19/05/2026
Je, wewe ni mwandishi wa habari mwenye mapenzi na ari ya kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu nchini?
HakiElimu inakukaribisha kutuma maombi ya kushiriki katika Programu ya Uwezeshaji Waandishi wa Habari za Elimu kwa mwaka 2026!.
Programu hii inalenga kuwawezesha waandishi kuandaa habari na simulizi zenye mguso kutoka ngazi ya jamii zikionesha uhalisia wa maisha ya watoto, wazazi, walimu, na wadau wa elimu, hususan kutoka makundi yaliyoko kwenye mazingira hatarishi au yaliyotengwa.
SIFA ZA MWOMBAJI:
1️⃣ Awe na Ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB).
2️⃣ Uzoefu katika vyombo vya habari (Magazeti, Redio, Televisheni, au Majukwaa ya Kidigitali).
3️⃣ Uzoefu au hamasa katika kuandika masuala ya elimu, usawa wa kijinsia, na haki za kijamii.
4️⃣Ushirikiano na chombo cha habari au uthibitisho wa mahali kazi zake zitakapochapishwa/kutangazwa (kwa waandishi wa kujitegemea/freelancers).
FAIDA UTAKAZOPATA:
✅ Kufanya kazi bega kwa bega na wahariri wakongwe pamoja na wataalamu wa sera za elimu.
✅ Kushiriki kwenye warsha za mafunzo ya kina kuhusu Uandishi wa Habari za Takwimu (Data Journalism), Usimulizi wa Hadithi kwa Njia ya Dijiti (Multimedia Storytelling), na Sera za Elimu Jumuishi.
✅ Fursa ya kujiunga na Mtandao wa Wahitimu wa Programu hii (Post-Fellowship Alumni Network).
JINSI YA KUTUMA MAOMBI:
Tuma nyaraka zifuatazo kupitia barua pepe: [email protected]
✅Wasifu wako binafsi (CV) usiozidi kurasa 2.
✅Nakala ya kitambulisho cha Ithibati ya JAB na barua ya mdhamini kutoka chombo cha habari au jukwaa litakalochapisha/kutangaza kazi zako.
✅Viunganishi (links) 3 ya habari zako zilizochapishwa/kutangazwa (kipaumbele kitatolewa kwa habari za elimu).
MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI: 25 Mei 2026.