18/08/2026
GenZERO Sicklecell 2050 GenZero Sickle Cell 2025 Tanzania ya Ruge Mutahaba Foundation π₯π¨ππ π π¨π§πππππ ππ’π¨π‘πππ§ππ’π‘ imesaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na KAI, Kesho Angavu Initiative Kesho Angavu Initiative , kwa ajili ya kutoa elimu ya Siko Seli ikiambatana na upimaji wa hiari wa vinasaba, mapema kabla ya maamuzi ya ndoa na uzazi.
Hesabu ni simpo. Wazazi wawili wenye kinasaba cha Siko Seli, kila mimba ina uwezekano wa asilimia 25 wa mtoto kuzaliwa na ugonjwa wa Siko Seli. Lengo la MoU hii ni kuhakikisha hesabu hiyo inajulikana kabla haijatokea. Ndiyo maana Siko Seli inazuilika, kwa sababu inatabirika.
Kabla ya kurasimisha ushirikiano huu, GenZERO na KAI tumeshafanya kazi pamoja katika matukio 3, ambapo vijana 286 walipima vinasaba vyao baada ya kupata elimu sahihi. Mkataba huu haukuanza kwenye karatasi, bali kwenye utekelezaji ambao umezaa dhamira ya kuwafikia vijana 3,000 kwa mwaka 2026/27.
Sasa KAI rasmi ni GenZERO Komando πͺπΎ
GenZERO Komando si cheo cha heshima peke yake. Ni jina la yeyote anayechukua hatua tatu: kujifunza, kupima, na kisha kuiongoza jamii yake kufanya vivyo hivyo. Ni watu na taasisi wanaobeba ujumbe huu kwenye jamii zai wenyewe. KAI wamefanya hivyo, na sasa wanaelekea kufikia lengo muhimu la vijana 1,000 wa kwanza, itakayowapatia tuzo ya heshima.
Taasisi yako inataka kuwa GenZERO Komando? Tuandikie kupitia genzerosicklecell2050.tz
Kwa ushirikiano, elimu na hatua madhubuti, tunaweza kupunguza idadi ya watoto wanaozaliwa na Siko Seli ifikapo 2050.
GenZero Sickle Cell 2025 Tanzania
β¨ β¨