/2026
FASIHI IMEFIKA UWANJANI
UWARIDI tunatoa pongezi za dhati kwa mtangazaji wa Azam TV, Bwana Ramadhan Ngoda, kwa namna alivyoiinua na kuiweka fasihi andishi ya Kiswahili katika jukwaa kubwa la michezo kupitia matangazo ya Kariakoo Derby, tarehe 3 Mei, 2026.
Katika zama ambazo vijana wengi hukutana zaidi na simulizi kupitia burudani nyinginezo, hatua yake ya kuitaja na kuhusisha fasihi andishi kwenye matangazo ya soka si jambo dogo.
Ni kitendo cha kuifanya fasihi kuwa sehemu ya mazungumzo ya kawaida ya jamii kwa kuionesha (jamii) kuwa riwaya, hadithi waandishi wetu na maandishi yetu vinaweza kuishi sambamba na michezo, muziki na maisha ya kila siku.
Kwa kufanya hivyo, amechangia kile tunachokiita:
“Kuipa Fasihi ya Kiswahili Sauti.”
UWARIDI tunaamini kuwa taifa linalosoma ni taifa linalofikiri. Na kila sauti inayobeba vitabu, waandishi na simulizi za Kiswahili kwenda kwa umma, ni “sauti ya fasihi," na mshirika wa mapinduzi ya kifikra na kimaarifa nchini.
Asante Ramadhan Ngoda kwa kuitambua fasihi.
Asante kwa kuipa fasihi jukwaa.
Asante kwa kuifanya fasihi isik**e katikati ya shangwe za kabumbu.
Wewe ni Sauti ya Fasihi.