20/10/2024
(Pichani; Majid Pembe kushoto na Muddyb kulia, mnamo tarehe 29 Julai, 2023โVingunguti barabarani).
MSIBA KIWALANI.
____________________
Kiwalani ina wenyewe. Ukitaka kutaja wenyewe, huwezi kumuweka kando larger than life Majid the big Pembe katika kipengele hicho. Majid ni taswira ya upendo bila rika.
Nikiwa kijalunga, nilikuwa nikhimwona sana pale kwa Rehema Mgeni akipata masanga. Ni ndoa ya milele baina yao na masanga. Utamwita, ataitika ataulizia hali yako bila kujali umri wako. Pengine angejitenga na sisi vijana wadogo wa enzi hizo. Hapana! Hakuwa hivyo.
Majid ni mshikaji wa kila mtu. Mchizi fulani anayependeka. Simba mwana saaanaaa! Aliipenda hadi kuwa mwenyekiti wake. Pandikizi la baba. Kila ukimwona ananing'iniza tabasamu usoni pake. Aisee! Jamaa fulani hivi ambalo ukikaa nalo linatema madini.
Majid! Aaah mshikaji!
Vijana tulifurahi sana ulipoingia katika ulingo wa siasa. Enzi zako ukiwa mwenyekiti, ukilitimba wa pesa za barua ulikufa. Ulikufa jumla. Kila mmoja alipenda huduma yako. CHAUSTA! Majid k**a mwenyekiti. Hupishani sana Madenge wa Minazi Mirefu. Ni watu wenye upendo.
Ila sasa, wema kubaki duniani ni ahadi ambayo haiwezi kutekelezeka. Majid we mzee umeumwa na kufa ghafla. Matendo haya mawili yamefuatana upesi sana. Sisi wana Kiwalani tunalia sana kuondoka kwako. Bado tulihitaji upendo na ucheshi wako.
Majid daah! Majid weh!
RIP Big brother!