Warehouse Christian Center

Warehouse Christian Center MAFUNDISHO YA KINA YA NENO LA MUNGU KWA USAHIHI - NENO LA MUNGU, NDOA, MAHUSIANO YA VIJANA NA UCHUMBA
(1)

07/06/2026

MFANYE MUNGU AWE MCHUNGAJI WAKO

07/06/2026

SUNDAY SERVICE - 07 JUNE 2026

02/06/2026

WCC - BIBLE STUDY 2 JUNE 2026

02/06/2026

WAPENDWA SHALOM SHALOM..... Hii salamu yetu... ni siku moja tu kwa mwezi! Tunapata nafasi ya kusifu na kuabudu

WCC - HATUNAGA HABARI MBAYA

02/06/2026

JIPE FURAHA, AMANI NA MOTISHA WEWE MWENYEWE. USISUBIRI MTU MWINGINE AKUPE SABABU YA KUTABASAMU.

WATU UNAOWASUBIRI WAKUTIE MOYO NA WAO WANAPITIA VITA VYAO KIMYA KIMYA. FURAHA YA KWELI HAIANZI KWA WENGINE, INAANZIA NDANI YAKO.

AMUA KUCHEKA, AMUA KUSHUKURU, AMUA KUSONGA MBELE HATA K**A MAMBO HAYAJAKAA SAWA. UKIWEZA KUJITIA MOYO MWENYEWE, HAKUNA KIKWAZO KITAKACHOWEZA KUSIMAMISHA HATMA YAKO.

KUMBUKA: NGUVU YAKO KUBWA SIYO WATU WALIO KARIBU YAKO, BALI NI UWEZO WAKO WA KUJITIA MOYO WAKATI HAKUNA ANAYEKUSHANGILIA.

Mwalimu George Luhui - WCC

01/06/2026

MWANAUME YESU NI KIBOKO YAO! πŸ”₯🦁

Alishinda kifo na mauti.
Shetani akimuona, anatetemeka.
Mapepo, majini na nguvu zote za giza zikimuona, zinatetemeka.

Wanamtambua k**a Simba wa Kabila la Yuda Mshindi wa milele, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana! πŸ‘‘

Ilikuwa ni ibada ya kipekee ya sifa na kuabudu mbele za Bwana, iliyojaa uwepo wa Mungu, furaha na ushindi.

Je, uko tayari kwa Season 4? πŸ”₯

Usipange kukosa kile ambacho Mungu ameandaa kwa ajili yako.

Mungu awabariki sana CA's The Heroes kwa kujitoa kwenu, upendo wenu na huduma yenu ya kumtukuza Mungu.

WCC – Upendo Ndio Pumzi Yetu ❀️

01/06/2026

Tunamshukuru Mungu kwa kutuvusha salama kutoka mwezi uliopita na kutuleta katika Mwezi wa 6. Sio kwa nguvu zetu, sio kwa akili zetu, bali ni kwa neema na rehema zake.

Huenda miezi iliyopita haikuwa rahisi. Huenda uliomba na bado hujaona majibu. Huenda ulilia kimya kimya wakati wengine walidhani unaendelea vizuri. Lakini Mungu anayejua mwisho tangu mwanzo anakwambia leo: "Usiogope, mimi niko pamoja nawe."

Mwezi huu wa 6 usiwe mwezi wa kukata tamaa, bali uwe mwezi wa kuamini tena. Amini tena ndoto zako. Amini tena maombi yako. Amini tena ahadi za Mungu juu ya maisha yako. Kile ambacho kilionekana hakiwezekani, Mungu anaweza kukigeuza kuwa ushuhuda wako.

Ninaomba mwezi huu uwe mwanzo wa habari njema ulizokuwa ukizisubiri. Mungu afungue milango ambayo hakuna mwanadamu anaweza kuifunga. Akufanyie njia mahali ambapo uliona hakuna njia. Akubadilishe machozi yako kuwa furaha, maumivu yako kuwa ushuhuda, na mapambano yako kuwa ushindi.

Usikate tamaa. Endelea kusonga mbele. Endelea kuomba. Endelea kumwamini Mungu. Kumbuka: Ikiwa Mungu amekuvusha hadi leo, basi ana sababu ya kukuweka hai. Na sababu hiyo ni kubwa kuliko changamoto unazopitia.

