HakiElimu

HakiElimu Our non-profit organisation strives for an open, just and democratic society with quality education.

01/06/2026

Huwezi kusaidia changamoto ya mtoto usiyoijua!

Karibu kutazma video hii fupi sasa hivi uone ni kwa nini utambuzi na upimaji wa mapema kupitia vituo vya ESRAC ndio ufunguo wa kuokoa mustakabali wa watoto wetu.

01/06/2026

📍 Mbeya, Green City! Simu Yenu Imepokelewa!

Tukutane 03 Juni 2026. Viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge, Soweto kuanzia saa 3:00 Asubuhi.

Ungana nasi katika safari hii muhimu ya kuweka msingi thabiti wa maisha ya baadaye ya watoto wetu.

Maendeleo yanaanza na hatua moja, na hatua hiyo inaanzia Mbeya keshokutwa!

Karibuni nyote!

Je, wewe ni mwandishi wa habari kutoka Tabora, Manyara, Tanga, Dodoma, Mtwara au Kagera?Ulipitwa na muda wa kutuma maomb...
28/05/2026

Je, wewe ni mwandishi wa habari kutoka Tabora, Manyara, Tanga, Dodoma, Mtwara au Kagera?

Ulipitwa na muda wa kutuma maombi ya kushiriki Programu ya Uwezeshaji Waandishi wa Habari za Elimu 2026? Habari njema ni kwamba dirisha la maombi limefunguliwa tena!

Usikose nafasi hii ya kuwa sehemu ya safari ya kujifunza, kukuza uwezo na kufanya mabadiliko kupitia uandishi wa habari za elimu.

📩 Tuma maombi yako sasa na jiunge nasi katika programu hii muhimu.

Mwisho wa kupokea maombi: 05 Juni 2026

Je, wewe ni mwandishi wa habari mwenye mapenzi na ari ya kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu nchini? HakiElimu inaku...
19/05/2026

Je, wewe ni mwandishi wa habari mwenye mapenzi na ari ya kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu nchini?

HakiElimu inakukaribisha kutuma maombi ya kushiriki katika Programu ya Uwezeshaji Waandishi wa Habari za Elimu kwa mwaka 2026!.

Programu hii inalenga kuwawezesha waandishi kuandaa habari na simulizi zenye mguso kutoka ngazi ya jamii zikionesha uhalisia wa maisha ya watoto, wazazi, walimu, na wadau wa elimu, hususan kutoka makundi yaliyoko kwenye mazingira hatarishi au yaliyotengwa.

SIFA ZA MWOMBAJI:

1️⃣ Awe na Ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB).

2️⃣ Uzoefu katika vyombo vya habari (Magazeti, Redio, Televisheni, au Majukwaa ya Kidigitali).

3️⃣ Uzoefu au hamasa katika kuandika masuala ya elimu, usawa wa kijinsia, na haki za kijamii.

4️⃣Ushirikiano na chombo cha habari au uthibitisho wa mahali kazi zake zitakapochapishwa/kutangazwa (kwa waandishi wa kujitegemea/freelancers).

FAIDA UTAKAZOPATA:

✅ Kufanya kazi bega kwa bega na wahariri wakongwe pamoja na wataalamu wa sera za elimu.

✅ Kushiriki kwenye warsha za mafunzo ya kina kuhusu Uandishi wa Habari za Takwimu (Data Journalism), Usimulizi wa Hadithi kwa Njia ya Dijiti (Multimedia Storytelling), na Sera za Elimu Jumuishi.

✅ Fursa ya kujiunga na Mtandao wa Wahitimu wa Programu hii (Post-Fellowship Alumni Network).

JINSI YA KUTUMA MAOMBI:

Tuma nyaraka zifuatazo kupitia barua pepe: [email protected]

✅Wasifu wako binafsi (CV) usiozidi kurasa 2.

✅Nakala ya kitambulisho cha Ithibati ya JAB na barua ya mdhamini kutoka chombo cha habari au jukwaa litakalochapisha/kutangaza kazi zako.

✅Viunganishi (links) 3 ya habari zako zilizochapishwa/kutangazwa (kipaumbele kitatolewa kwa habari za elimu).

MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI: 25 Mei 2026.

Je, unajua kuwa takribani Sh. Bilioni 2.68 za ruzuku ya elimu hazikufika shuleni? Katika mwaka wa fedha 2024/25, uchambu...
18/05/2026

Je, unajua kuwa takribani Sh. Bilioni 2.68 za ruzuku ya elimu hazikufika shuleni?

Katika mwaka wa fedha 2024/25, uchambuzi unaonesha kuwa shule katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) tisa (9) nchini hazikupata kiasi hiki cha fedha kati ya Sh. Bilioni 13.46 zilizohitajika. Hii ni sawa na kusema shule zinashindwa kujiendesha kikamilifu.

Miongozo ya matumizi ya fedha za ruzuku ya uendeshaji wa shule za msingi na sekondari inaelekeza kuwa, kila mwanafunzi wa shule ya msingi anapaswa kupata Sh. 10,000 na wa sekondari Sh. 25,000 kwa mwaka. Fedha hizi zinatakiwa kwenda shuleni moja kwa moja ili kuepuka urasimu na ucheleweshaji.

