07/09/2026
TAARIFA YA SADAKA β KANDA YA DAR ES SALAAM NA PWANI
Jumapili, tarehe 06/09/2026, Kanda ya Dar es Salaam na Pwani ya Sadaka Yetu ilifanya tukio la kwenda kumtembelea na kumpa pole Mama Naomi, anayesihi Tabata Senene, Dar es Salaam.
Mama Naomi anakabiliwa na changamoto ya saratani ya kizazi, ambayo imefikia hatua ya mwisho. Kutokana na hali hiyo, kwa sasa hawezi kufanyiwa upasuaji, na anaendelea kupata matibabu maalum katika Taasisi ya Ocean Road kwa ajili ya kupunguza makali ya ugonjwa.
Mama Naomi anaendelea kuhudumiwa na binti yake wa pekee, Naomi, ambaye pia ni mwanasadaka mwenzetu kutoka Kanda ya Dar es Salaam na Pwani.
Baada ya kanda kupata taarifa kuhusu changamoto anayopitia mwanasadaka mwenzao katika kumhudumia mama yake, waliamua kumtembelea nyumbani kwao Tabata Senene kwa lengo la kumpa pole, kumfariji na kumtia moyo katika kipindi hiki kigumu.
Katika ziara hiyo, Kanda ya Dar es Salaam na Pwani ilifika ikiwa na mahitaji mbalimbali yenye thamani ya TZS 208,000/= (Laki Mbili na Elfu Nane) pamoja na mchango wa fedha taslimu wa TZS 150,000/= (Laki Moja na Elfu Hamsini).
Kwa pamoja, msaada huo ulikuwa na thamani ya jumla ya:
TZS 358,000/= (Laki Tatu na Elfu Hamsini na Nane).
Tunawapongeza na kuwashukuru wanasadaka wote walioshiriki katika jambo hili la upendo, faraja na utu. Mchango huu, pamoja na thamani yake, ni ishara ya kuwa hakuna mwanasadaka anayepaswa kupitia changamoto peke yake.
Tunaendelea kuamini katika nguvu ya upendo, mshikamano na kusaidiana katika nyakati za furaha na changamoto.
Mungu awabariki sana wote mliohusika na kuwaimarisha Mama Naomi na binti yake Naomi katika kipindi hiki.
!