Sadaka Yetu Group

Sadaka Yetu Group Huu ukurasa ni kwa ajili ya kuwasaidia wenzetu ambao hawana uwezo kifedha kuwawezesha kupata mitaji ya kuanzisha biashara ama kutatua changamoto wanazopitia.

Walengwa wakuu ni yatima, wajane, walemavu na wenye uhitaji maalum

Changia damu, okoa maisha 🩸Tone lako la damu linaweza kuwa sababu ya mtu mwingine kupata nafasi ya kuendelea kuishi. Tuj...
13/05/2026

Changia damu, okoa maisha 🩸
Tone lako la damu linaweza kuwa sababu ya mtu mwingine kupata nafasi ya kuendelea kuishi. Tujitokeze kwa pamoja kuonyesha upendo, utu na kujali jamii yetu❀️

Finally we are done. Mungu ambariki kila mmoja aliyegusa maisha ya dada huyu πŸ™πŸ½
12/05/2026

Finally we are done. Mungu ambariki kila mmoja aliyegusa maisha ya dada huyu πŸ™πŸ½

Tunapowapost mama zetu na mama wa watoto wetu kuwatakia heri katika siku yao (Mother's day) tusimsahau huyu mama anayepi...
10/05/2026

Tunapowapost mama zetu na mama wa watoto wetu kuwatakia heri katika siku yao (Mother's day) tusimsahau huyu mama anayepigania maisha yake kitandani. Watoto wake nao wanatamani angekua mzima wamtakie heri na kufurahi nae.

Mimi na wewe tuna nafasi ya kuokoa maisha yake. Gharama anazohitaji kwa ajili ya upasuaji ni TZS 4.5M. Familia yake imepambana na kupata 1.2M, na sisi hadi sasa tumeweza kumchangia 1.6M. Hivyo kwa ujumla tayari ana kiasi cha TZS 2.8M. Hivyo basi bado 1.7M tu ili aweze kufanyiwa upasuaji.

Muweke kwenye nafasi ya mama yako, dada yako au mkeo. Mwenye watoto wadogo wanaomtegemea lakini yupo kwenye hatari ya kupoteza maisha kwa kukosa 4.5M tu ya oparation.

Shiriki nasi kurudisha matumaini ya kuishi kwa dada Esteria M-PESA #0752581983, Tigopesa #0719744954, CRDB #0150633516500, NMB 24110012109 Gifted Hearts Foundation | RudishaTabasamu | LetLoveLead

Umaskini umeweka rehani maisha ya dada yetu. Tunaumia kuona anakufa na hatuna namna ya kumsaidia. Tunaomba msaada kuokoa...
10/05/2026

Umaskini umeweka rehani maisha ya dada yetu. Tunaumia kuona anakufa na hatuna namna ya kumsaidia. Tunaomba msaada kuokoa maisha ya dada yetu.” Ujumbe kutoka kwa mdogo wake Esteria ukiambatana na simu ya kilio.

Esteria Gabriel Tarimo mkazi wa Tarakea, Rombo alipata ajali ya pikipiki tar.03 Agosti 2024 na kuumia kichwani. Alivuja damu nyingi na kupoteza fahamu. Alikimbizwa Kituo cha Afya Karume na kupewa huduma ya kwanza, kisha kupewa rufaa kwenda hospitali ya wilaya.

Kutokana na hali yake alipewa ambulance na kukimbizwa hospitali ya kanda KCMC kujaribu kuokoa maisha yake. Vipimo vilionesha alipata majeraha makubwa kichwani ikiwemo fuvu lake lilipasuka na damu kuvuja ndani ya kichwa.

Alifanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa kwa haraka, ili kunusuru maisha yake. Upasuaji huo ulienda vizuri na akatoka theatre salama. Baada ya hali yake kutengemaa aliruhusiwa kurejea nyumbani.

Alihudhuria kliniki KCMC kwa ajili ya uangalizi na hali yake ilionekana kuimarika. Hata hivyo mwezi May 2025 hali yake ilibadilika akaanza kulalamika maumivu makali ya kichwa. Kuna wakati alianguka na kukak**aa k**a mtu mwenye degedege.

Baadaye ukajitokeza uvimbe sehemu yenye jeraha kichwani. Uvimbe huo ulianza polepole lakini uliongezeka kadri siku zilivyosogea. Alirudishwa KCMC na baada ya vipimo madaktari walishauri afanyiwe upasuaji kuondoa uvimbe huo kwa sababu hauwezi kupona kwa dawa.