Kutotolewa kwa fedha hizi kunaathiri wanafunzi kitaaluma kwa kuwa uendeshaji wa shule unategemea ruzuku ya elimu bila malipo. Fedha hizi huziwezesha shule kupata rasilimali muhimu k**a vile vifaa vya kufundishia na kujifunzia ambavyo vinanachangia katika utoaji wa elimu bora.

Je, umeona athari gani za kuchelewa kwa ruzuku kwenye shule ya mtaani kwako?
Karibu tujadiliane. 👇

Tunayofuraha kuwapokea wanafunzi kutoka Chuo Kishiriki cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) waliofika katik...
14/05/2026

Tunayofuraha kuwapokea wanafunzi kutoka Chuo Kishiriki cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) waliofika katika ofisi za HakiElimu kujifunza kwa undani mchakato mzima wa Uandaaji, Utekelezaji na Tathmini ya Mitaala ya elimu nchini.

Tunaamini katika kuwajengea uwezo walimu watarajiwa ili waweze kuleta mabadiliko chanya kwenye sekta ya elimu nchini.

HakiElimu is looking for a reputable and experienced firm to provide internal audit services for the 2026 fiscal year. W...
13/05/2026

HakiElimu is looking for a reputable and experienced firm to provide internal audit services for the 2026 fiscal year. We are looking for partners committed to excellence and transparency to help strengthen our organizational impact.

Key Details:

o Duration: One year (Renewable based on performance).

o Application Deadline: 22nd May 2026.

Download the full Terms of Reference (ToR) here: https://shorturl.at/Cu2SE

Je, unajua kuwa takribani shule 2,072 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) 26 nchini bado hazijahamia kwenye matumi...
08/05/2026

Je, unajua kuwa takribani shule 2,072 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) 26 nchini bado hazijahamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia?

Ripoti ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ya Machi 2026 imebaini kuwa shule hizi (zenye wanafunzi zaidi ya 100) zinaendelea kutumia kuni na mkaa, jambo ambalo lilipigwa marufuku tangu Januari 2024.

Je, Unafikiri nini kinakwamisha shule hizi kutumia nishati safi? Karibu tujadili.

Bajeti ya Elimu 2026/27: Je, Tanzania Imejipanga kwa Dira 2050?Elimu ndiyo msingi wa kufanikisha Dira ya Taifa 2050! Kue...
05/05/2026

Bajeti ya Elimu 2026/27: Je, Tanzania Imejipanga kwa Dira 2050?

Elimu ndiyo msingi wa kufanikisha Dira ya Taifa 2050! Kuelekea Bajeti ya 2026/27, HakiElimu imetoa mapendekezo sita ya kisera ili kusaidia mipango na bajeti ya sekta ya elimu kuwiana na matarajio ya kitaifa tangu mwanzo, mapendekezo haya yanalenga kuleta mageuzi yatakayotuvusha kuelekea maisha bora na jamii ya kidijitali.

Mambo 6 ya kimkakati tuliyoyapendekeza:

1️⃣ Uwekezaji wa Teknolojia (STI): Serikali iongeze bajeti ya Sayansi na Teknolojia kutoka Tsh Bilioni 92.1 hadi kufikia walau 0.5% ya Pato la Taifa (Tsh Trilioni 1.02) kwa kuzingatia pato la taifa la mwaka 2024.

2️⃣ Mkakati wa Mtaala Mpya: Kutokana na ongezeko la wahitimu wa mkupuo (Double Cohort) watakaojiunga na kidato cha kwanza mwaka 2028, ni muhimu kwa Serikali kutenga Shilingi trilioni 2.12 kuanzia sasa. Fedha hizi zitawezesha ujenzi wa miundombinu ya madarasa, maabara, vyoo, pamoja na ajira kwa walimu wapya wa sekondari ili kukabiliana na ongezeko hilo.

3️⃣ Ulinzi wa Mtoto: Kuanzishwa kwa fungu maalumu la bajeti kwa ajili ya "Ulinzi na Usalama wa Mtoto Shuleni" ili kutokomeza ukatili.

4️⃣ Stadi za Msingi (K*K): Kuboresha uwiano wa mwalimu kwa mwanafunzi katika elimu ya awali kwa kuajiri walimu waliobobea ili kuboresha uwiano kutoka 1:151 hadi 1:45 ili kuhakikisha watoto wanajua kusoma, kuandika na kuhesabu mapema.

5️⃣ Elimu Jumuishi: Kutenga bajeti maalumu kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Utambuzi na Upimaji wa Awali wa Mtoto (ESRAC) katika halmashauri 148 zilizosalia.

6️⃣ Maji na Usafi (WASH): Kutenga fedha za matengenezo ya miundombinu ya maji shuleni ili kufikia agizo la serikali la kuhakikisha shule zote zinakuwa na maji ifikapo mwaka 2027.

Tembelea www.hakielimu.or.tz/publications au bofya kiunganishi https://shorturl.at/wDAxi kusoma tamko hili kwa undani zaidi.

Jasho la leo ndio faraja ya kesho. Heri ya sikukuu ya
30/04/2026

Jasho la leo ndio faraja ya kesho. Heri ya sikukuu ya

Address

Upanga
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:30
Tuesday 08:00 - 16:30
Wednesday 08:00 - 16:30
Thursday 08:00 - 16:30
Friday 08:00 - 14:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when HakiElimu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to HakiElimu:

Share