RSA Tanzania

RSA Tanzania Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani Tanzania (Tanzani Road Safety Ambassadors) inashughulika na kuimarisha usalama barabarani kupitia elimu. Karibuni sana
(2)

Taasisi haitawajibika na maoni yanayokiuka sheria. KARIBU katika Mtandao wa Mabalozi wa Usalama Barabarani Tanzania. RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani. Motto wetu: "USALAMA BARABARANI NI HAKI NA JUKUMU LETU SOTE"

Kundi hili lilianzishwa 17.12.2013. Malengo ya kundi hili na RSA kwa ujumla ni:
1. Kufanya kazi k**a trafiki jamii kwa kuripo

ti matukio yote ya uvunjifu wa sheria za babarani.
2. Kutoa elimu kwa umma kuhusu usalama barabarani
3. Kuelimishan RSA kwa RSA kuhusiana na masuala mbalimbali yahusuyo usalama barabarani na bima
4. Kuwa chachu ya mabadiliko ya sera, sheria za usalama barabarani, mienendo na tabia za askari na madereva barabarani.
5. Kuwa mfano wa kuigwa(balozi) wa kutii bila shuruti sheria na taratibu za Usalama barabarani.
6. Kushirikishana uzoefu kutoka mahali mbalimbali duniani kuhusu usalama barabarani.
7. Kutumia jukwaa hili k**a sehemu ya kuuliza maswali, kujibu maswali, na kujadili masuala mbalimbali yahusuyo usalama barabarani.
8. Kupeana taarifa mbalimbali kuhusiana na usalama barabarani na hali ya barabara. Kundi hili lina makundi dada mengine yaliyopo whatsapp yanayoitwa RSA-KULIKONI BARABARANI. Admins wanayo haki ya kufuta post au maoni yoyote yanayokinzana na lengo la kundi. Katika kundi hili unashauriwa kutumia lugha ya staha katika kutoa malalamiko au kujenga hoja au kuuliza swali. Hapa tunabishana kwa hoja zenye ushahidi na sio siasa.

03/06/2026

ETI UNAONA UNAKARIBIA KUPISHANA NA GARI JINGINE UNAPUNGUZA MWANGA, UKIMKARIBIA KABISA UNAMWASHIA FULL, NDIO NINI? ILI IWEJE?

03/06/2026

HATA WEWE DEREVA UKISHUKA KWENYE USUKANI NI MWENDA KWA MIGUU, HIVYO HESHIMU WAENDA KWA MIGUU KWENYE ZEBRA

03/06/2026

Fahamu kuwa KUWAPIGIA HONI WANAOVUKA KWENYE ZEBRA WAVUKE HARAKA NI KOSA KISHERIA

03/06/2026

UNAYETUMIA "FULL" BARABARANI FAHAMU KWAMBA WEWE UNAFURAHI KUONA VIZURI, ILA WENZIO WANAPATA TABU KUONA

Ndugu DerevaSheria ya Usalama barabarani kupitia kifungu chake cha 78(10) inataka usimame nyuma kidogo ya eneo la kuvuki...
03/06/2026