Alitakiwa kufanyiwa upasuaji July 2025 lakini mpaka sasa hajafanyiwa, kwa sababu familia imeshindwa kumudu gharama ambazo ni TZS 4.5M. Kwa takribani mwaka mmoja sasa familia imeomba msaada kwa ndugu, jamaa na marafiki na kupata TZS 1.2M tu ambayo haifiki hata nusu ya gharama zinazohitajika. Kwa sasa matumaini ya kuokoa maisha ya dada yao yamefifia na ni k**a wamekata tamaa.

:
Leo ni siku ya akina mama duniani. Tudedicate siku hii kuokoa maisha ya mama huyu. Kwa sadaka zetu ndogo tunaweza kurudisha tena matumaini ya kuishi kwa Esteria ili naye apate neema ya kulea watoto wake. M-PESA #0752581983, Tigopesa #0719744954, CRDB #0150633516500, NMB #24110012109 Gifted Hearts Foundation | RudishaTabasamu | LetLoveLead

πŸ”₯ Jiandae kwa tukio la kihistoria ndani ya Jiji la Arusha πŸ”₯Get Together kubwa itakayowakutanisha wanasadaka @⁨all⁩  kuto...
09/05/2026

πŸ”₯ Jiandae kwa tukio la kihistoria ndani ya Jiji la Arusha πŸ”₯

Get Together kubwa itakayowakutanisha wanasadaka @⁨all⁩ kutoka sehemu mbalimbali za nchi kwa ajili ya kufahamiana, kubadilishana mawazo, kujifunza na kufurahia pamoja. 🀝

Usikose kuwa sehemu ya kumbukumbu hii ya kipekee ndani ya jiji la utalii na burudani.

Mimi nitakuwepo, wewe je? !

Mtag rafiki yako mmoja unatamani awepo kwenye Get Together Kanda ya Kaskazini.

Mzee huyu anaitwa Sudi, mkazi wa Mbezi Msumi, Dar es Salaam.Mzee Sudi aliachwa na mke wake ambaye alimkimbia na kumuachi...
08/05/2026

Mzee huyu anaitwa Sudi, mkazi wa Mbezi Msumi, Dar es Salaam.
Mzee Sudi aliachwa na mke wake ambaye alimkimbia na kumuachia watoto wawili. Kabla ya kuondoka, mke wake aliacha deni la Kausha Damu kiasi cha TZS 500,000/= (laki tano).

Mzee Sudi pia ana changamoto za kiafya. Kutokana na hali ngumu ya maisha, analazimika kutembea karibu kilomita 100 kwa siku β€” kutoka Msumi hadi Ilala Boma kufuata nguo za mitumba kwa miguu, kisha kuanza kuuza na kutembea nazo kutoka Ilala mpaka Msumi. Hali hiyo imesababisha kupata matatizo ya kiuno pamoja na changamoto nyingine za kiafya.

Kabla ya kufikisha taarifa hii hapa, uongozi ulifanya ziara kwa Mzee Sudi pamoja na baadhi ya WANASADAKA wa hapa ili kujionea mazingira anayoishi. Baada ya kuona hali halisi, mmoja wa WANASADAKA alitoa sadaka papo hapo kwa kumnunulia:
βœ… Godoro
βœ… Sare za watoto
βœ… Vyakula
Pia mwana sadaka huyo alipunguza deni la Mzee Sudi na kubakiza TZS 160,000/= (laki moja na elfu sitini). Kabla ya hapo, watu wa Kausha Damu walikuwa wakimtishia kuuza baadhi ya vitu vya ndani ili kufidia deni hilo lililoachwa na mke wake.

Baada ya uongozi kuona mazingira na hali halisi ya maisha ya Mzee Sudi, umeridhia kumwongezea mtaji wa TZS 200,000/=(Laki mbili) ili aweze kukuza biashara yake ya mitumba na kujikimu pamoja na watoto wake kupitia biashara hiyo.

Mzee Sudi ana umri wa miaka 60+.
(Tafadhali rudia kusoma tena simulizi ya maisha yake na namna anavyopambana kutafuta riziki licha ya umri wake na changamoto alizonazo.)

πŸ™ Mbarikiwe sana!

Uongozi wa Sadaka Yetu Kanda ya Pwani, ukihusisha mikoa ya Dar es Salaam na Pwani Region, ulifanya tukio maalum la kuwag...
27/04/2026

Uongozi wa Sadaka Yetu Kanda ya Pwani, ukihusisha mikoa ya Dar es Salaam na Pwani Region, ulifanya tukio maalum la kuwagusa watu wenye mahitaji maalum katika Mlandizi Vocational Center, kilichopo Mlandizi.

