04/01/2026
MALEZI YA MTOTO NJITI BAADA YA MIEZI SITA
Malezi ya mtoto njiti yanahitaji umakini wa hali ya juu, hasa baada ya kufikisha miezi sita.
Kwanza, ni muhimu kuhakikisha mtoto anaendelea kupata multivitamin k**a alivyoelekezwa na mtaalamu wa afya.
Pili, mzazi ahakikishe mtoto anaendelea kwenda kliniki bila kukosa, na kufuatilia afya yake ikiwemo kufahamu uwingi wa damu (HB).
Katika diet, ni muhimu kuongeza vyakula vinavyoongeza damu k**a beetroot.
Mzazi anatakiwa kujua kuwa mtoto huanza kuhesabiwa miezi tangu anapozaliwa, hata k**a alizaliwa kabla ya muda (mtoto njiti).
Hairuhusiwi kumuanzisha mtoto chakula chochote kabla hajafikisha miezi sita, hata maji, kwa sababu maziwa ya mama yana zaidi ya asilimia 70 ya maji.
Baada ya miezi sita:
Wiki ya kwanza, anza na uji laini sana, huku ukizingatia kuangalia reaction yoyote itakayojitokeza mwilini mwa mtoto.
Baada ya hapo, mtoto anaanza kubadilishiwa chakula taratibu, na hii ni mifano ya vyakula vingine zaidi ya uji na mtori, k**a:
Boga lishe
Mtori/boko
Mboga za majani n.k.
Ni vyema kumbadilishia mtoto vyakula ili:
Asiboreke
Kuongeza hamu ya kuonja vyakula mbalimbali
Zingatia kutokuweka sukari nyingi wala chumvi nyingi kwenye chakula cha mtoto.
Epuka asali na maziwa ya ng’ombe kwa mtoto chini ya mwaka mmoja.
Nitaendelea kutoa mifano ya milo ya mtoto kidogo kidogo.
Dr. Idda Averil Luhanga (Mama Chuchi)
✨ Happy New Year ✨