Karibu Mwezi wa 6
Mwezi wa Neema
Mwezi wa Fursa Mpya
Mwezi wa Ushuhuda
Mwezi wa Kushinda

Mungu akupiganie na akukushindie katika kila vita vya maisha yako.

Amen.

31/05/2026

WCC - SUNDAY SERVICE 31 MAY 2026

WATAFITI waliwahi kusema kuwa katika kila watu kumi, kuna wawili wenye tabia ngumu au zinazotusumbua. Hii ina maana kwam...
31/05/2026

WATAFITI waliwahi kusema kuwa katika kila watu kumi, kuna wawili wenye tabia ngumu au zinazotusumbua. Hii ina maana kwamba katika kila watu mia, unaweza kukutana na watu ishirini wa aina hiyo.

Lakini ukweli ni kwamba, hawapo kwa bahati mbaya. Mara nyingi Mungu huruhusu tukutane na watu wa aina hii ili kutuinua kiroho, kutufundisha uvumilivu, hekima, maombi, na namna ya kuhusiana na watu tofauti katika maisha.

Wapo watu wanaotufanya tukumbuke kuwa kuna maombi na kufunga. Kuna wakati unafika unasema: β€œEe Mungu, hii ni nini tena?” Na Mungu anakujibu: β€œBila hao usingenitafuta kwa bidii, usingeomba kwa kina, usingejifunza hekima ya kuishi na watu.”

Ni lazima tukutane na watu wa aina tofauti ili tabia, imani, na ukuaji wetu wa kiroho uweze kukomaa.

Hata Yesu Kristo, akiwa Mwana wa Mungu, alikuwa na watu wa aina tofauti ndani ya timu yake. Lakini alijua namna ya kuishi nao, kuwaongoza, na kufanikisha kusudi lake pamoja nao hadi mwisho wa safari.

Kwa nini usome kitabu hiki cha: β€œAINA 12 ZA WATU WASUMBUFU KATIKA JAMII NA JINSI YA KUCHUKULIANA NAO”?

Kwa sababu hawa ni watu tunaokutana nao kila siku kazini, kanisani, kwenye biashara, kwenye mahusiano, hata ndani ya familia zetu. Mara nyingi kwa kutokuelewa tabia zao, tumedhani ni wachawi, mapepo, au wameinuliwa na adui dhidi yetu, kumbe ni aina fulani ya watu ambao hatujajifunza namna sahihi ya kuhusiana nao.

Kitabu hiki kitakupa: βœ… Maarifa ya kuelewa tabia za watu
βœ… Hekima ya kuishi nao kwa amani
βœ… Namna ya kujilinda kihisia na kiroho
βœ… Uwezo wa kujenga mahusiano bora katika jamii

πŸ“š AINA 12 ZA WATU WASUMBUFU KATIKA JAMII NA JINSI YA KUCHUKULIANA NAO
πŸ”₯ BEI YA OFFER: TSHS 20,000 TU
⚠️ ZIMEBAKI NAKALA CHACHE!

WCC β€” UPENDO NDIO PUMZI YETU
PATA MAARIFA, JENGA HEKIMA, ISHI KWA AMANI.

Mahusiano ya muhimu kuliko mahusiano mengine yote ni mahusiano yetu na Mungu.Hata hivyo, kabla ya kujenga mahusiano imar...
31/05/2026

Mahusiano ya muhimu kuliko mahusiano mengine yote ni mahusiano yetu na Mungu.

Hata hivyo, kabla ya kujenga mahusiano imara na Mungu, mwenzi wako, au watu wengine, kuna mahusiano ya kwanza yenye umuhimu mkubwa zaidi nayo ni mahusiano yako binafsi na wewe mwenyewe.

Mtu anayejitambua, anayejiheshimu, na mwenye amani ndani yake, huwa na uwezo mkubwa wa kujenga mahusiano yenye afya na Mungu pamoja na watu wengine.

George Luhui, WCC

Address

Mbezi Beach, Rafia Near Africana
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00
Saturday 08:00 - 16:00
Sunday 07:00 - 14:00

Telephone

+255713183939

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Warehouse Christian Center posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share