Ndugu Dereva
Sheria ya Usalama barabarani kupitia kifungu chake cha 78(10) inataka usimame nyuma kidogo ya eneo la kuvukia (zebra) ili kumpisha mtu yeyote anayevuka au anayekusudia kuvuka barabara. Sheria hiyo haijasema hadi watu waonataka kuvuka wawe kikundi, bali ni kuanzia mtu mmoja na kuendelea. Kwa mantiki hiyo, ufikapo eneo lenye kivuko cha waenda kwa miguu, ama kwa kiingereza *pedestrian crossing* au maarufu k**a *ZEBRA*, basi hata k**a ni mtu mmoja anataka kuvuka simama mpishe avuke, tena wala usimpigie honi za kumtisha tisha au kupiga piga resi kumharakisha avuke.
Nimepata kushuhudia baadhi ya madereva wakionesha kukasirika pale ambapo watu wameingi barabarani na kulazimisha kuvuka baada ya kuona magari hayasimami. Kuna siku nimepata kushuhudia boda boda mmoja akipita kwa kasi mbele ya watu waliokuwa wanavuka kwenye zebra pale Kibamba sokoni halafu akageuka nyuma na kuanza kuwatukana wavukaji. Nilijisemea moyoni tu kuwa huyu hastahili kuwepo barabarani. Halafu pia kuna wale madereva ambao dereva wa mbele akisimama kupisha watu wavuke, wenyewe huku nyuma wanaanza kupiga honi nyingi za kero kumlazimisha yule dereva wa mbele aendelee kuendesha. Huku na kwenyewe ni kutojitambua, ni aina nyingine ya upunguani barabarani.
Kumbuka kwenye zebra ndio mahali pekee barabarani ambapo mwenda kwa miguu amepewa haki ya kuvuka barabara. Pale ndio eneo lake la kujidai. Lakini *dereva usisahau kuwa na wewe na familia yako pia ni waenda kwa miguu*, ukishuka kwenye gari unafikaje kwako si unatembea kwa miguu na wewe? Je, madereva wasipokuwa wanakupisha wewe au mwanao avuke unajisikiaje?
Mwelimishe na mwenzio

RSAadmin1
RSA Tanzania
Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote.

HIVI HAWA NDIO MNAWAITA "WAKONGWE" HUMU NDANI. NDIO MNASEMA HAWATAKIWI KWENDA SHULE HATA ZA REFRESHER TU, SABABU WAKONGW...
02/06/2026

HIVI HAWA NDIO MNAWAITA "WAKONGWE" HUMU NDANI. NDIO MNASEMA HAWATAKIWI KWENDA SHULE HATA ZA REFRESHER TU, SABABU WAKONGWE?
Na wengi mnaoongiza kwa kuandika andika shombo humu ni wa umri wa hawa jamaa.

*TAARIFA* Mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Mtwara kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali leo tarehe 31/05/2026 tulib...
02/06/2026

*TAARIFA*

Mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Mtwara kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali leo tarehe 31/05/2026 tulibahatika kufanya matendo ya huruma ya kuwaona wagonjwa katika hospital ya Rufaa LIGULA.

Katika ibada hiyo tuliweza kutembelea wodi zote na kuwaona wagonjwa mbali mbali wapatao sabini na tano (75) na kuweza kuwalipia wagonjwa wawili ambao walisharuhusiwa kutoka tangu tarehe 28/05/2026 na kushindwa kuondoka kutokana na kushindwa kulipa rasilimali fedha.

Uongozi wa hospital ya Ligula unatoa shukrani za dhati kabisa kwa kitendo hiki tulichokifanya leo kwa kuwagusa wagonjwa kwa namna moja ama nyengine na kutuomba tuwe tunawatembelea wagonjwa kwan wakituona kwao pia ni faraja.

Pia uongozi wa RSA mkoa wa mtwara unatoa shukrani kwa wadau mbalimbali walioweza kufanikisha ibada hii.

*imetolewa na uongozi rsa mkoa wa mtwara*

*USALAMA BARABARANI NI JUKUMU LETU SOTE*

https://tanzaniapanorama.com/?p=10563
02/06/2026

https://tanzaniapanorama.com/?p=10563

Katika kuendelea kutekeleza kampeni ya Commit to Act 2026, Shirika la Road Safety Ambassadors of Tanzania (RSA Tanzania) hivi karibuni lilifanya ziara maalum

02/06/2026

BAADHI YA ASKARI ACHENI MAKOSA YA KUTAFTIZA, MTU AU GARI YENYE MAKOSA MAKOSA YAKE YANAONEKANA WAZI KABISA

Address

Road Safety Ambassadors Of Tanzania
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when RSA Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to RSA Tanzania:

Share