HakiElimu

HakiElimu Our non-profit organisation strives for an open, just and democratic society with quality education.

Binti si aibu ya kufichwa—ni ndoto inayopaswa kuchanua! 🌺Kupevuka si tiketi ya ndoa, ni fursa ya kusoma na kufikia maish...
29/08/2026

Binti si aibu ya kufichwa—ni ndoto inayopaswa kuchanua! 🌺

Kupevuka si tiketi ya ndoa, ni fursa ya kusoma na kufikia maisha anayoyatamani. Elimu ni haki yake, si hisani!

Ukiona binti anazuiwa kusoma au kutaka kuozwa, usinyamaze!. Ripoti mara moja Shuleni, Serikali ya Mtaa/Kijiji, au Dawati la Jinsia (Polisi) ili hatua stahiki zichukuliwe.

Tumlinde binti, tuokoe ndoto zake!

Through SAUTI ZETU project,  Elimu is supporting five partners to strengthen community-led accountability for better and...
25/08/2026

Through SAUTI ZETU project, Elimu is supporting five partners to strengthen community-led accountability for better and more inclusive education.

When communities actively participate in conversations about the changes they want to see, their experiences, voices and evidence can help shape more responsive and inclusive education systems.

At the 2nd East African Regional Education Conference, we are bringing these experiences to the regional conversation—sharing what is working, learning from others, and exploring how community voices can help move inclusive education from commitments to impact.

When communities are part of the conversations shaping the change, they want to see, systems can respond better.

HakiElimu inawatakia Waislamu na Watanzania wote Sikukuu Njema ya Maulid An-Nabi. Amani na baraka ziwe nanyi. Maulid Mub...
25/08/2026

HakiElimu inawatakia Waislamu na Watanzania wote Sikukuu Njema ya Maulid An-Nabi. Amani na baraka ziwe nanyi. Maulid Mubarak! 🌙✨

Tunawezaje kumsaidia mwanafunzi mwenzetu anapopewa adhabu iliyopitiliza? Swali hili kutoka kwa mwanafunzi liliibua mjada...
19/08/2026

Tunawezaje kumsaidia mwanafunzi mwenzetu anapopewa adhabu iliyopitiliza?

Swali hili kutoka kwa mwanafunzi liliibua mjadala mzito wakati wa Mjadala wa Shule kwa Shule (Interschool Dialogue) uliofanyika katika wilaya za Babati Mji (Manyara) na Korogwe (Tanga).

Kupitia jukwaa hili, wanafunzi walipata fursa ya kukutana, kubadilishana mawazo, kujifunza kutoka kwa wenzao na kujadili kwa kina masuala ya ulinzi na usalama wa mtoto.

Wanafunzi walitaja adhabu ya viboko iliyopitiliza kuwa moja ya aina za ukatili wanazokutana nazo shuleni. Akijibu hoja hiyo, Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Bi. Elitruda Kashuku, aliwasisitiza wanafunzi kutumia sanduku la maoni la “Sauti Yangu” au kupiga namba 116 kutoa taarifa wanapokutana na vitendo vya ukatili dhidi yao au wenzao, ili waweze kupata msaada na hatua stahiki kuchukuliwa. Aidha, aliwakumbusha na kuwasisitiza walimu kuzingatia sheria na taratibu za utoaji wa adhabu kwa wanafunzi, ili kuhakikisha shule zinakuwa sehemu salama kwa kila mtoto kujifunza na kustawi.

Kupitia mijadala hii, tunaendelea kujenga sauti ya mtoto, kuimarisha ushiriki wa wanafunzi, na kuweka mazingira salama ya kujifunzia ambapo kila mtoto analindwa, anasikilizwa, anaheshimiwa, na anaweza kutoa taarifa bila hofu.

Mjadala huu umewezesha wanafunzi kutoka shule 10 za msingi na sekondari zinazotekeleza Mradi wa Mageuzi ya Usawa wa Kijinsia katika Elimu (MMUKE/GET) kuwa mabalozi wa ulinzi wa mtoto

K**a mzazi/mlezi au mdau wa elimu, unaona tunapaswa kufanya nini ili kuhakikisha nidhamu shuleni inalindwa bila kuwavunjia watoto haki zao au kuwafanyia ukatili? Tushirikishe mtazamo wako kwenye maoni!

17/08/2026

Have a passion for storytelling? We want to hear from you. Apply now!.
13/08/2026

Have a passion for storytelling? We want to hear from you. Apply now!.

Tunawatakia Watanzania wote heri ya Sikukuu ya Nanenane 8.8.2026
08/08/2026

Tunawatakia Watanzania wote heri ya Sikukuu ya Nanenane 8.8.2026

Every child deserves a safe place to learn. Moments from the official launch of the Safe to Learn (STL) Diagnostic Repor...
28/07/2026

Every child deserves a safe place to learn.

Moments from the official launch of the Safe to Learn (STL) Diagnostic Report during the ARISE Africa II Convening at the African Union Headquarters in Addis Ababa, Ethiopia.

The launch brought together regional leaders, policymakers, and civil society organizations united by a shared mission: ending violence in and through schools across Africa.

📲 Tap the link in our bio to explore the key findings and recommendations!

📸 Highlights from the event ➡️

Mabadiliko ya kweli huanza pale tunapothubutu kuhoji yale tuliyozoea na kuyaamini. Mila ni sehemu ya utambulisho wetu, l...
25/07/2026

Mabadiliko ya kweli huanza pale tunapothubutu kuhoji yale tuliyozoea na kuyaamini.

Mila ni sehemu ya utambulisho wetu, lakini pale zinapogeuka chanzo cha maumivu na kuwanyima watoto haki zao zinahitaji kutazamwa upya.

Jamii yenye ustawi wa kweli ni ile inayochagua kulinda maisha na mustakabali wa watoto wake kuliko kuendeleza desturi zinazowaumiza.

Mabadiliko hayawezi kuletwa na mtu mmoja pekee. Hujengwa na jamii inayokubali kujifunza, kusikiliza, na kuchukua hatua za makusudi kwa manufaa ya watoto. 🤝

Kila mtoto anastahili kukua salama, kupata elimu, na kuandika hadithi ya maisha yake kwa matumaini si kwa hofu.

Sauti ya Mama Inaponyamaza, Ndoto ya Binti InazamaUkimya wa mama si ishara ya ridhaa; mara nyingi ni matokeo ya hofu, sh...
23/07/2026

Sauti ya Mama Inaponyamaza, Ndoto ya Binti Inazama

Ukimya wa mama si ishara ya ridhaa; mara nyingi ni matokeo ya hofu, shinikizo la kijamii na mifumo inayowanyima wanawake nafasi ya kushiriki katika maamuzi yanayogusa familia zao.

Mtoto wa k**e anahitaji sauti zinazomsimamia, si maamuzi yanayomuumiza. Ukeketaji na ndoa za utotoni si njia ya kumjengea maisha; ni vikwazo vinavyomnyima afya, elimu na fursa ya kufikia ndoto zake.

Jamii yenye usawa hujengwa pale kila sauti inapopewa thamani, na maamuzi yanapoweka mbele ustawi na maslahi ya mtoto kuliko mila zinazodhuru.

Kila mtoto ana haki ya kukua salama, kupata elimu na kutimiza ndoto zake. Kila mwanamke ana haki ya kushiriki katika maamuzi yanayogusa maisha ya watoto wake.

Address

Upanga
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:30
Tuesday 08:00 - 16:30
Wednesday 08:00 - 16:30
Thursday 08:00 - 16:30
Friday 08:00 - 14:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when HakiElimu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to HakiElimu:

Shortcuts

Share