IDC TZ

IDC TZ Inclusive Development for Citizens is a formal registered NGO with directed efforts towards active i

Uhamishaji wa EACOP umesababisha kukosekana kwa huduma muhimu za kijamii. Baada ya watu kuhamishwa, baadhi walijikuta wa...
08/06/2026

Uhamishaji wa EACOP umesababisha kukosekana kwa huduma muhimu za kijamii. Baada ya watu kuhamishwa, baadhi walijikuta wakiishi maeneo ambayo hayana shule, zahanati, au huduma za maji safi. Hili limeongeza gharama za maisha na kuathiri hasa watoto na wazee
Kukosekana kwa ushirikishwaji wa jamii kwenye maamuzi huzua hasira na uasi. Wananchi wengi hawakushirikishwa kikamilifu katika hatua za maamuzi kuhusu ardhi yao kupisha mradi wa EACOP

Taifa lisilo na demokrasia linakumbwa na matatizo mengi k**a ukandamizaji, rushwa, migogoro na umaskini. Ni wajibu wa ki...
08/06/2026

Taifa lisilo na demokrasia linakumbwa na matatizo mengi k**a ukandamizaji, rushwa, migogoro na umaskini. Ni wajibu wa kila raia kushiriki, kuitetea na kuilinda demokrasia kwa ajili ya sasa na vizazi vijavyo
Uchaguzi ni nyenzo muhimu ya kuwapa wananchi nafasi ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa njia ya haki, huru na ya wazi. Katika mfumo wa demokrasia, uchaguzi unatoa jukwaa kwa raia kushiriki mchakato wa maamuzi ya kitaifa na kuwawajibisha viongozi

Chaguzi zinazofanyika kwa sasa  hazihakisi demokrasia ya vyama vingi bali kuibeba CCM na makada wake hili waendelee kuta...
07/06/2026

Chaguzi zinazofanyika kwa sasa hazihakisi demokrasia ya vyama vingi bali kuibeba CCM na makada wake hili waendelee kutawala kwa namna wanavyojisikia au furahi wao k**a chama na sio kwa maslahi ya nchi.
Mfumo wa uchaguzi wa sasa ni wa kupandikiza watawala wanatumia kila mbinu kuhakikisha tunaingia kwenye chaguzi na sheria mbovu zaidi kila mara, ni wajibu wa wananchi kupata hili kuondokana na ukoloni huu

Fidia hazikuzingatia  thamani ya ardhi imesababisha umaskini,EACOP haikuzingatia athari za muda mrefu. Baadhi walilipwa ...
07/06/2026

Fidia hazikuzingatia thamani ya ardhi imesababisha umaskini,EACOP haikuzingatia athari za muda mrefu. Baadhi walilipwa fidia ndogo, wakashindwa kuwekeza kwenye maisha mapya, hatimaye kuingia kwenye umaskini.
Katika jamii nyingi za Kitanzania, wanawake hawamiliki ardhi moja kwa moja, hivyo fidia hulipwa kwa wanaume. Hali hii huwafanya wanawake na watoto kuwa waathirika wakuu wa ukosefu wa makazi, kipato na huduma za msingi

K**a CCM  wanakwamisha   , Wananchi tunaweza tumia njia nyigine za  kidemokrasia hasa nguvu ya umma kupata katiba ya wan...
06/06/2026

K**a CCM wanakwamisha , Wananchi tunaweza tumia njia nyigine za kidemokrasia hasa nguvu ya umma kupata katiba ya wananchi. Moja ya Hamasa ya wananchi ni kupata Katiba bora hili kukomesha tabia ya mamlaka kuvunja haki za binadamu na ufisadi ?
Wananchi wana hamasa ya kuona nchi inarudishwa mikononi mwao ili kunufaika na maliasili za Taifa na kulinda haki zao

Uhamishaji wa famili akwa ajili ya EACOP umevuruga sana  maisha ya kijamii na kiutamaduni. Familia nyingi zilizohamishwa...
06/06/2026