Tukio hilo lilifanyika tarehe 26/04/2026, ambapo ilikuwa ni siku ya furaha iliyojaa kucheza, kuimba, na kula pamoja na watoto.

Jumla ya mahitaji yenye thamani ya TZS 661,500/= (laki sita elfu sitini na moja na mia tano) yaliwasilishwa katika kituo hicho, ikiwa ni sadaka maalum kutoka kwa wanachama wa Kanda ya Pwani.

Uongozi wa kituo hicho ulitoa shukrani za dhati kwa shughuli zinazofanywa na Sadaka Yetu, na pia kuendelea kutuombea na kututia moyo ili tuendelee kuwagusa wenye uhitaji.

Mbarikiwe sana Kanda ya Pwani!

Kwa nini tukio la Get Together limepewa siku ya kihistoria ndani ya Jiji la Arusha?Ni siku ambayo wanafamilia wa Sadaka ...
25/04/2026

Kwa nini tukio la Get Together limepewa siku ya kihistoria ndani ya Jiji la Arusha?

Ni siku ambayo wanafamilia wa Sadaka Yetu watashiriki katika matukio makubwa matatu yenye kugusa maisha ya watu moja kwa moja:
1. Kuwatembelea watoto njiti kuwapatia mahitaji – Mount Meru Hospital
2. Kuchangia damu – Mount Meru Hospital
3. Get Together – Orlando Garden, Sakina – Arusha

Matukio yote yatafanyika tarehe 05-07-2026.
Usipange kukosa.

Kanda ya Kaskazini iko tayari kuwapokea na kuwakarimu wageni wote kutoka sehemu mbalimbali.

Jipatie kofia kali za Sadaka Yetu kwa gharama nafuu ya TZS 10,000/=.Usambazaji utafanyika katika mikoa yote ya Tanzania,...
24/04/2026

Jipatie kofia kali za Sadaka Yetu kwa gharama nafuu ya TZS 10,000/=.

Usambazaji utafanyika katika mikoa yote ya Tanzania, mahali popote Sadaka Yetu ilipo, na zitawafikia wahusika.

Booking kwa wahitaji itafanyika kwa kufanya malipo kupitia uongozi wa kanda, ambao pia utakupatia tisheti na kofia yako. Hivyo, zoezi hili litafanyika kwenye group za kanda pekee na si hapa. Utachagua rangi na size yako.

Sample ya tisheti ni hizi hapa chini πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Mbarikiwe sana!

+255744176828

TAARIFA!Tayari tumetoa oda ya tisheti na kofia za Sadaka Yetu, na kwa sasa zinaendelea kutengenezwa. Tisheti na kofia hi...
24/04/2026

TAARIFA!

Tayari tumetoa oda ya tisheti na kofia za Sadaka Yetu, na kwa sasa zinaendelea kutengenezwa. Tisheti na kofia hizi zitakuwa nembo na utambulisho wa Mwana Sadaka wanapokutana kikanda na kushiriki katika matukio mbalimbali ya kuwasaidia wahitaji.

Tunazo rangi mbili tu: nyeusi na nyeupe. Tisheti zote ni Form Six.

Bei elekezi ya uongozi:
Tisheti: TZS 20,000/=
Kofia: TZS 10,000/=

Usambazaji utafanyika katika mikoa yote ya Tanzania, mahali popote Sadaka Yetu ilipo, na zitawafikia wahusika.

Booking kwa wahitaji itafanyika kwa kufanya malipo kupitia uongozi wa kanda, ambao pia utakupatia tisheti na kofia yako. Hivyo, zoezi hili litafanyika kwenye group za kanda pekee na si hapa. Utachagua rangi na size yako.

Sample ya tisheti ni hizi hapa chini πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Mbarikiwe sana!

+255744176828

YETU KWA AJILI YA WENGINE!

SADAKA YETU kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa Damu Salama wameandaa zoezi maalum la kuchangia damu.Tunakualika ushi...
23/04/2026

SADAKA YETU kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa Damu Salama wameandaa zoezi maalum la kuchangia damu.
Tunakualika ushiriki nasi katika tendo hili la upendo na ubinadamu la kuokoa maisha ya wengine. Damu yako inaweza kuwa tumaini la uhai kwa mtu anayehitaji msaada wa haraka.

Tukio hili la kipekee litafanyika katika Mount Meru Regional Referral Hospital tarehe 05-07-2026, kuanzia saa tatu asubuhi.

Kwa maelezo zaidi na ushiriki, wasiliana nasi kupitia: 0755-559013

Karibu tushirikiane kuokoa maisha.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255755559013

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sadaka Yetu Group posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share