11/05/2026
Mei 11, 2026 – Mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na Masafa Early Childhood Foundation umefanya kikao cha tathmini ya utekelezaji wa PJT-MMMAM kwa robo ya kwanza (Januari–Machi) katika Halmashauri ya Ubungo.
Kikao hiki kimewakutanisha maafisa kutoka idara mbalimbali zikiwemo Ustawi wa Jamii, Afya, Lishe, Elimu, Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto, Maendeleo na Mwandishi wa Habari Kinara.
Katika majadiliano hayo, washiriki walipitia maazimio na mikakati iliyowekwa katika kikao kilichopita, pamoja na kutathmini utekelezaji wake. Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni umuhimu wa kuimarisha ushirikiano baina ya idara, kushirikisha wadau kikamilifu, na kuendelea kutoa elimu jumuishi kwa jamii ili kuboresha ustawi wa mtoto na familia kwa ujumla.