Uhamishaji wa famili akwa ajili ya EACOP umevuruga sana maisha ya kijamii na kiutamaduni. Familia nyingi zilizohamishwa kutoka maeneo yao ya asili zimepoteza mazingira ya kijamii, historia ya ukoo, na utambulisho wa kitamaduni.
EACOP imesababisha Kutengwa kwa familia kutoka ardhi waliyoizoea kunasababisha kuporomoka kwa mifumo ya maisha ya kijamaa, k**a desturi za usaidianaji na mila za kijamii, hali inayosababisha mtafaruku wa kijamii na kiakili

Mazingira ni urithi wa vizazi vijavyo. Misitu, mbuga na vyanzo vya maji si vya kizazi cha sasa pekee. Uharibifu wake una...
05/06/2026

Mazingira ni urithi wa vizazi vijavyo. Misitu, mbuga na vyanzo vya maji si vya kizazi cha sasa pekee. Uharibifu wake unaweza kuwa mzigo kwa watoto na wajukuu.
Mabadiliko ya tabianchi yanaongezeka kutokana na mafuta. Miradi ya mafuta huongeza hewa chafuzi zinazochangia ongezeko la joto duniani, ukame na mafuriko yanayoathiri kilimo.

Je ni  mambo gani  tunayodai yabadilishwa kwa  hili  Tuweze kuwa na nchi yenye katiba inayozingatia  haki, utu na uwajib...
05/06/2026

Je ni mambo gani tunayodai yabadilishwa kwa hili Tuweze kuwa na nchi yenye katiba inayozingatia haki, utu na uwajibikaji? Nguvu ya umma itasaidia kudai ambayo itajenga mifumo bora ya Uchaguzi hivyo wananchi kupata nguvu kuweka madarakani viongozi wanaotoka na kura. Tunapataje Nguvu ya umma ?

Ardhi yenye rutuba na maji safi ni muhimu kwa uzalishaji wa chakula. Miradi inayoharibu mazingira inaweza kusababisha nj...
04/06/2026

Ardhi yenye rutuba na maji safi ni muhimu kwa uzalishaji wa chakula. Miradi inayoharibu mazingira inaweza kusababisha njaa au kupanda kwa gharama za chakula, kwenye maeneo ya vijijini kutokana mpango duni wa mradi kuamisha wanakijiji

Utalii huzalisha ajira nyingi zisizo za kitaalamu pekee mfano Waongoza watalii, madereva, wapishi, wauza vinyago, hoteli na wafanyakazi wa usafiri wote hunufaika kupitia mazingira yaliyohifadhiwa vizuri. Baadhi ya mazingira yanaharibiwa na mradi wa EACOP

Mafuta ni rasilimali inayokwisha, mazingira yanaweza kudumu milele. Mafuta yakisha, mradi huisha. Lakini misitu, maziwa na ardhi vinaweza kuendelea kutoa faida kwa karne nyingi ikiwa vitalindwa.
Uchafuzi wa mafuta utaharibu vyanzo vya maji. Endapo kutatokea uvujaji wa mafuta, mito na visima vinaweza kuathirika, jambo litakalogusa afya ya wananchi, mifugo na kilimo.

Utalii huongeza biashara nyingi hata biashara ndogo ndogo k**a Mama lishe, mafundi, wauza bidhaa za asili na wasanii hunufaika na watalii kwa kiwango kikubwa kuliko miradi ya muda mfupi ya ujenzi.

Nini ulichoelewa kuhusu hii katuni ?
04/06/2026

Nini ulichoelewa kuhusu hii katuni ?

Address

Kinondoni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:30 - 17:00
Tuesday 08:30 - 17:00
Wednesday 08:30 - 17:00
Thursday 08:30 - 17:00
Friday 08:30 - 17:00
Saturday 09:00 - 14:00

Telephone

+255222198073

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IDC TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share